Wanaume wengine ni hasara tu

Wanaume wengine ni hasara tu

Huo ni zaid ya mfumo dume tena wakishamba.kunajiran yangu naskia nae anambana mkewe mpaka bas.Mke anafanya kazi nzuri sana Serikalin but ukimuona unaweza sema ni house girl kwa jins alivyochakaa.Mumewe anakausafiri kake ila huwa hampi hata lifti yakwenda kazin
 
Wapare najua mtanishambulia lakini badilikeni jamani. Ubahili too much mpaka mnakera
 
Dada yetu tulimsomesha wenyewe ajabu baada tu ya kupata ajira akaleta mpare mmoja nyumbani eti anataka kuolewa, sasa tangu aolewe hajui ATM inafananaje wala ina rangi gani jamaa kateka kadi ya Benk.

Na hata akishachukua hiyo salary yake hampi ata mia hadi sister anatupigia simu kutuomba tumpige tafu, jamani kweli huu ni ungwana?

Umeshindwa kutumia akili kidogo tu, hicho mlichoshindwa kumpa, huyo mpare ndio anamtitmizia na inaonyehsa anammudu vyema. Unakereka wew wakati ATM katoa mwenyewe???!!!! Mbaya zaidi na hizo mnazojifanya kumtumia nazo anampelekea.........
 
He he he!
Mkuu kumsaidia ni wajibu wako kama ndugu kwa kile kiasi Mola alichokujalia ila nakushauri swala la kuingilia mapenzi yao wacha kabisa,,,

kumsomesha mumsomeshe wenyewe hela ale mwingine bado muongezewe mzigo wa kumpiga kick sista

ukitoa ushauri kwa dadako juu ya uhuru na mali zake hujaingilia mapenzi ya mtu coz unajaribu kupunguza un necessary disturbances.

Dah jamaa nae amekua kupe aisee,mi ningemchana kama ni mbwai ni mbwai tu lah!!
 
Hasara ni huyo dada yenu..

ahaa kaka si unajua hawa dada zetu wakisha kuwa under someone hawawezi kuwa na maamuzi mpaka wame zao waseme
na yule jamaa ni cha pombe sana kwa hiyo nafikili pesa yote analipa madeni ya pombe
 
Huyo dada yenu mpole sana

ndiyo bwana dada yangu anaga makuu, kwanza ata ninaumia sana nikifikilia upole wake na anavyofanyiwa, na uwa hapendi kuomba omba vijicent vya mtu ukiona kakuomba basi ujue kweli kaishiwa.
 
Ndo maana enzi hizo akina babu hawakuthubutu kumpeleka mtoto wa kike shule! Usipate shida ndo maisha na mume aliyemchagua!
 
Yaani MankaM siku ukimpata mmoja hutaamini ulichokuwa unakosa. Nakuhakikishia wala hatakuomba hiyo ATM, utamuomba mwenyewe aichukue.

huhuhuuu bila shaka wew ni mpare naona unajisafisha hii ya kupewa ATM ni mtu tu aamue loo umenikumbusha mndamba mmoja enzi hizoo sio gud tym ile huhuhuuuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom