Wanawake acheni hii tabia

Wanawake acheni hii tabia

lazima ukae

JF-Expert Member
Joined
May 15, 2013
Posts
791
Reaction score
417
Kuna hii tabia unakuta mwanaume umepata pesa lakini mara tu baada ya kupata pesa unampigia mpenzi wako ili muonane uweze kumpatia na yeye pesa ya matumizi lakini shida inakuja pale anapogundua tu umepata pesa atakuambia mkutane sehemu fulani mfano Mlimani City au sehemu yoyote nyingine ambayo watu wanafanya manunuzi ya vitu mbalimbali.

Mkishakutana tu kabla hata hujamkabidhi pesa ataanza mara oooh baby ninunulie hiki mara ninunulie kile kiasi kwamba kama ulipanga kumpa laki tatu karibu laki mbili yote itaishia kwenye kulipia manunuzi ya vitu alivyochukua huku akiwa na matarajio kwamba bado kuna fungu ambalo unataka umpatie.

Binafsi ninachofanyaga nikikutana na tukio kama hili huwa nafanya hivi, kama nilipanga kukupa laki tatu na umeshatumia laki mbili nakumalizia tu laki moja iliyobaki ili usiniharibie bajeti zangu.Haiwezekani kabla hatujakutana uanze kuniongezea bajeti zingine zisizo na kichwa wala miguu.

Wanawake jitahidini kubadilika otherwise mtabadili mabwana kila uchao.Sisi wanaume thamani yenu huwaga tunaiona pale ambapo bado tunakua hatujafanikiwa kuwavua nguo zenu za ndani ila tukishawavua tu mnakua wakawaida sana na tunakua hatuna tena chakupoteza hivyo ni jukumu lenu kuwa waangarifu na tabia zenu.

Povu ruksa
 
Yani unapata pesa unawazia kukutana na mwanamke??



Badala ya kufikiria kusave au kuwekeza!

Nataka nikwambie jambo moja litakusaidia, the best time for appointment is when you're broke
 
Ukishamjua hulka yake, unapopata pesa usimwambie.
Fanya mambo ya maendeleo tu.

Kama unamwita mwitie nyumbani kwako.

Sasa wewe unapata pesa unatangaza. Usipende kujionesha unapopata pesa.
 
Haahahhahaaha eti laki3 uzi wako haufanani na kiasi unachohonga mkuu
 
Yani unapata pesa unawazia kukutana na mwanamke??



Badala ya kufikiria kusave au kuwekeza!

Nataka nikwambie jambo moja litakusaidia, the best time for appointment is when you're broke
Thubutuuuuu!! Ukiwa broke kumbatia mito ulale.
 
Pole sana mkuu..mpenz unampa laki tatu?atajua unazo then ukija kumuoa ukaanza kumpa elfu kumi au ishirin lazima akukimbie..tafuta mpenzi wa kumpa elfu ishirin au thelathin then ukimuoa umpe laki tatu atakaa milele..you choose wrong corse
 
Sasa kama pesa yako kwa nini upangiwe pa kukutana?

Hapo hata hupaswi kulalamika aisee sababu wewe ndio ulipaswa kusema njoo sehemu fulani nikupatie pesa. Bhaas.
Hoja mubashara kabisa hii. Mgonjwa hufuata mganga na si vinginevyo.
 
Wanawapangia sehemu salama ambayo hela yenu haitapotea kwa kuporwa😀😀

Kingine, inakuwa ni invitation ya kushuhudia inflation rate... uone jinsi gani hela yako inavyotumika kihalali kulingana na bei ya bidhaa.

😉😉
 
Hiyo hela kafanye training ya forex anza kupiga pesa
 
Sasa kama pesa yako kwa nini upangiwe pa kukutana?

Hapo hata hupaswi kulalamika aisee sababu wewe ndio ulipaswa kusema njoo sehemu fulani nikupatie pesa. Bhaas.
Huyu atakuwa mwanaume toleo la pili sio bure!
 
Back
Top Bottom