Wanawake kujisahau wanapokuwa kwenye ndoa

Wanawake kujisahau wanapokuwa kwenye ndoa

stephot

JF-Expert Member
Joined
Mar 1, 2012
Posts
17,746
Reaction score
27,217
Kumekuwa na matatizo makubwa sana ya mizozo ndani ya ndoa,kudharauliana,kujibishana,kutukanana na hata kukashifiana,hili jambo mnapoanza urafiki mpaka kufika mnaoana huwezi kulikuta au inaweza chukua hata miaka kadhaa 2-3 kukiwa shwari kabisa,katika udadisi nilioufanya nimegundua kuna kundi kubwa la wanaume walio kwenye ndoa wakilalamika kuwa wanawake ndio chanzo kikubwa cha mambo haya na hili linatokea immediately baada ya kuanza kuzaa,kwani wanawake huhamishia mapenzi kwa watoto na kuona wanaume ni kama mizigo tu kwenye familia na hawahitaji kuendelea kupata special treatment kama ilivyokuwa hapo awali,tufunguke kwenye hili wadau nani hasa anastahili lawama na nini kifanyike kuepukana na hii mifarakano kwenye ndoa inayosababishwa na wanawake?
 
Kumekuwa na matatizo makubwa sana ya mizozo ndani ya ndoa,kudharauliana,kujibishana,kutukanana na hata kukashifiana,hili jambo mnapoanza urafiki mpaka kufika mnaoana huwezi kulikuta au inaweza chukua hata miaka kadhaa 2-3 kukiwa shwari kabisa,katika udadisi nilioufanya nimegundua kuna kundi kubwa la wanaume walio kwenye ndoa wakilalamika kuwa wanawake ndio chanzo kikubwa cha mambo haya na hili linatokea immediately baada ya kuanza kuzaa,kwani wanawake huhamishia mapenzi kwa watoto na kuona wanaume ni kama mizigo tu kwenye familia na hawahitaji kuendelea kupata special treatment kama ilivyokuwa hapo awali,tufunguke kwenye hili wadau nani hasa anastahili lawama na nini kifanyike kuepukana na hii mifarakano kwenye ndoa inayosababishwa na wanawake?

Mfano: aache kunyonyesha am-brashie mme viatu au kumnyooshea?
kuna mambo mengine mtu unatakiwa uelewe tu kuwa kwa muda flani huwezi kutimiziwa!!!
japo ni kweli huwa kunakujisahau baadhi ya mambo kwa wanawake walio kwenye ndoa
 
Wanaume wawasaidie wanawake katika kulea watoto sio financially tu hata kusaidia kubembeleza mtoto anapolia na pia kumpumzisha mama kidogo kwa baba pia kucheza na mtoto hata usiku baba naye amke ampe mtoto maziwa ya chupa mama naye alale kidogo. Vile vile majukumu mengine yanayo muhusu mama anapopata mtoto baba ajaribu kuyafikia yale majukumu hasa domestic works.

Hii ndoa inadumje?
Ninamifano hai!
 
Kama kweli unampenda huyo mtoto ambaye wewe ndiye uliyesababisha kupatikana kwakwe, basi nawe utaelewa kuwa sasa kuna aliyeongezeka na atachukua nafasi yako kwa muda tu, halafu wewe unarudia pale pale.
Pia wanaume hamna jema Ukiolewa ukazaa shida, usipozaa keroooooooooooooo! keroooooooooooo! mpk moyo unaweza ukatoka ukaacha mwili kwa maneno ya mume na nduguze, sasa nyinyi mnataka tufanyeje? maana tunawalea nyiyi na watoto tuaowazalia lakini bado mnalalamika, kwa nn na nyinyi msitusaidie kufanya vitu ambavyo unaona nilikuwa nafanya wakati sina mtoto kwako na kwa sasa sifanyi na mnajua sababu ni nn, inatakiwa mtusaidie.
Na mkumbuke sisi ni wanadamu kama nyinyi na tunatumia akili, busara, uvumilivu na upendo kukaa na nyinyi mpk ukitoka nje unajidai kuwa mm nina familia. mnapaswa mtupende na mtuelewe.
 
Siyo kwamba wanawake ndio wanaharibu ndoa, bali kwa muda huo inawawia vigumu kuyatimiza yote kama awali.

Hebu fikiria mwanamke anakaa na mtoto toka asubuhi mpaka jioni halafu ukizingatia watoto wanavyosumbua unadhani atakuwa anastahili lawama yoyote katika hilo, ukizingatia alikuwa anafanya kazi muda wote? Mtoto akilia tu, mama huyo.

Ikifikia hapo inatakiwa mwanaume na yeye amuelewe mkewe, aangalie kazi ambazo mkewe anazifanya toka kulipo kucha mpaka kunapokuchwa.

Kwahiyo hata akipata mara moja moja haina shida.
 
