Wanaume wanaokataa ndoa sijawahi kuona sababu yao ya kimantiki, na wanaume sisi ndio waharibifu

Bandiko Lako ni refu, lakini halijazingatia hoja wanazoongelea timu kataa ndoa. Wewe unazungumzia sogea tuishi kama ndio Moja ya ajenda yao, wakati wao hata hiyo sogea tuishi hawaitaki.

Alaf kingine ambacho hujakigusia au pengine hukijui, ni kwamba, kwenye timu kataa ndoa kuna makundi ya aina mbili. Kundi la kwanza ni wale wanaokataa ndoa kwa kutamka (hawa ni wanaume), lakini pia kuna kundi jingine ambalo linakataa ndoa kwa vitendo (hapa wengi ni wanawake). Ili kundi la pili, ndio limeibua kundi la kwanza.
Mkuu chek vzur kaandika kama kukataa ndoa ni kila mtu akae kivyake
 
Juzi jirani yangu mmoja ni mwanamama anakaa mwenyewe mme wake yuko mkoani. Jamaa kaja kabeba vizawadi ame drive km zaidi ya 300 kum surprise mke wake.

La haula. Kufika anagonga anayekuja kufungua ni kijeba ya mbaba yuko kavaa kaptula sebleni wako na mke wake. Jamaa kupigana hawezi maana jamaa mchepuko ni kipande cha mtu, ikabidi aanze kuita watu na kelele huku ana record. Ugomvi, kupigana na kurishiana silaha vikaanza.

Nikaona huu ujinga, nikafunga mlango nikamwambia wife hakuna kutoa pua nje sijui kusikiliza ujinga wao. Nikaendelea kucheki game ya Newacastle na Man City.

Kibaya zaidi watu walijaa na mwanamke alivyo mpumbavu akamkana mme wake, mme akaondoka na zawadi zake mwanamke anabaki na njemba. Nikasema dah

Nikawakumbuka jamaa zangu wa Kataa Ndoa, chini ya Mwenyekiti dronedrake
 
Juzi jirani yangu mmoja ni mwanamama anakaa mwenyewe mme wake yuko mkoani. Jamaa kaja kabeba vizawadi ame drive km zaidi ya 300 kum surprise mke wake.

La haula. Kufika anagonga anayekuja kufungua ni kijeba ya mbaba yuko kavaa kaptula sebleni wako na mke wake. Jamaa kupigana hawezi maana jamaa mchepuko ni kipande cha mtu, ikabidi aanze kuita watu na kelele huku ana record. Ugomvi, kupigana na kurishiana silaha vikaanza.

Nikaona huu ujinga, nikafunga mlango nikamwambia wife hakuna kutoa pua nje sijui kusikiliza ujinga wao. Nikaendelea kucheki game ya Newacastle na Man City.

Nikawakumbuka jamaa zangu wa Kataa Ndoa, chini ya Mwenyekiti dronedrake
Yaan ujinga tupu jamn,
 
Juzi jirani yangu mmoja ni mwanamama anakaa mwenyewe mme wake yuko mkoani. Jamaa kaja kabeba vizawadi ame drive km zaidi ya 300 kum surprise mke wake.

La haula. Kufika anagonga anayekuja kufungua ni kijeba ya mbaba yuko kavaa kaptula sebleni wako na mke wake. Jamaa kupigana hawezi maana jamaa mchepuko ni kipande cha mtu, ikabidi aanze kuita watu na kelele huku ana record. Ugomvi, kupigana na kurishiana silaha vikaanza.

Nikaona huu ujinga, nikafunga mlango nikamwambia wife hakuna kutoa pua nje sijui kusikiliza ujinga wao. Nikaendelea kucheki game ya Newacastle na Man City.

Nikawakumbuka jamaa zangu wa Kataa Ndoa, chini ya Mwenyekiti dronedrake
Ss Mm najuulza hapo huyo mke aliyeingizA mchepkko hapo ni kwa Mme wake? 🤣🤣
 
Hapana, ni kama mke na mume wako kikazi mkoa tofauti. So hua ni kama mme hua anakuja one time na kuondoka. Mwanamke kwa jinsi nlivyomuona sio mwaminifu, maana hua naona vijamaa vinaingia na kutoka. Ndoa hizi kazi sana. Ndo maana wanaume tunaishi maisha mafupi
duh sema kwwl ila hawa wanaosafr wanawake wanachepuka sana mm nilona jamaa anasafri kwnda Congo mpaka Miez 3 ajarud.
 
Mkuu Analyse,

Labda bado hujanipata, sogea tuishi hawaitaki. sawa kama hiyo sogea tuishi hawaitaki kwahyo wanaume hawa hawana mamlaka na wanawake hao?
Kama ni kila mtu aishi kivyake, je matokeo ya ngono ni nini? Kupata watoto. Halafu je hao watoto wanalelewa kila mtu akiwa kivyake?

Kama sogea tuishi hawataki huoni kwamba wanaendeleza ongezeko la singo mama mitaani?
Embu wewe watetee mantiki yao ni ipi?
Ukitaka kuwaelewa wanaokataa ndoa, kwanza wasikilize sababu zao.

Unajua karibia wote waliopo kwenye hiyo timu, ni kwamba mapenzi yaliwababua sana, kiasi wakapoteza uvumulivu. Na hapo ndio inapokuja mantiki yangu kwamba, hata hiyo sogea tuishi hawaitaki Tena. Kataa ndoa ni matokeo ya kumbukumbu mbaya za mahusiano.

Alafu ukisema kuhusu kuhalalisha ngono, walio kwenye ndoa ndio wanacheza rafu kuliko kawaida.
 
Ukitaka kuwaelewa wanaokataa ndoa, kwanza wasikilize sababu zao.

Unajua karibia wote waliopo kwenye hiyo timu, ni kwamba mapenzi yaliwababua sana, kiasi wakapoteza uvumulivu. Na hapo ndio inapokuja mantiki yangu kwamba, hata hiyo sogea tuishi hawaitaki Tena. Kataa ndoa ni matokeo ya kumbukumbu mbaya za mahusiano.

Alafu ukisema kuhusu kuhalalisha ngono, walio kwenye ndoa ndio wanacheza rafu kuliko kawaida.
Na walio kwenye ndoa ndio watamu jmn maana kuna vitu wanavikosa, kule hawapewi miuono feni, style ni mojaa tuu, hakuna vionjo ila nje jamani kuna kuna kila aina ya utamu kwenye ndoa ni kuzaa tuu nje ni starehe. Kataa ndoa nawasalimia, hv mabaharia mpo kweli maana siwasikii kabisa
 
Wakuu habari za uzima?

Nikiwa zangu hapa sandaland na bro joh napitia stori za wana JF. Nikaona wimbi kubwa la wanawake wakilalamikiwa ni matapeli, kausha damu na maneno mengine mabaya

Leo nitaongea na KATAA NDOA mimi hawa sijawahi kuona sababu yao kimantiki na wengi ni fata mkumbo tu wasijue nini wanachoongelea.

Mosi, kukataa ndoa ni kuhalalisha uasherati na uzinzi. Mwanaume rijali lazima awe na mke ndani.
Wengi wanakataa ndoa kwa madai ya kwamba Ati mkiachana lazima mgawane pasu kwa pasu! Hilo linaweza kuwa kweli na lisiwe kweli vilevile. Kama ulichukua mtoto wa watu mkaanza kulala kwenye maboksi bila neti, godoro, kitanda na samani zingine na kakuvumilia. Iweje tayari umeshajipata Ati useme wewe nenda na hapa huna chako?

