Wanaume tuache kujiendekeza

Wanaume tuache kujiendekeza

sijaweza kujua mwanzisha uzi anaongea kwa ushaidi au uzowefu gani
kwanza nawasiwasi na yeye kama ni mahusiano ndo kaanza kuyajua sasaivi labda
pia ajakutana na wanawake yeye anakutana na visichana vya kawaida

nashindwa elewa niandikaje ila namuombea mungu amtunze mana atakuja na uzi mwingine muda si mrefu
Ahsante kwa kuniombea MUNGU anitunze, nawe nakuombea kwa MUNGU azidi kukubariki, uje na mawazo mazuri zaidi ili tuzidi kupata elimu.
 
Hii ni sababu ya uongo kupata kutokea. Sababu ya mwanzo ya hili ni maendelei ya viwanda na wanaharakati wenyewe kupiga kauli mbiu, hili lilianza tangu karne ya 19 au 20.

Haya ya leo ni matokeo tu ya upumbavu wa baadhi ya wanawake na wanaume wenye sifs za kike. Leo mwambie mwanamke akae nyumbani kisha umletee chakula na umpe kila kitu,wstakwambia ooh, kuna leo kuna kesho je ukifa ? (Walivyokuwa mazwazwa wanafikiri wao hawafi ).

Kisha rudi katika historia.
Sheikh Jurjan, umeandika kwa hasira na matokeo yake umechanganya mambo japo lengo lako ni zuri.

Ni hivi ukiona taasisi, kampuni, asasi au hata serikali inayumba au inafanya vuzuri angalia kiongozi mkuu aliyeko madarakani kisha chunguza mienendo yake kwa maana yeye (Kiongozi) ndiye anayeweza kuiwezesha serikali/taasisi yake kuwa na maendeleo mazuri au mabaya.

Vivyo hivyo katika taasisi ya ndoa/familia, Baba (Mwanaume) ndiye kiongozi na ndiye anayetegemewa kuongoza taasisi hiyo kuelekea katika mafanikio, sasa basi Baba akiwa imara na kuongoza kwa haki familia itasonga mbele na mafanikio yataonekana na hutosikia upumbavu wa haki sawa katika familia hiyo, Baba huyo huyo akiwa lege-lege (hasa kwenye utafutaji na maamuzi) ndipo manug'uniko, dharau, ujuaji (kwa ujumla uana harakati) huanza.

Najua changamoto za maisha zipo na zitaendelea kuwepo (maana hata mimi ninazo na ninazikabili ipasavyo) lakini kiukweli wanaume wengi hasa waliozaliwa kuanzia miaka ya 1990 wana tabia ya kujiliza-liza mbele ya wanawake ili kutafuta huruma kitu ambacho binafsi kinanikera (Mfano. MC Pilipili). Lengo la uzi huu ni kuwakumbusha wanaume wa aina hiyo kuwa wasitafute mtu wa kumbebesha mizigo ya lawama pale chombo kinapoenda mrama bali wajitafute ni wapi wamekosea na wajirekebishe ili chombo kirudi kwenye mstari.

Habari ya mapinduzi ya viwanda ipo zaidi kwenye Historia na Uchumi, wataalamu wa mambo hayo wapo jukwaa la uchumi na historia.

Karibu tena!!
 
Hv mtelezo n nn
Chief, Ahsante kwa swali lako zuri. Mtelezo ni neno la mpito (mengine ni kitonga, dezo nk) ikimaanisha mtu au watu wanopenda kupewa vya bure. mfano, kula chakula asichokitolea jasho (Hasa Wanaume)/ Kuwa omba omba wakati uwezo wa kufanya kazi anao.
 
Kuna msemo maarufu miongoni mwa wanaume wapumbavu kuwa eti "WANAWAKE HAWAELEWEKI",huku ni kujazana ujinga na kuwajaza ujinga watoto wetu wa kiume kwa maana kabla hata ya kuja kwa maandiko matakatifu, asili pekee ilionyesha na kumfanya mwanaume kuwa kiongozi na msimamizi, ndio maana bila mwanaume kusimamisha uume wake, uzao hauwezi kuendelea na wanasayansi walikuja kugundua kuwa mwanaume (kupitia mwili wake na bila hiyari yake) ndiye anayeamua mtoto wa jinsia ipi azaliwe ( maana mwanamke ana cromosome x,x wakati mwanaume ana cromosome x,y). Hivyo kwa asili Mwanaume ni kiongozi wa familia (muamuzi wa mwisho) na ikitokea akakataa anakuwa amekwepa wajibu tu na hivyo anatakiwa achukuliwe hatua.