Evelyn Salt na Lisa labda muweke wazi huo muda ambao mnataka mwanamke aachiwe kuhudumia mtoto ni mpaka atakapotimiza miaka mingapi ndio mrudishe hayo mapenzi back to Mwanaume,kwa maana unakuta matatizo wakati mwingine yanaendelea mtoto au watoto wako above 10yrs of age!
 
Last edited by a moderator:
Mfano: aache kunyonyesha am-brashie mme viatu au kumnyooshea?
kuna mambo mengine mtu unatakiwa uelewe tu kuwa kwa muda flani huwezi kutimiziwa!!!
japo ni kweli huwa kunakujisahau baadhi ya mambo kwa wanawake walio kwenye ndoa

Wanaume tujifunze kuvaa viatu vya wenzetu....!!!The problem of men ni selfishness bhaaaasi!!!Unataka mwanamke asibadilike limekua jiwe hilo!!
 
Jambo la msingi ni kila mtu kutimiza wajibu wake ndani ya nyumba ingawa wanawake hasa hawa wakiswahili kabla ya ndoa atafanya kila k2 vilivyopo na vya ziada, muoe sasa uone mbilinge zake! Tena usirogwe ukajidai unamsaidia kazi kwa mapenzi tu pale mwanzo kama kufua, kupiga pasi, kujipelekea maji bafuni km hamna maji, kupika hata kuandaa chakula! Utajuta na roho yako. Mwenzio ataona huo ni wajibu wk na ukimchenjia tu kosa. Ooh umebadilika, unawanawake na maneno kibao kumbe ye ndo ameshindwa kukuenzi.
 
Wanaume wawasaidie wanawake katika kulea watoto sio financially tu hata kusaidia kubembeleza mtoto anapolia na pia kumpumzisha mama kidogo kwa baba pia kucheza na mtoto hata usiku baba naye amke ampe mtoto maziwa ya chupa mama naye alale kidogo. Vile vile majukumu mengine yanayo muhusu mama anapopata mtoto baba ajaribu kuyafikia yale majukumu hasa domestic works.

Hii ndoa inadumje?
Ninamifano hai!

Tena baadhi hawana hata huruma akisikia mtoto analia utaona kakunja sura kama ya mbuzi anageuka na pembeni utamsikia "arooo bembeleza mtoto wako" hapo ni usiku wa manane mama yupo bize na mtoto yeye anakoroma...tu !!!

Afu asubuhi anakuja na maneno mbofu mbofu eti wanahitaji spesho treatment, uamke unyooshe, ubrash usiku hata hujalala....kueni na huruma kwa wake zenu sio marobot hao!!!!!!
 
Evelyn Salt na Lisa labda muweke wazi huo muda ambao mnataka mwanamke aachiwe kuhudumia mtoto ni mpaka atakapotimiza miaka mingapi ndio mrudishe hayo mapenzi back to Mwanaume,kwa maana unakuta matatizo wakati mwingine yanaendelea mtoto au watoto wako above 10yrs of age!

Nimetoa mfano na pia nikasema "japo ni kweli kuna baadhi ya wanawake wanajisahau kwenye ndoa zao"
 
ukipanga ratiba zako vizuri utamuhudumia mumeo ipasavyo na mtoto au watoto wako ipasavyo bila ya malumbano tatizo letu ni kuiga hata visivyoigilizika.
 
Wanaume tujifunze kuvaa viatu vya wenzetu....!!!The problem of men ni selfishness bhaaaasi!!!Unataka mwanamke asibadilike limekua jiwe hilo!!

Halafu ishu hata sio kubadilika, ishu ni muda gani kabadilika.... kama mwanamke yupo tu home akitoka job ni kukwangua kucha na kushika remote hata mi namuona zuzu!!! lakini unaona kabisa mwanamke anamajukumu ambayo ni kweli yanamfanya ashindwe kumhudumia mme wake afu unalaumu daah hata huyu mwanaume nae atakuwa zuzu tu mtu gani asie na huruma!!!!!!!!!!!!!!
 
Sidhani kama mwanamke akipanga ratiba vizuri anaweza shindwa kutimiza wajibu wake kwa mume na motto tatizo lao ni kwamba wanawatumia watoto kusingizia. Kila siku ukitoka kazini unamkuta kwa majirani kupiga soga unapofika wewe ndo anaanza kuhangaika mara maji yameisha mkaa hamna nepi sijafua
 
Wanaume wanapenda kubembelezwa sana, emagine una mtoto wa miezi mi4, unaishi madale, unafanyakazi mjini, unatoka kazini saa kumi na moja mpaka ufike home saa mbili , umechoka mtoto anakuhitaji na mwanaume anasema unaounguza mapenzi kwake how? mtoto na baba nani bora? na wengine mtoto akilia hatakama ndo unampahayo malavidavi atakutoa mbio 'wewe mtoto humskii' now mtu ufanye nini? bado unaamka saa 10usiku kilasiku, familia inakutazama wewe(mama, wifi shemeji)nahao wanataka uwaridhishe.

