Wanaume hatufaidi ndoa, tunatumika tu kama tingatinga

Wanaume hatufaidi ndoa, tunatumika tu kama tingatinga

Hivi hii thread inahusu baba kutengwa na mke au watoto kukaa mbali na baba?

Sikia, watoto kamwe hawawezi sahau ufala uliokuwa ukiwafanyia wao na mama yao. Mimi nimelelewa kibabe najua ninachokionengea. Sio kinyongo bali ni subconscious barrier, hakuna mazoea na mzee hata iweje, na hautoona tabu kumuacha peke yake na wala hautojali.

Kama ulilelewa kirafiki na baba yako basi huwezi elewa mada.
wewe na mimi tumelelewa malezi ya aina moja,naona watu wanawatetea wakina baba hapa huenda labda wengi wa wanaotetea ni wale waliolelewa kirafiki na baba zao,ila mimi binafsi kwa namna nilivyolelewa kikatili na mzee wangu aisee ni ngumu sana kuniambia eti nimjali sana mzee kuliko mama,japo mimi ni mwanaume ila kuwa na huruma na baba yangu siwezi,NEVER EVER ni bora humu jamvini mkaniona mwanaume wa ajabu tu kuliko kubadili huu msimamo wangu
 
Nani ni mfaidi wa ndoa, kati ya mke, watoto na mme? Mstaafu wa miaka 68 alifanya kazi maisha yake yote ili familia yake iishi katika first class life style, na kulinda hiyo 'status quo' limemgharimu karibia maisha yake yote, hassling for the wife and children, akijinyima kila kitu kuhakikisha watoto wake wanasoma shule nzuri za private na wapate kozi nzuri vyuoni.

Mke wake ambaye amefikisha 60yrs amechukuliwa na mtoto wake wa mwisho Amsterdam in the Netherlands, mzee anapambana na high blood pressure, na kisukari, lakini upweke kwenye bagalow lake ndo shida kubwa kuliko, mzee hakuzaa watoto wengi aliza wawili tu. Ambao wameamua kuchukua na kulea mama yao na kuacha baba yao.

Hivi kwanini watoto hususani wa kiume wakikua wana tuchukia sisi Baba wakati sisi ni factor kubwa katika mafanikio yao?

Wanatutenga na kuthamini mama zao wengine wanatamani tufe mapema wachukue urithi loh!

NB.

1. Wanaume tujiandeni kwa wakati wa kustaafu hao watoto na wake zetu hubadilika na kuwa adui zetu tukistaafu (nolonger productive)

2. Early birth and late birth ni muhimu Zaeni watoto wa ukubwani kwa mke mdogo ukiwa 55 to 60yrs ( ukistaafu angalau uwe na wakukaa nao nyumbani, monogamy ina maumivi badaye polygamy inatatua shida zingine badaye.

View attachment 2948887
✋👋👏🎬
Safi sana sana sana ....
 
Hii ndio scenario Ilivyo mimi na mzee, ule ukuta kati yangu na yeye uko mpaka leo hata kwenye simu haizid dakika mbili mazungumzo yashaisha na si kwa makusudi ila kutokana na ukauzu wake aliokuaga nao..
Ilifika muda mzee atasubiri ukosee ndio akuseme, ukiwa na shida basi huna uwezo wa kumwambia mpaka umwambie mama ndio amwambie mzee.. Automatically ile connection unashtuka haipo mpaka uzeen na hapo yeye wala hajui kwann watoto hatuna story nae
Atakapo watoka ndo mtakimbuka umuhimu wake kuepo duniani mtaomba msmaha kwanini hamkuhudumia zaidi, Baba zetu sio watu wakutubembeleza ila wana umuhimu sanaa.
 
Kitu ulichoandika hapa unaonekana una umri mdogo sana yaani chini ya miaka 25.

Jukumu la msingi la Baba ktk familia ni kuhakikisha familia iko salama na kupata mahitaji yote msingi ndani uwezo wake.

