Wanawake msikurupuke kutukana watu wakipiga simu

Wanawake msikurupuke kutukana watu wakipiga simu

Aise, ila una moyo mzuri tu,
Changu kingekuwa ni hela, simu ningeirudisha maeneo yale yale niliyoikuta.
 
Hahahah umenikumbusha zamani nilikuwa nina hasira mtu apokee simu sio yake.

Basi bwana mwenye simu na aliyepokea simu majina yanafanana halafu ni ndugu, sasa sauti ya muhusika naifahamu, namwambia namtaka fulani (nataja jina), ananiambia ndio mimi, kila nikisema sio wewe yeye anabisha, "nilishusha mafuriko ya maneno mabaya" hakutegemea nikamwambia kama kakutuma uchezee akili yangu siku nyingine hutarudia.

Duuuh huu ndio ulikuwa mwisho wa kuongea hovyo kwenye simu, maana nikaitwa kutambulishwa yule nilomtukana, nilitambulishwa vizuri utapenda,"kaka fulani huyu ndo fulani mke wangu mtarajiwa"(hapo nyumbani washapeleka posa washapangiwa mahari ndo wanajipanga wapeleke), nae akajibu, "anhaaa, nashukuru kukufahamu, lakini si ndio huyu ulozaa nae" akajibu ndio basi kaka yake akamalizia, "kama ndio huyu nafurahi sana maana nilishasikia sifa zake kabla, anafaa"

Mimi macho chini pale nikaanza tena kuomba samahani, nashukuru alikuwa muelewa akanisamehe na hakuna aliyejua zaidi ya sisi watatu, ila nilijifunza sana siku ile(huyu ndugu yake alikuwa anaishi mbali hivyo sikuwa namfahamu kabla na jina nilishatajiwa ila nilisahau). Sitarudia teeeeenaaaaaaaa
Huyu mwanamke kazidi yani anaongea kama cherahani yanayo khusu na na yasio khusu,kwanza huyo jamaa yako kama hujui anatumia dawa za kikongo usione anajua kusugua bure ni dawa hizo na mimi ndio nilompa leo anajitia ki***m yani gazeti.
 
Unajua huyu jamaa alipokuja kuchukua mfuko wake nilimwambia plz hesabu kahesabu nikamwambia ziko sawa
kasema ndio nikamwambia haya kwaheri,nimemuache hapo kaduwaa nimeondoka.
kama wasemavyo "tenda kheri ulipwe Shari" Pole kwa hayo madogo...ila naona hawakufanya shopping siku hiyo !!?!! Nimefurahi kwa kula halali yako, Wema wako utaukuta huko mbele....!!

Mamndenyi mali ya hivo haidumu hata siku moja!! Dunia bado ina watu wema jamanii... na baraka zipo nyingi..!!
 
Last edited by a moderator:
kama wasemavyo "tenda kheri ulipwe Shari" Pole kwa hayo madogo...ila naona hawakufanya shopping siku hiyo !!?!! Nimefurahi kwa kula halali yako, Wema wako utaukuta huko mbele....!!

Mamndenyi mali ya hivo haidumu hata siku moja!! Dunia bado ina watu wema jamanii... na baraka zipo nyingi..!!
yani hata sikuyauliza yani nimepokea simu kwa bashasha matokeo yake unaambulia matusi sema hakua na jipya hata moja yote ndio yale yale ya zamani anaya rejea rejea tuu...
 
yani hata sikuyauliza yani nimepokea simu kwa bashasha matokeo yake unaambulia matusi sema hakua na jipya hata moja yote ndio yale yale ya zamani anaya rejea rejea tuu...
" Makamu yako kwa Moula imepanda daraja " wewe kumkaaliya kimya ndo umemaliza !!
 
Mara zote sie wanawake tuna roho mbaya,
Unatukana mtu hata usiyemjua;

Lakini ulifanya tu kosa moja,
Ungefungulia kule kule ulikookota, uchukue chako vyake mwachie huko huko;

Dunia hakuna wema kabisa.

Unajua huyu jamaa alipokuja kuchukua mfuko wake nilimwambia plz hesabu kahesabu nikamwambia ziko sawa
kasema ndio nikamwambia haya kwaheri,nimemuache hapo kaduwaa nimeondoka.
 
Back
Top Bottom