Habari zenu jamani.
Naomba kuuliza, inawezekana mie nimesahau mafundisho ya shangazi, wanawake wenzangu mnawezaje kuishi na mwanaume anaye fokafoka? Maana mimi naona yamenifika hapa!
Huyu mwanaume amenizidi umri kwa miaka saba, sasa sijui ananichukulia mimi mdogo yake! Yaani nikikosea kitu kidogo atafoka huku ananikata jicho kali, haijalishi kuna dada wa kazi karibu, ni atafoka tu! Huyo dada wa kazi nae anafokewa hadi namuonea huruma mtoto wa watu.
Huwa nanyamaza kisha namtafutia pose zuri namwambia anavyonikwaza ila routine ni ile Ile, nahisi kukonda, kugombana nae siwezi atanibonda nife.
Naombeni mbinu jamani nifanyeje, yamenifika kwa koo mwenzenu?!
Naomba kuuliza, inawezekana mie nimesahau mafundisho ya shangazi, wanawake wenzangu mnawezaje kuishi na mwanaume anaye fokafoka? Maana mimi naona yamenifika hapa!
Huyu mwanaume amenizidi umri kwa miaka saba, sasa sijui ananichukulia mimi mdogo yake! Yaani nikikosea kitu kidogo atafoka huku ananikata jicho kali, haijalishi kuna dada wa kazi karibu, ni atafoka tu! Huyo dada wa kazi nae anafokewa hadi namuonea huruma mtoto wa watu.
Huwa nanyamaza kisha namtafutia pose zuri namwambia anavyonikwaza ila routine ni ile Ile, nahisi kukonda, kugombana nae siwezi atanibonda nife.
Naombeni mbinu jamani nifanyeje, yamenifika kwa koo mwenzenu?!