Mgeni wa Jiji
JF-Expert Member
- Jul 27, 2017
- 10,484
- 19,989
Kuna wakati haya mambo yanachangiwa na sisi sisi wanaume hasa tukiwa kwenye miaka 40 - 50 huwa tunakuwa wajinga sana kama vijana wanao balehe. Wengine huita hichi kipindi balehe ya pili ya mwanaume.
Hapa ndio pale ambapo tunakuwa wakorofi bila sababu, tunakuwa na mipango ya kando, hatueleweki na kuna wakati tunawatamkia wake na watoto wetu maneno ya ajabu. Tunasahau kuwa hayo mambo na maneno wanaishi nayo hadi uzeeni kwao.
Biblia kwa wakristu inawaasa wanaume kuishi na wanawake kwa akili, lakini wengi wetu hatuishi na wanawake (wake) kwa akili bali kwa janja janja tu. Hatujui namna bora ya kuishi nao bali tunawalaghai jambo ambalo halina afya kwa maisha ya baadae.
Mfano ni kwenye huu uzi mleta uzi ameshauri ukifika 55 utafute watoto wa uzeeni kwa mpango wa kando, huku sio kuishi na mwanamke kwa akili bali kwa janja janja tu.
Ukichunguza maeneo mengi watu wakiwashauri vijana namna za kuishi na wake zao huwa wanawashauri mambo ya hovyo sana, mara uwe mkali (unakuwaje mkali kwa mke wako?) mara hakikisha umekula kabla hujarudi nyumbani (hatujui inaumiza namna gani kumpikia chakula mtu asikile), mara uwe na mpango wa kando (usaliti) haya yote huwa ndio chanzo cha kuvuruga ndoa ya kijana yoyote.
Hautaona matokeo mapema ila amini huyo mwanamke anajuta kila mara ila hana namna sababu kwanza kashajichanganya kuolewa na wewe mtu wa hovyo, pili kashakuzalia hivyo anaangalia zaidi watoto mlionao wewe anaanza kukupuuza, sasa ngoja uzeeke au upate.ugonjwa mkali au kwa namna yoyote ugeuke kuwa mtegemezi kwake.
Hapo ndio utaona kabadilika lakini kiuhalisia sio kwamba kabadilika ila ndio wewe umefikia level sawa na yeye (level ya utegemezi) sasa unaona madhara yake. Yeye alishakuwa hivyo kitambo sana ila wewe usingeweza kuona sababu ulikuwa na uwezo wakujitegemea.
Mfano wa pili, wewe unaenda bar unakula nyama choma, pombe na mambo mengine alafu unarudi nyumbani hujabeba hata nusu kilo kwa ajili ya familia yako, wewe ni mbinafsi na siku ukigeuka tegemezi haustahili huruma ya mtu yoyote.
Hakuna mtu ambaye uzeeni anateseka kwa kutelekezwa n familia ambaye ujanani alikuwa sawa na familia yake. Wengi ukiwachunguza walikuwa wazinguaji sasa wanatafuta huruma za jamii.
Wanaume tuishi na wanawake kwa akkli na sio janja janja.
Hapa ndio pale ambapo tunakuwa wakorofi bila sababu, tunakuwa na mipango ya kando, hatueleweki na kuna wakati tunawatamkia wake na watoto wetu maneno ya ajabu. Tunasahau kuwa hayo mambo na maneno wanaishi nayo hadi uzeeni kwao.
Biblia kwa wakristu inawaasa wanaume kuishi na wanawake kwa akili, lakini wengi wetu hatuishi na wanawake (wake) kwa akili bali kwa janja janja tu. Hatujui namna bora ya kuishi nao bali tunawalaghai jambo ambalo halina afya kwa maisha ya baadae.
Mfano ni kwenye huu uzi mleta uzi ameshauri ukifika 55 utafute watoto wa uzeeni kwa mpango wa kando, huku sio kuishi na mwanamke kwa akili bali kwa janja janja tu.
Ukichunguza maeneo mengi watu wakiwashauri vijana namna za kuishi na wake zao huwa wanawashauri mambo ya hovyo sana, mara uwe mkali (unakuwaje mkali kwa mke wako?) mara hakikisha umekula kabla hujarudi nyumbani (hatujui inaumiza namna gani kumpikia chakula mtu asikile), mara uwe na mpango wa kando (usaliti) haya yote huwa ndio chanzo cha kuvuruga ndoa ya kijana yoyote.
Hautaona matokeo mapema ila amini huyo mwanamke anajuta kila mara ila hana namna sababu kwanza kashajichanganya kuolewa na wewe mtu wa hovyo, pili kashakuzalia hivyo anaangalia zaidi watoto mlionao wewe anaanza kukupuuza, sasa ngoja uzeeke au upate.ugonjwa mkali au kwa namna yoyote ugeuke kuwa mtegemezi kwake.
Hapo ndio utaona kabadilika lakini kiuhalisia sio kwamba kabadilika ila ndio wewe umefikia level sawa na yeye (level ya utegemezi) sasa unaona madhara yake. Yeye alishakuwa hivyo kitambo sana ila wewe usingeweza kuona sababu ulikuwa na uwezo wakujitegemea.
Mfano wa pili, wewe unaenda bar unakula nyama choma, pombe na mambo mengine alafu unarudi nyumbani hujabeba hata nusu kilo kwa ajili ya familia yako, wewe ni mbinafsi na siku ukigeuka tegemezi haustahili huruma ya mtu yoyote.
Hakuna mtu ambaye uzeeni anateseka kwa kutelekezwa n familia ambaye ujanani alikuwa sawa na familia yake. Wengi ukiwachunguza walikuwa wazinguaji sasa wanatafuta huruma za jamii.
Wanaume tuishi na wanawake kwa akkli na sio janja janja.