Kipindi unaondoka kazini anamuangalia mtoto kuanzia akiwa mdogo mpaka anaenda shule anafatilia maendeleo yake, na suala la kufatilia maendeleo ya watoto wanaume tupo nyuma sana na huo muda hatuna. Amekupikia, alikuwa anakufulia nguo na unaonekana mtanashati huko unapokwenda kwanini ukimuacha unataka aondoke bila kitu? Huo ni ukatili mkubwa sana.

Kama mwanaume anapaswa kukataa ndoa, let’s say sawa tukatae ndoa for the sake of argument. Ni mwanaume gani yupo radhi mtoto wake wakike achukuliwe bila utaratibu na aende kuishi na mwanaume mwingine? Kama huyo baba yupo hapa aseme?

Ndoa si lazima uende kanisani gharama za suti, shera, ukumbi na mengineyo. Hata kwenda kwa wazazi wa binti wakakupa baraka za kuishi na mtoto wao hiyo ni ndoa.

Kama hutaki kugawana mali na mwanamke ipo sheria ya kuandikisha mali zako ambazo tayari unazo wanasheria watanikumbusha sheria hiyo. Kwa maana hiyo Mke wako atajua kabisa kwamba mali fulani ni za kwangu. Na katika mgawanyo ataangaliwa mchango wake katika ndoa hiyo.

kuishi na mwanamke kwa kipindi cha miaka miwili hiyo ni ndoa (rebuttable presumption). Kwa maana kuwa kama umekuwa na mwanamke kwa kipindi hicho hio inatambulika ni ndoa kisheria.

Kama wanaopinga ndoa ni ile kwamba kila mtu akae kivyake je watoto mtakaowapata watapata wapi malezi ya baba na mama? Mtoto anahitaji malezi ya pande zote hivyo lazima muwepo pamoja na kukaa pamoja kwa miaka miwili na zaidi na ikathibitika hivyo hio ni ndoa.
Nataka niwaulize hao wanaopinga ndoa wanaelewa hata wanachoongelea?

Ndoa za kimila zinaweza kuwa hazina gharama kubwa, katibu tarafa lazima awepo katika ndoa hizi sababu yeye ndio anahusika kufatilia vyeti vya usajili.

Kukataa ndoa ni kuhalalisha uasherati na uzinzi.
Matatizo ya kwenye ndoa wanaume tunachangia 80% .

Embu fikiri, mtu anafahamu huyu ni Mke wa mtu na bado anaendelea kumtongoza na kumshawishi mpaka anafanikiwa. Unafikiria mume wake akifahamu hiyo ndoa itaendelea ku survive?

Kuna Hawa wanaopinga wanawake wawe watu wa nyumbani. sawa ngoja nikubaliane naye.
Baba mmoja alikuwa ni dereva bajaji posta alipata ajali akagongwa na kufa, ameacha watoto watano na kama alikuwa ni mama wa nyumbani. Embu fikiria mama huyu yupo katika kipindi gani katika kulea hao watoto?

Boss anafahamu huyu ni Mke wa mtu lakini anafanya visa kumpa kazi nyingi na kumtishia atamuachisha kazi. Hafikirii kwamba anaumiza watoto na mwanaume mwenzake ambaye yupo nyumbani kwa muda huo akimsubiri Mkewe. Tatizo ni mwanaume au kupata kazi mwanamke?

Kama yupo mwanaume ambaye mtoto wake wakike kamlea tangu udogoni mpaka anakuwa mtu mzima na anaona kijana anakaa na binti yake bila utaratibu maalumu na akaridhika ajitokeze aseme?

Kukataa ndoa kunasabbisha:

• Watoto kukosa upendo wa wazazi wote.
• Ongezeko la masingo maza
• Kama mtoto atalelewa na mama kuna hatihati aka adapt tabia za kike na kuingia katia ushoga.
• Mtoto kupitia manyanyaso Iwapo mwanamke huyo ataolewa na mwanaume mwingine, au mwanaume huyo atakaa na mwanamke mwingine hivyo mtoto huyo kupitia manyanyaso (si wote lakini.