Ukiwa mwanaume (Baba) siku zote jambo la msingi kwetu ni kuheshimika tu sio kupendwa. Watoto wajinga wajinga ndio huwa wanamsahau Baba.
Kwa mfano leo ni mepinga mtoto wangu 13yrs limepewa suspension shuleni kwa kuvunja dirisha la bweni, mama ake kalifungia chumbani eti nisimpige zaidi,.... huo ushezi siwezi kuvumilia kisa ni pendwe eti nikizeeka hapana
 
Kwa mfano leo ni mepinga mtoto wangu 13yrs limepewa suspension shuleni kwa kuvunja dirisha la bweni, mama ake kalifungia chumbani eti nisimpige zaidi,.... huo ushezi siwezi kuvumilia kisa ni pendwe eti nikizeeka hapana
kwa hiyo kesi huyo mwanao ndo amekosea,ila kwa sisi wengine tunaposema tumelelewa kikatili na wazee(baba) wetu hatumaanishi scenarios kama hiyo yako,watu tumebeba mengi sana mengine hakuna haja ya kuyaweka humu jf
 
Atakapo watoka ndo mtakimbuka umuhimu wake kuepo duniani mtaomba msmaha kwanini hamkuhudumia zaidi, Baba zetu sio watu wakutubembeleza ila wana umuhimu sanaa.
Wewe swala la kumuhudumia ni swala lingine.. halafu mzee ni mtu anajiweza.. Na hata akitaka msaada siwez kukataa kama uko ndan ya uwezo..
Nachozungumzia mimi ni ukaribu tu kati yangu mimi na yeye.
 
Muwamba ngoma.....hii part ya mwanaume inaelezewa mwanaume katenda memaaaa katenda memaaaa maishani mwisho kazeeka katengwa, serious????

Hii situation sometimes iko hivi, mwanaume ukiwa na nguvu zako unakua kivuruge, kivuruge kweli, kama ni mlevi mlevi mbwa kero nyingi....unavumiliwa tu, wakati unavumiliwa hata mioyoni watu wanakutoa inabaki ile basi tuuuu.....ukishazeeka sasa huna nguvu za kupiga sarakasi muda huo unataka urudishe mapenzi na upendwe huo moyo wa kupendwa haupooo inabaki tu huruma ya kibinadamu, ndo muda huu zinaibuka ngonjera za kutengwa.

Kuwa mwema wakati wote, usisubirie kipindi huna nguvu
Ulichoelza hapa ni baadh ya situation ambazo huchangiq baba kutojaliwa.....Base kwnye hali alisemea mwenye Uzi tafadhal
 
Dawa Mwanaume mwenzang pambana ujanan mwako, Pata pesa wekeza uwezavyo kwaajil ya uzee wako....Achana na habar ya kutegemea watoto au ndugu, au mke utakufa kabla ya muda......
 
Jenga ukaribu na watoto wako toka wakiwa wadogo.. ili wawe connected na wewe.. kwa mwendo huo hata ufanye jambo gan la maana sheikh bado utapigwa bao tu uzeen na mwanamke
Chagua kujenga ukaribu au usimame kama baba familia istawi kimaadili na kiuchumi. Mzee wangu alikuwa mkali na alitudiscipline haswa ila kamwe siwezi kusahau alivyotujenga na kutuhudumia ili tustawi katika dunia hii haswa kwa mtoto wa kiume. Naletewa mashtaka kila siku na mama, mara hili mara lile ila namwambia mama mmeshafika uzeeni hayo mambo waachieni vijana ishini kwa amani sasa. Nitamsikiliza ili apate amani yake ya moyo ila baba yangu atabaki kuwa baba yangu, hata akalale na vimada mia uko ila najua alivyotutunza sisi na mama kwaujumla. Sio haki yangu wala nafasi yangu kumuadhibu mzee kwasabanu actually alitunoa kwasababu ningelelewa soft katika dunia hii ngumu ya upambanaji sijui ningekuwa wapi. Perform your duties and responsibilities hayo ya kutaka kupendwa au kulelewa ni akili ya mtoto mwenyewe asipokuwa na kutambua hali halisi ya maisha ilivyo ni upumbavu wake yeye mwenyewe.
 
Dawa Mwanaume mwenzang pambana ujanan mwako, Pata pesa wekeza uwezavyo kwaajil ya uzee wako....Achana na habar ya kutegemea watoto au ndugu, au mke utakufa kabla ya muda......
Safi sana sana sana 👏👋✋🙏
 
Chagua kujenga ukaribu au usimame kama baba familia istawi kimaadili na kiuchumi. Mzee wangu alikuwa mkali na alitudiscipline haswa ila kamwe siwezi kusahau alivyotujenga na kutuhudumia ili tustawi katika dunia hii haswa kwa mtoto wa kiume. Naletewa mashtaka kila siku na mama, mara hili mara lile ila namwambia mama mmeshafika uzeeni hayo mambo waachieni vijana ishini kwa amani sasa. Nitamsikiliza ili apate amani yake ya moyo ila baba yangu atabaki kuwa baba yangu, hata akalale na vimada mia uko ila najua alivyotutunza sisi na mama kwaujumla. Sio haki yangu wala nafasi yangu kumuadhibu mzee kwasabanu actually alitunoa kwasababu ningelelewa soft katika dunia hii ngumu ya upambanaji sijui ningekuwa wapi. Perform your duties and responsibilities hayo ya kutaka kupendwa au kulelewa ni akili ya mtoto mwenyewe asipokuwa na kutambua hali halisi ya maisha ilivyo ni upumbavu wake yeye mwenyewe.
hayo ya kutaka kupendwa au kulelewa ni akili ya mtoto mwenyewe asipokuwa na kutambua hali halisi ya maisha ilivyo ni upumbavu wake yeye mwenyew............umenena point mkuu
 
Atakapo watoka ndo mtakimbuka umuhimu wake kuepo duniani mtaomba msmaha kwanini hamkuhudumia zaidi, Baba zetu sio watu wakutubembeleza ila wana umuhimu sanaa.
Tatizo sio kuhudumia mzee. Mzee atakula, atavaa, ataishi anavyotaka, vyote nitamfanyia.

Tatizo ni ile connection ya kirafiki ya baba na mtoto wake wa kiume. Haipo kabisa. Mnaishi kama majirani hivi. Au kijeshi kati ya askali mkubwa na mdogo, kila kitu kipo formal na kufuata commands. Baba yako unakuwa unamuogopa zaidi ya Mungu.

Haucheki na mzee. Ni "ndio mzee" kwenda mbele, usipomsikiliza utajuta kuwa hai. Faida niliyoipata ni nimekuwa mbabe na competitive aggressively.

Kuna wale mmelelewa kibabe lakini mzazi bado alikuwa karibu. Mimi nimelelewa kibabe na mzee alikuwa haangaliki machoni, akirudi usiku mnakimbilia vyumbani na akiwepo sebuleni hapakaliki. Hamuwezi kuelewa aisee.

Watoto wangu nimewazaa mwenyewe nataka nicheze nao na nifurahi nao, nifurahie creation yangu mwenyewe. Sio wanione kama lishetani fulani hivi. Hili nataka niliepuke kwa akili zangu zote.
 
Muwamba ngoma.....hii part ya mwanaume inaelezewa mwanaume katenda memaaaa katenda memaaaa maishani mwisho kazeeka katengwa, serious????

Hii situation sometimes iko hivi, mwanaume ukiwa na nguvu zako unakua kivuruge, kivuruge kweli, kama ni mlevi mlevi mbwa kero nyingi....unavumiliwa tu, wakati unavumiliwa hata mioyoni watu wanakutoa inabaki ile basi tuuuu.....ukishazeeka sasa huna nguvu za kupiga sarakasi muda huo unataka urudishe mapenzi na upendwe huo moyo wa kupendwa haupooo inabaki tu huruma ya kibinadamu, ndo muda huu zinaibuka ngonjera za kutengwa.

Kuwa mwema wakati wote, usisubirie kipindi huna nguvu
Coment ya mwaka hii....

Ifanyiwe lamination , kisha iwekwe kwenye ubao wa matangazo pale nje ya hall la kikao cha wanaume.

Ni muhimu wajikumbushe hili kila wanapokutana kwenye vikao vyao.
 
