wanawake ni zaidi ya....

by default

JF-Expert Member
Jul 11, 2011
839
215
Habari wana jf,katika family yetu tupo watoto wanne wakike 3 wakiume 1 na kwa baba mkubwa watoto wa ndoa wanne wote midume na mmoja wa nje ya ndoa wakiume(hapa nahsi alikuwa anatafuta wakike).
Mada ipo hapa kabla mama yangu ajafariki nilimuuliza mbona hauna ushirikiano na mke wa baba mkubwa simuoni akija kwenye harusi za dada zangu zaidi namuona baba mkubwa peke yake. Mama aliniambia ni story ndefu mke wa baba mkubwa alimkashfu sana alipokuwa akijifungua dada zangu (sorry) alikuwa anasema ameleta mambwa jike duniani so nilpozaliwa mimi mama alfarijika sana na akafunga kizaz. Kilichotokea katika familia ya baba mkubwa hadi sasa ana wajukuu 8 wakike na 2 wakiume na katika ao wajukuu wakike 3 ni micharuko kweli.
Juzi dada yangu amejifungua vipimo vilishaonesha atapata baby gal,yeye akawa anatamani baby boy baada ya kujifungua na kujua ni mtoto wa kike aligoma kumpokea kwa masaa kazaa.
Hivi kwa nini wanawake nyie wenyewe ampendani hadi mnaichukia jinsia yenu na kutupiana maneno makali kama haya. Na je kwa kitendo alichofanya dada yangu kinaweza kuja mwadhiri mtoto katika ukuwaji wake.
 
Hii dhana wakati mwingine huathiriwa na waume zao kwa maana mara nyingi wanaume hupenda watoto wa kiume ndio awe wa kwanza hivyo kwa mwanamke kupata mtoto wa kiume hudhani anaifikisha furaha katika familia yake ila hilo la kususia mtoto kwa masaa kadhaa ni dhahiri upendo hautokuwepo kwa asilimia mia hapo.
 
Suala si kutokupendana wanawake. Hapo ni suala binafsi la mtu na roho yake+preference yake..ambapo anahitaji kuchange. Mtoto ni mtoto,kama anamuona hafai aumbe wake au amrudishe alipomtoa!najua haiwezekani, so akubali matokeo. Haya masuala ya child preference yapo ktk jamii nyingi za kiAfrica.
Mama uyo,inabidi akubaliane na matokeo kuwa Mungu anapanga,.na kuhusu kumuathiri ktk ukuaji wake inategemea na atakavyomtreat akuapo. Ila ni suala la elimu binafsi ya uelewa na hofu ya Mungu,kuwa ye ndo mpangaji. Wote wanaochagua watoto,wanakosea sana.
 
Ingawa mimi siyo mtaalam wa mambo ya uzazi ila nasikia kwamba mbegu za mwanaume ndiyo zinaamua mtoto anayezaliwa awe ni wa jinsia gani na mwanamke hana mchango katika hilo.
 
mtoto ni mtoto tu jamani kwanza shukuru mungu kakupa huyo kuna wengine mimba wanazitafuta hawapati. Halafu wanaume wanaopenda watoto wakiume si watoe mbegu yy basi! mnachoka sana ndio maana mnaishia kutoa mbegu xx zinazopelekea mtoto wa kike. mama hahusiki ktk jinsia ya mtoto ni baba tu ndie sababu.
 
Ingawa mimi siyo mtaalam wa mambo ya uzazi ila nasikia kwamba mbegu za mwanaume ndiyo zinaamua mtoto anayezaliwa awe ni wa jinsia gani na mwanamke hana mchango katika hilo.

Ni kweli kabisa
 
dada yako anahitaji ushauri nasaa, hilo ni tatizo lake binafsi halihusu wanawake wote, especially wanapojifungua.....
 
Wakati niko 6 moons preg, nilifanya utra sound, Dr akaniambia ni baby gal nikashangilia kwa furaha; baadaye akasema 'wait ni wa kiume', nikanyweea saana. lakini l love my son mpaka basi ingawa nilitaka 1st born wangu awe wa kike.

Hivyo sio kweli kuwa wanawake hatupendi jinsi zetu; mimi ni living testimony.

kwa upande mwingine, jamii inamtazamo tofauti juu ya watoto wa kike; hivyo mama anapata pressure from outside na kwa vile ni assumption ya muda mrefu yeye mwenyewe keshaiamini.