Kuna wanaume waliotendwa kama mimi kabla sijapata Mke wangu wa sasa nikasema sitaoa. Kama ulitendwa tambua ni mwanaume mwenzako mwenye tamaa ya ngono ndio alikusabaishia.

Mwenye kupangua hoja karibu hapa.

Karibuni kwa wenye kuhitaji nguo quality tunatuma mikoani na nje ya nchi.

Kariakoo kwa sasa.
Unasema kataa ndoa ni kuhaalisha uasherati na uzinzi? Vipi mme anayeshindwa kumridhisha mke na mke kuchepuka? Vipi mke anayebania utamu na kupelekea mume kuchepuka? Hapo ndoa imetatua uzinzi? Mifano ya wanandoa wanaouana ipo mingi unaijua.

Unasema Baba akienda kazini, Mama anabaki kufatilia watoto, kupika na kufua. Kwani Baba huko anapokwenza kazini anaenda kupumzika? Baba anatafuta pesa Mama na mtoto wale, pesa hiyo hiyo ndiyo inampeleka mtoto shule, pesa hiyo ndiyo inampa nguvu mama ya kumfatilia mtoto, pesa hiyo hiyo inanunua chakula cha huyo mama kupika na chakula hicho kinampa mama nguvu ya kufua. Baba kutafuta pesa kusifananishwe na kazi za nyumbani., Zingatia hilo.

Kumbuka kataa ndoa hawataki hata hiyo unayoita sogea tuishi, wanajua hata kwenye ndoa usaiti upo kwahiyo ni bora kuzini kuliko kufanya dhambi ya usaliti + kuzini (2 in 1). Kama binti akitaka yeye mwenyewe sogea tuishi sawa ila kataa ndoa wenyewe hawataki. Kwahiyo hoja yako ya mwanaume kuishi na binti bila utaratibu imekosa mashiko hapo.

Hapo hoja ni hiyo tu watoto kukosa malezi ya Baba na Mama.
 
Na walio kwenye ndoa ndio watamu jmn maana kuna vitu wanavikosa, kule hawapewi miuono feni, style ni mojaa tuu, hakuna vionjo ila nje jamani kuna kuna kila aina ya utamu kwenye ndoa ni kuzaa tuu nje ni starehe. Kataa ndoa nawasalimia, hv mabaharia mpo kweli maana siwasikii kabisa
Alafu wewe jamaa, naomba usiniquote Tena popote unapokuta nimecomment.
 
Yale majukumu ya ndoa hatuyataki tunayaona ni mazito yanahitaji kujitoa sana. Wengi mnachukulia hili kama ubinafsi, sawa.

Sio kila anaekataa ndoa anataka watoto, watoto nao ni jukumu zito. Mtoto unaweza pata bila ndoa, ni makubaliano tu na mwanamke kataa ndoa mwenzako.

Mtoto anaweza pata malezi ya wazazi wote bila ndoa, na mtoto haharibiki kwa kukosa malezi ya wazazi wote, anaharibika ikiwa hamna maelewano kati ya wazazi.

Upweke ni suala mtambuka, kuoa/kutokua hakukuondolei upweke.

Hilo la ushoga mmesema nyie, nijuavyo hata mashoga wanataka kuoana.

Hoja ya dini siizingatii, mimi simuamini mungu, utawauliza kataa ndoa wanaomuamini mungu.
 
Halafu kuna hoja naipenda wanasema 'ndoa inatakiwa ije kama matokeo, sio kama jukumu.' yaani utakapokutana na mtu mkapendana mkaishi miaka na miaka kwa maelewano, ndo mfikirie kuoana.

Tatizo imezoeleka ukikaa na mtu muda mrefu lazima umuoe, sijui utampotezea muda, sijui utamchezea nk.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom