Wanawake hii tabia mbaya inawasaidia nini?

Wanawake hii tabia mbaya inawasaidia nini?

Kila wakati uko kwenye Whatsapp inbox yangu, unaangalia nachat nini na mama yangu na dada yangu?
Huu ni upumbavu wa hali ya juu sana.
Nina haki ya faragha. Unaiingilia ili iweje?
Mbona mimi sichunguzi mawasiliano yako na ndugu zako?
Mianamke ya kiswahili haina adabu wala haina akili.
Muda unaotumia kupekua simu yangu si bora ukaongeze elimu na ujuzi wako?
Pumbavu
[emoji38] [emoji38] [emoji38] mweee hasira hizi asa si umwambie mwanamke wako kuwa hupendi io tabia unadhani uku amekusikia sasa!?!
 
Mbaya ni kuona na kuongea ila kama anaona halafu anajinyamazia muache achangamshe macho.

Pia sio ukosefu wa akili kama usemavyo nadhani ni mapenzi juu yako.
 
Kuna watu ugonjwa wao ni kusoma inbox za watu hata kama haziwasaidii kitu, tena ukiona mtu anasoma mpaka chat zako na mama ako ujue hajiamini na huwa anakuongelea vibaya kwa watu wake wa karibu sasa anahisi na wew unafanya hivyo ndo maana anajihami kwa kutaka kuona mnachozungumza. Hii tabia ipo sana kwetu wanawake, halafu sio waswahili tu hata wanaojikuta wa kishua kuna wenye tabia hizo.
 
Kila wakati uko kwenye Whatsapp inbox yangu, unaangalia nachat nini na mama yangu na dada yangu?
Huu ni upumbavu wa hali ya juu sana.
Nina haki ya faragha. Unaiingilia ili iweje?
Mbona mimi sichunguzi mawasiliano yako na ndugu zako?
Mianamke ya kiswahili haina adabu wala haina akili.
Muda unaotumia kupekua simu yangu si bora ukaongeze elimu na ujuzi wako?
Pumbavu
Makubwa sasa!Kama huna wasiwasi na unachochat unamficha nini? Af watu kama wewe ndo number moja akipokea simu unasogea karibu usikilizie anaongelea nini! Akitabasamu tu kidogo atachezea kichapo. Bora yeye huchunguza mukiwa wote. Wewe unasibiri aingie bafuni ndo umkague hasa
 
Ngoja nitoe na yangu, Mimi nimepewa masharti kuwa profile picture ya whatsap yangu niweke picha yake, akanitumia picha ya kuweka. Alafu akasisitiza tafadhali weka sasahivi....basi nikatoa yangu nikaweka yake. Baadae akaanza kuwapigia watu wake akawajuza kuwa namba ile (yaani yakwangu) kuwa ni yake......pia akaanza kusema unajua mume wangu kuna watu wengi sana wananipenda alafu wananisumbua ila mm sina mpango nao. Upande wangu rafiki wananihoji kuwa imekuaje mbona umeweka picha ya mwanamke wakati hujaoa? Sasa nimesafiri kila nikiweka picha yangu pale anapiga simu anagomba, mda huu nimeweka kipicha cha vikatuni ndio naona katulia. Cha ajabu kwake yeye kaweka picha yake, wanawake wanashida sana aisee!
 
Back
Top Bottom