Wanaumeee. ..... Itikeni Naam......

Wanaumeee. ..... Itikeni Naam......

huyu kamiss kufuliwa,kudekiwa nyuma na kupikiwa vzr zaidi ya hapo hamna shida. tena kama una hela ndo hamna shida kbs...mi nilijua maskini
 
hhehehehe mie sipo kwangu toka alhamis !bas hayo maswali ya"UNATEGEMEA KURUDI LINI' meeeeeengi!pyeee !

apambane na hali yake! au la akafie hukooo!(BInamu yako)
umempata gudume wa Jf huna habari na mumewe
 
Binamu yako ana roho ya chips, wengine tuna roho za mihogo waifu akisepa na watoto nampa mwezi tu asiporudi atakuta nimemwoa mama sangelima wa mtaa wa pili
 
Huyo Ana mapungufu makubwa sana
Mwanamke mmeanza nae maisha mme hustle pamoja amekuvumilia,umemvumilia kuna siku hata mkalala njaa mkila mnashea sahani moja hadi hapo mlipo leo umepata vijisenti unamuona mwanamke wako shithole unaenda kwa vidosho ...mwanamke anaondoka then roho ya majuto inakuja kwa kasi kubwa mwisho wa siku unaishi maisha ya guilty life vidosho wanakukimbia pengine umeanza kuishiwa mana si ulikua unawahonga, downfall inakuja kwa kasi maana machozi ya mwanamke yanajibiwa kwa kasi kubwa kama ya 4G na Mungu, pengine tena hapo uombe tu katika downfall yako hujanyaka magonjwa ya gono ...ndivyo ilivyo what goes around.......
 
Nyumba ni mwanamke,na mara nyingi wanaume huwa tunajutia kuondoka kwa mwanamke ikiwa sisi ndiyo chanzo cha migogoro.Yapata mwezi sasa mama watoto wangu kaondoka kwa matatzo yake mwenyewe niliyoshindwa kuyavumilia na kuamua kumpa likizo ndefu kbs.Moyo wangu una amani kabisa na ninafanya kazi zangu nikiwa very comfortable.Awali niliwaza akiondoka nitatafuta kipozeo lkn hari imekuwa tofauti kidogo maana nmejikita kwenye kazi zangu,tena bidii imeongezeka,huyo binamu yako ndy chanzo cha migogoro ndiyo maana yupo na hari hiyo(anajutia)
 
Halafu mkishaitika nisaidieni haya maswali yanayonizonga kichwani maana sielewi atii....

Hivi mwanaume ulishakuwa na familia maana ya mke na watoto kadhaa, kwa namna yeyote ile yule mwanamke akiondoka kwenye nyumba na watoto akakuacha uendelee na maisha mwenyewe huwa inawauma sana? Hata kama kuna magomvi yaani mwanaume anaweza hata kukonda na au kuwa mlevi na hajijali tena? Unakuta huyu mwanaume ana hela zake ila kuachwa na mke na watoto anakuwa anashindwa kabisa kuendelea kuishi.... bila kujali yeye mwanaume kila siku ndo alikuwa anamtamkia mkewe kuwa ntakufukuza na vifaranga vyako, hata ukiondoka hata sijali tena ntaoa mwanamke mwingine. Shangaa sasa mke akiondoka..... haoi hanunui milupo badala yake kila siku anadhoofika..... sielewi nini huwa kinatokea.

Hiki nilichoona hapo juu nina ushahidi nacho, binamu yangu mmoja yuko hooii amebaki kwenda kazini tuu ndo nguvu aliyonayo. Ana pesa nzuri na anakaa kwenye nyumba yake Tegeta ila alimkorofisha sana mkewe kumnyanyasa sana kumfuja hatimaye mke akaondoka na watoto weeh yaani hivi niandikavyo binamu anatia huruma. Naomba ni wanaume mnieleweshe.... kwanini huwa mnakata tamaa sana, mkizoea kuishi na mwanamke akiwa mbali nanyi huwa hamuwezi kuendelea mbele?

Sijui mnaenielwa....!!!?

Kasie Kasiba.
Mi naonaga hawajitambui tu tuwasamehe tu bure tuwaache hivyo walivyo
 
Naam Kasie,
Inawezekana sana mwanaume akashindwa kujiongoza pindi mke akiondoka. Humu mitandaoni huwa watu watabisha na kusema "huyo ni mvulana", "mwanaume suruali", lakini mara nyingi divorces zinaleta matatizo na kuyumba kwa watalaka na hatimaye wengine huishia kutumia mihadarati na pombe.

Vijana hawawezi kuelewa coz bado hawajui maana ya mke ndani ya nyumba.
very well stated, wasiojua thaman ya ndoa or ya mwanamke. either husemaga kama mtu alikua`bondwd so much na mwenzie they cant handle it na si ujinga they are strong to go thru that stage and eventually they will get over it or get back to their wivws.
 
Nyumba ni mwanamke,na mara nyingi wanaume huwa tunajutia kuondoka kwa mwanamke ikiwa sisi ndiyo chanzo cha migogoro.Yapata mwezi sasa mama watoto wangu kaondoka kwa matatzo yake mwenyewe niliyoshindwa kuyavumilia na kuamua kumpa likizo ndefu kbs.Moyo wangu una amani kabisa na ninafanya kazi zangu nikiwa very comfortable.Awali niliwaza akiondoka nitatafuta kipozeo lkn hari imekuwa tofauti kidogo maana nmejikita kwenye kazi zangu,tena bidii imeongezeka,huyo binamu yako ndy chanzo cha migogoro ndiyo maana yupo na hari hiyo(anajutia)
true fact, anajutia coz yeye ndiyo kasababisha na hakutegemea siku moja mke angesepa coz alishazoea m`take for granted..sasa analia na wakwao tuu..
 
Back
Top Bottom