trudie
JF-Expert Member
- Jan 15, 2014
- 4,444
- 10,790
Tukiwa tunaianza wikiendi tulivu kabisa nawasalimu wanajukwaa wote.
Kilio changu mimi ni kwa wanaume hasa waliooa, wanaoishi na wachumba au wapenzi wao iwe kwa kutoa mahari au kinyemela ila unaishi nae. Awe kakuzalia watoto au bado Mungu hajawajalia.
Jamani wanaume waheshimuni sana wenzi wenu maana huyo ndio anayekulelea watoto wako. Usimseme vibaya mwenzi wako kwa ndugu na marafiki zako mfichie madhaifu na mapungufu yake.
Unaposhiriki kumsema vibaya jua kwamba humuaibishi yeye tuu bali na wewe unajiabisha kwa hao watu.
Wanaume jamani kamwe usikubali watu wakamwongelea vibaya mwenzi wako mbele zako na wewe ukacheka tuu mtetee onyesha kwamba wewe hufurahii hicho kitendo hata mwongeaji awe mama au baba yako mzazi mwenzi wako ni wa thamani sana.
Jambo lingine jamani wanaume usimdhalilishe mwenzi wako mbele ya watu, usimtukane wala kumkaripia. Hata akikukosea kuna sehemu sahihi ya kumwambia kosa lake ila sio mbele za watu unamfanya akose raha na kukosa "confidence". Mheshimu sana mama watoto wako maana amejitoa sana kukuletea hao watoto alibeti kifo chake kuingia leba ili tuu uitwe baba.
Mwisho kabisa wanaume wakwe zako ndio waliokufanya upate mke nae atakuletea watoto wazuri jaribu kuwaheshimu na kuwajali. Kuwajali namaanisha hata kuwasalimia na kuwatembelea angalau wanaona mtoto wetu ameenda sehemu sahihi.
Ni hayo tuu kwa leo enyi wanaume. Nawatakia wikiendi njema.
Kilio changu mimi ni kwa wanaume hasa waliooa, wanaoishi na wachumba au wapenzi wao iwe kwa kutoa mahari au kinyemela ila unaishi nae. Awe kakuzalia watoto au bado Mungu hajawajalia.
Jamani wanaume waheshimuni sana wenzi wenu maana huyo ndio anayekulelea watoto wako. Usimseme vibaya mwenzi wako kwa ndugu na marafiki zako mfichie madhaifu na mapungufu yake.
Unaposhiriki kumsema vibaya jua kwamba humuaibishi yeye tuu bali na wewe unajiabisha kwa hao watu.
Wanaume jamani kamwe usikubali watu wakamwongelea vibaya mwenzi wako mbele zako na wewe ukacheka tuu mtetee onyesha kwamba wewe hufurahii hicho kitendo hata mwongeaji awe mama au baba yako mzazi mwenzi wako ni wa thamani sana.
Jambo lingine jamani wanaume usimdhalilishe mwenzi wako mbele ya watu, usimtukane wala kumkaripia. Hata akikukosea kuna sehemu sahihi ya kumwambia kosa lake ila sio mbele za watu unamfanya akose raha na kukosa "confidence". Mheshimu sana mama watoto wako maana amejitoa sana kukuletea hao watoto alibeti kifo chake kuingia leba ili tuu uitwe baba.
Mwisho kabisa wanaume wakwe zako ndio waliokufanya upate mke nae atakuletea watoto wazuri jaribu kuwaheshimu na kuwajali. Kuwajali namaanisha hata kuwasalimia na kuwatembelea angalau wanaona mtoto wetu ameenda sehemu sahihi.
Ni hayo tuu kwa leo enyi wanaume. Nawatakia wikiendi njema.
,