Tabia hii ya baadhi ya Wanaume wapumbavu kutowajibika ipasavyo ndiyo iliyopelekea baadhi ya wanawake kujipa mamlaka na kiburi cha kudai haki sawa na wanaume (kitu ambacho ni upotovu kwa asili), na baadhi ya wanaume wajinga ili kuhalalisha ujinga wao wakaamua kuanzisha msemo kuwa "MWANAMKE HAELEWEKI NA UKIONA UMEANZA KUMUELEWA JUA KIFO KINAKARIBIA" kitu ambacho ni uongo.

Wazee wa kipemba wana msemo wao unasema kuwa "MAPATANO NI NCHI KAVU, BAHARINI NI KUVUA TU" hivyo kwa Wanaume waerevu mapatano na mke mtarajiwa yanaanzia kwenye urafiki hadi uchumba (nchi kavu), mkiisha funga ndoa (baharini) ni kuvua tu. Sasa wanaume wengi tunafanya makosa kwenye mapatano (nchi kavu) kwa kuzingatia vitu visivyo na msingi mfano msambwanda/chura, rangi nyeupe, chuchu saa sita nk. na kuacha vitu vya msingi mfano tabia njema, ucha MUNGU nidhamu ya mtarajiwa, uvumilivu, utu wema nk. Matokeo yake mambo yakibadilika na kuwa mabaya ndani ya ndoa tunakuja na misemo ya kujihami kumbe wakati mwingine ni uzembe wetu ndo umesababisha hayo kutokea.

Rai yangu kwa wanaume ambao hawajaoa ni kuwa mjiandae kisaikolojia kwa maana FEDHA ni jibu la mambo yote, hivyo penzi la kweli na penzi la kitapeli yote yanahitaji fedha (akili kumkichwa), hivyo unatakiwa ujue kuwa wanawake na wanaume sote tunahitaji fedha kama huna tafuta kulalamika hakusaidii zaidi ya kukudhalilisha na ukiona hupati fedha basi achana na wanawake kwanza. (Simaanishi kuwa wanawake hawana upendo, wanao ila kwao kipaumbele ni ulinzi na usalama wao, hivyo Mwanamke kuolewa na Mwanaume asiyempenda lakini mwenye ukwasi, isikushangaze maana wao wanaangalia mbele)

Hivyo basi, kwa mujibu wa wanasaikolojia na wasomi mbalimbali walio elimika (Sio wasomi vyeti), ukiwa na utulivu wa akili Mwanamke anaeleweka. Kama Mwanamke uliyenaye humuelewi na umeishi naye zaidi ya miaka mitano bora umuundie tume ya uchunguzi na wajumbe wa hiyo tume iwe ifuatavyo:- Muuza urembo/Msafisha kucha, muuza nyama, Bodaboda, wenye maduka ya jirani, wauza genge na madreva tax/Uber nina hakika majibu yao yatakushangaza (Ila hii ifanyike pale utakaposhindwa kumuelewa hata baada ya kutuliza akili na kujihoji kwa kina)

Mwisho japo siyo kwa umuhimu tambua kuwa Mwanaume ni kiongozi kwa asili (Siyo kwa kuwa misahafu imeandika bali tulikuwa hivyo kabla ya misaafu kuja), hivyo tunatakiwa kujua kujiongoza wenyewe kwanza na pia tunatakiwa tujipende kwanza sisi wenyewe ili iwe rahisi kuwaongoza na kuwapenda wenzi wetu na familia kwa ujumla,tabia ya kujiliza-liza bila utaratibu na kuwalaumu wanawake kwa makosa ambayo tumeshindwa kuyazuia kizembe ni kujidhalilisha. Ukikosea ni bora kuomba msamaha kuliko kutafuta mtu wa kumtwishwa zigo lako.

UKIONA HUMUELEWE MWANAMKE ULIYENAYE JUA WEWE NDIYO HUJIELEWI KWA MAANA JUKUMU MOJA WAPO LA KIONGOZI NI KUWAJUA NA KUWAFAHAMU ANAOWAONGOZA.

#Mitandao ya kijamii
Mbona hujaweka ""STATEMENT ABOUT BIKRA""

Jokajeusi njoo uone HII MBUZI

#YNWA
 
Sheikh Jurjan, umeandika kwa hasira na matokeo yake umechanganya mambo japo lengo lako ni zuri.

Ni hivi ukiona taasisi, kampuni, asasi au hata serikali inayumba au inafanya vuzuri angalia kiongozi mkuu aliyeko madarakani kisha chunguza mienendo yake kwa maana yeye (Kiongozi) ndiye anayeweza kuiwezesha serikali/taasisi yake kuwa na maendeleo mazuri au mabaya.