KUMBUKA, Kabla hujanioa nilikuwa nakaa kwetu, kula kulala bure, sina mtegemezi yeyote, sina stress zozote za maisha kama rent, umeme, school fees, maji etc, no mama wakwe, wifi, shemeji or any sibling kunisumbua, i was just single lady. now my head full of staff and some of the staff wewe ndo unasababisha.

Wanaume achane kuwa selfish, kumbukeni maisha yanabadilika na mawazo ya maisha ya kitamthilia ondoeni vichwani mwenu kuweni na maisha halisia.
 
Evelyn Salt na Lisa labda muweke wazi huo muda ambao mnataka mwanamke aachiwe kuhudumia mtoto ni mpaka atakapotimiza miaka mingapi ndio mrudishe hayo mapenzi back to Mwanaume,kwa maana unakuta matatizo wakati mwingine yanaendelea mtoto au watoto wako above 10yrs of age![/QUOT
mimi nilikuwa namaanisha mtoto akizaliwa mpk akifika 2yrs basi mama na baba wanatakiwa waendelee kumlea mtoto wao na mapenzi yao kama kawaida. na hata wakati mtoto kazaliwa baba ukiona mkeo anampenda sana mtoto uwe unamkumbusha kuwa mbona wanisahau? Au na wewe mpende mtoto.
Pia hapo kwenye red , Mh! Patakuwa na mashaka, kama mtoto ameshatimiza miaka hiyo lakini baba hapati haki yake sawa sawa. Mh! sijui na sina Comment hapo
 
Dr, mbona huwa tunakubali ushauri jamani?
Mi nataka tuongelee na kwa wanaume kujisahau. Kama unakuta wife kazibyake.kila akiona mashati, vest, pants na socks anakununulia. Kuna saa mwanamke anakaa anawaza mara ya mwisho mr kuninunulia hata tuhereni twa kichina lini, haoni kabisaa!
Staki kuongelea uhanga wa chakula cha usiku! Unajua wanawake ndo wahanga wakubwa? Tukipoteza appetite tunalaumiwa tujiongeze, ooh weight sijui nini. Akipoteza baba appetite still lawama kwetu, ooh boresha mazingara sijui pungua! Yeye na kitambi chake haulizwi.

Muhimu wanandoa wote kwa pamoja wasijisahau. Na mwenzio akikukumbusha usiwe mkali, jiongeze!
Stephot utakoma leo....bado 'makungwi' hawajaja, utatafuta pa kutokea leo!
 
Hakuna ilipoandikwa kuwa mwanamke afue nguo, anyooshe wala ampelekee maji mme bafuni yote ni kwa ajili ya mapenzi. Tatizo kubwa wanaume wanapooa wanadhani kuwa sasa wamepata watumwa wa kuwafanyia kila kitu ndani ya nyumba zao.


Wanawake nao ni binadamu wanachoka na shughuli za nyumbani hata kama siyo wafanyakazi maofisini. Kweli kama una mapenzi na mwenzio unaona ana angaika kumuhudumia mtoto nawe unalalamikak uwa hatimizi majukumu yake kwani huyo mtoto wewe hakuhusu? Jirekebisheni na muache kulalamika kusiko na sababu!
 
Dr, mbona huwa tunakubali ushauri jamani?
Mi nataka tuongelee na kwa wanaume kujisahau. Kama unakuta wife kazibyake.kila akiona mashati, vest, pants na socks anakununulia. Kuna saa mwanamke anakaa anawaza mara ya mwisho mr kuninunulia hata tuhereni twa kichina lini, haoni kabisaa!
Staki kuongelea uhanga wa chakula cha usiku! Unajua wanawake ndo wahanga wakubwa? Tukipoteza appetite tunalaumiwa tujiongeze, ooh weight sijui nini. Akipoteza baba appetite still lawama kwetu, ooh boresha mazingara sijui pungua! Yeye na kitambi chake haulizwi.
Muhimu wanandoa wote kwa pamoja wasijisahau. Na mwenzio akikukumbusha usiwe mkali, jiongeze!

Da King'asti..ndio maana mimi nina filosofia ya 'mapenzi huisha', kwa sababu mbali mbali. Haijalishi ni sababu gani, iwe ya mume au mke au both...but it is a reason enough kumaliza mapenzi, na mapenzi yanapoisha ndio kunabaki kuvumilia na mazoea. Sasa hapo ndio tunapotofautiana...wengine wanaweza vumilia longer, wengine mazoea tu maisha yanaendelea..na wengine ndio hawawezi hiyo 'biashara'. Na kwa wasioweza hapo ndio inafuata kuflirt, kucheat, na kwa wasio wastaarabu even masengenyo, magomvi, na pengine mpaka kudhuriana mwili!

Sa kisa nini husubiri mpaka mfikie 'extreme'!? Ukiona mapenzi yameisha....chapa lapa! Kwani umezaliwa naye huyo!?
 
Back
Top Bottom