Awali ya yote niseme maisha ya mtu ni yake anawajibika kwa Mungu wake tu, haya mengine ya mtu na mke/mume, mtu na mchepuko, mtu na rafiki ni mahusiano tu ya wanadamu, viumbe vingine havina haya mahusiano. Ukioa au ukiolewa usimiliki maana hati miliki ya kila mtu iko kwa Mungu. Ukitaka kufa mapema jaribu kumiliki maisha ya mtu mwingine, utapagawa kama si kufa.
Sasa, nilisikia pia, naweza kusahihishwa, kwamba baadhi ya makabila, wazaramo, hufundishwa katika jando/unyago kuwa chungu hupikwa kwenye mafiga matatu. Sasa utandawazi sio kwa nchi tu hata hizi mila zimeingia kwenye utandawazi. kwa hiyo huwa hakuna sababu ya kuchepuka inayosababishwa na mwenzi au mazingira, huwa ni maamuzi mtu anayafanya kama anavyoamua kula nyama choma, kitimoto, maini, etc na anavyofanya hayo huwa yuko responsible kwa mmiliki wa maisha yake si kwa mtu mwingine. Anakuficha wewe ili kulinda mahusiano yenu tu, siku akikufanyia live basi ujue anakubeep uanze taratibu za kusitisha hayo mahusiano.
Mwanaume ni kusaka pesa, mahusiano mengine ya kibinadamu yanazunguka kwenye hiyo pesa.