Vivyo hivyo katika taasisi ya ndoa/familia, Baba (Mwanaume) ndiye kiongozi na ndiye anayetegemewa kuongoza taasisi hiyo kuelekea katika mafanikio, sasa basi Baba akiwa imara na kuongoza kwa haki familia itasonga mbele na mafanikio yataonekana na hutosikia upumbavu wa haki sawa katika familia hiyo, Baba huyo huyo akiwa lege-lege (hasa kwenye utafutaji na maamuzi) ndipo manug'uniko, dharau, ujuaji (kwa ujumla uana harakati) huanza.

Najua changamoto za maisha zipo na zitaendelea kuwepo (maana hata mimi ninazo na ninazikabili ipasavyo) lakini kiukweli wanaume wengi hasa waliozaliwa kuanzia miaka ya 1990 wana tabia ya kujiliza-liza mbele ya wanawake ili kutafuta huruma kitu ambacho binafsi kinanikera (Mfano. MC Pilipili). Lengo la uzi huu ni kuwakumbusha wanaume wa aina hiyo kuwa wasitafute mtu wa kumbebesha mizigo ya lawama pale chombo kinapoenda mrama bali wajitafute ni wapi wamekosea na wajirekebishe ili chombo kirudi kwenye mstari.

Habari ya mapinduzi ya viwanda ipo zaidi kwenye Historia na Uchumi, wataalamu wa mambo hayo wapo jukwaa la uchumi na historia.

Karibu tena!!
Kuna wanaume wanaudhalilisha sana uanaume wao.
 
"STATEMENT ABOUT BIKRA" ni mada inayojitegemea hata wewe unaweza kuiandaa siyo lazima awe Jokajeusi (Unatakiwa kujiamini). Hii mada inahusu wanaume wanaojiendekeza, halafu mimi ni Binadamu siyo mbuzi. Karibu uchangie.
Mbona hujaweka ""STATEMENT ABOUT BIKRA""

Jokajeusi njoo uone HII MBUZI

#YNWA
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Siku ukitoka hapo kwa shemeji yako ukaanza kujitegemea utabadili kauli tuu
 
Siku ukitoka hapo kwa shemeji yako ukaanza kujitegemea utabadili kauli tuu
Uzuri na ubaya wa humu ni kuwa hatujuani. Mimi ni mzee nina wajukuu sasa na ninaishi nyumbani kwangu. Kuhusu Mashemeji nimeisha wasomesha na wanajitegemea kwa sasa.
 
Narudia pale pale wanavyosema wenzangu....imagine unaingia mjini kichwa kichwa unaoa mtu kama Mama Diamond, unafikiri mambo yakiwa mabaya huko mbeleni atakuambia nini kuhusu watoto wenu mliozaa na kuwalea?
 
Narudia pale pale wanavyosema wenzangu....imagine unaingia mjini kichwa kichwa unaoa mtu kama Mama Diamond, unafikiri mambo yakiwa mabaya huko mbeleni atakuambia nini kuhusu watoto wenu mliozaa na kuwalea?
.............Du! Huo ni mtihani japo waliyotangulia walitwambia kuwa kila mtihani una "heri" ndani yake, kuijua hiyo "heri" iliyopo ndani ni mpaka ufaulu mtihani husika.
 
Ukitaka kumjua mwanamke zijue tabia za Paka, wanawake wote duniani wana tabia kama za Paka, ndio Paka huyu huyu Nyau.

wewe kaa mchunguze Paka utazijua tabia za wanawake.
Adam mwenyewe hakumwelewa Hawa pindi Mungu alipomuuliza swali,, akajibu si huyu mwanamke uliyeniletea haaaaahaaaa.
 
Adam mwenyewe hakumwelewa Hawa pindi Mungu alipomuuliza swali,, akajibu si huyu mwanamke uliyeniletea haaaaahaaaa.
Adamu alishindwa kujitambua na kutambua nafasi yake, maagizo ya kutokula lile tunda la mti wa katikati alipewa yeye kabla ya Hawa, Sasa kwa kuwa alikuwepo kabla ni dhahiri alitakiwa kumuongoza Hawa. Lakini kwa kuwa hakujielewa yeye ni nani na nafasi yake kwa Hawa ni ipi hivyo alishawishiwa na akajikuta akipokea lile tunda na kulila.

MUNGU alipokuja kumuuliza, badala ya kukiri makosa na kuomba msamaha (toba), yeye akaanza kumlaumu Hawa. Kitendo cha yeye kumlaumu Hawa kwa upande mwingine kiliashiria kuwa MUNGU alikosea kumpa msaidizi (jambo ambalo siyo la kweli). HII INATUFUNDISHA KUWA TUNAPOKOSEA TUNATAKIWA KUKIRI MAKOSA YETU NA SIYO KUTAFUTA MTU WA KUMTWISHA LAWAMA.
 
Back
Top Bottom