Kuna mtu mmoja alisema "The greatest challenge is not to believe what people say about you" wahanga wa kubwa wa challenge hiyo ni wanawake.
 
Ingawa mimi siyo mtaalam wa mambo ya uzazi ila nasikia kwamba mbegu za mwanaume ndiyo zinaamua mtoto anayezaliwa awe ni wa jinsia gani na mwanamke hana mchango katika hilo.

you are totally wrong mkuu! Rejea elimu ya uzazi na usome mambo ya "XY" NA "X" Halafu uje kujisahihisha mwenyewe hapa!
 
you are totally wrong mkuu! Rejea elimu ya uzazi na usome mambo ya "XY" NA "X" Halafu uje kujisahihisha mwenyewe hapa!
Actually yuko sahihi. hakuna eggs zenye Y-chromosome, so mwanamke hawezi kudetermine jinsia ya mtoto

Ingawa mimi siyo mtaalam wa mambo ya uzazi ila nasikia kwamba mbegu za mwanaume ndiyo zinaamua mtoto anayezaliwa awe ni wa jinsia gani na mwanamke hana mchango katika hilo.
true

........ mke wa baba mkubwa alimkashfu sana alipokuwa akijifungua dada zangu (sorry) alikuwa anasema ameleta mambwa jike duniani ........
its sad maana kutokana na mtazamo wake, mtu anaweza kuimwambia kwamba hata yeye alikuwa "m--- jike" once upon a time. hii ni inferiority complex iliyopitiliza
 
Jinsia ya mtoto sio choice ya mzazi jamani kwa nini watu hadi leo hawaelewi? Mie uncle wangu alizaa watoto 6 na wote wanawake, akawa na hamu ya wakiume na kweli last born akawa kidume. Sasa hicho kidume ndo kimekuwa hasara ya familia na wakike ndo faida ya familia!....
 
Ingawa mimi siyo mtaalam wa mambo ya uzazi ila nasikia kwamba mbegu za mwanaume ndiyo zinaamua mtoto anayezaliwa awe ni wa jinsia gani na mwanamke hana mchango katika hilo.

naam, pamoja na kwamba fertilization inatokea wakati upi wa mzunguko wa hedhi wa mwanamke. katika ule mzunguko siku ya 13 na 14 yai ndio kwanza limetoka hivyo sperms zikiingia, mara nyingi the chances are zinazokuwa za kwanza ni Y sperms (hizi ni sperms zenye kasi kubwa, nguvu kubwa na life span fupi ya masaa takriban 36 tu) kwaiyo hapa atatengenezwa baby boy. kama mke na mume watashirikiana before siku hizo (kwamba sperms zikiingia humo alafu "zikachomeshwa mahindi", baada ya saa 36 za Y zitakufa), zitabaki za X ambazo kasi na nguvu yake sio kubwa na life span yake ni ndefu, takriban saa 72, yai likipatikana hapo, atapatikana baby girl


walio wataalam zaidi wanaweza kusaidia hapo, na kuedit pale nilipomisinform...just incase....
 
Hapa ni kweli kabisa kwamba mpangilio wa kupataikana mtoto wa jinsia gani, baba na mama lazima wawezeshwe aina fulani ya elimu. Kisayansi inakuwa na asilimia fulani kama mtu ataeleweshwa, anaweza kupanga mtoto anayetaka kumpata. Ila kumbukeni mtoto ni mtoto. Shukuru kwa huyo uliyejaaliwa. Wengine hawapati mpaka wanaenda kununua.
 
you are totally wrong mkuu! Rejea elimu ya uzazi na usome mambo ya "XY" NA "X" Halafu uje kujisahihisha mwenyewe hapa!

nimeamua na mimi niseme, Baba hotoa XY na Mama XX, ikiwa X ina nguvu kuliko y mtoto ni KE, ikiwa Y ina nguvu kuliko X, mtoto ni ME....Hii ni biology yangu 4m4 enzi zile.phenotype na genotype nimekuongezea na hili hapa
We all know as per science XX is female XY is male then where are the creature Single X,Y And YY stand for?
Crossing of xx and yy
genes
x
y
x
xx
xy
x
xx
xy

XX=normal female
XY= normal male

XXY= a male with female characteristics
XYY= a male with abnormal strength (cruel in nature), mythical Hercules has this one
XXX= super female

X= an undeveloped female body
Y and YY does not contribute to embrayo formation
 
Back
Top Bottom