Tatizo ni ile connection ya kirafiki ya baba na mtoto wake wa kiume. Haipo kabisa. Mnaishi kama majirani hivi. Au kijeshi kati ya askali mkubwa na mdogo, kila kitu kipo formal na kufuata commands. Baba yako unakuwa unamuogopa zaidi ya Mungu.
Hii ndo style babangu alitulea ,
Alikuwa mkali km pilipili , haelezeki tulikuwa tunamwita rambo

Ila kwa sasa anayaona matokeo yake, hatuna ukaribu nae
tunaishi mkoa mmoja lkn ndo tunaweza maliza miez 3 hatuja onana, hii tabia ina muumiza , inamkula lkn ndo alivyotulea

Siku akikuita nyumbani unaanza kujiuliza kwan nimekosea nn?? Unaanza kuuliza kwa maza km kuna msala wowote ujipange kabla hujaenda
 
1. Kichwa kinalalama wanaume hawafaidi ndoa.....!!! Kwanza kufaidi ndoa ni kupi? Ninini ama ni kitu gani ambacho huyu mume hafaidi na anaona wanaofaidika na ndoa ni wanawake na watoto.....

2. Mwanaume kutumika kama tingatinga....
Bado najiuliza, hapa mwanamke hatumiki..??? Mtoto hatumiki?
Ama, kutumika ni nini? Ama kutumikaje?

Mada ni pana sana, licha ya maswali hapo juu twende nayo hivyohivyo kwa upana kufikia muafaka ama maelewano, maana ndo suluhu kubwa jamii inataka.

Kwanza hakunaga formula kwenye ndoa kwa maana namna ya kuendesha ndoa, kila ndoa inanendeshwa kutokana na yanayoikabili. Pia hakuna formula ya kulea watoto, mtoto yuko kwa namna yake na hulka zake, unakuta wamezaliwa 5 wote wamelelewa nyumba 1 na wazazi aina 1 ila 3 wanakuwa na adabu na maisha, 2 hawashikiki yaani wameshindikana...


Nikirudi kwenye mada, wacha niende kwa mifano kama 2 au 3 hivi kama hali itaruhusu.

1. Dingi mhasibu na mkewe mkunga wote dini moja wamepata watoto 5. Dingi anakuwa na safari za kikazi na kusafiri na mkewe na watoto hadi nje ya nchi, dingi ni mhasibu mbobezi. Kazi yake ilimfanya asionekane nyumbani, ila jumamosi na jumapili haendi kazini anashinda siku nzima kalala, ikifika saa 10 jioni anaamka, mke anamuandalia mlo anakula kisha anatoka kurudi usiku mnene. Watoto wamekua wanamuona mdingi anafatwa na SU tai kila siku kurudishwa jioni na SU, akirudi analala hadi saa 11 au 12 jioni anajiandaa kutoka na kurudi usiku mnene. Kesho tena mzunguko unaendelea. Dingi anaghqrimia familia mahitaji yote maana saa ingine anasema kuna hela nimemuachia mama yenu kwa matumizi fulani hivyo watoto wanatambua wajibu na mchango wa baba.

Mama ndo anaamshana na watoto jumatatu hadi ijumaa kuwaandaa shule, wakirudi wakute chakula tayari, mama awafundishe kufua nguo zao, usafi wa vyumba vyao. Mama aende kanisani na watoto awafundishe kutoa sadaka, kupanda daladala, kutengeneza bustani za maua na mbogamboga, kufuga kuku, kushona nguo iliyochanika na huku mama ni mkunga....

Mdingi anajisahau au sijui ndo asili, anaanza kutupa mbegu huku na kule, watoto wa nje wanazaliwa kunakuwa na tafrani, mke anakuwa kimyaaa, watoto wanaletwa ndani ya nyumba mke anawalea pamoja na watoto wake wa mwanzo. Hawa watoto wa nje hawaishi kiasi cha dingi kustaafu bado anarusha mbegu tuu.... ila mke yuko kimya analea.

Wale watoto wana mamazao ambao waliwatelekeza wakalelewe kwa baba yao wakakuta mke kajaa, ila wale watoto wakiita mama basi ujue wanamuita huyu mama mlezi sio mama zao wazazi. Dingi kuona haitoshi 60+ anahamia shamba anavuta binti na kuendelea kupata watoto....!!! Okay....

Wakati dingi ameenda shamba, kamuacha mke kwenye mji mwenyewe, mke nae kajistaafia anaendelea kumuabudu Bwana wa Mabwana..... miaka 5 mbele watoto wanamvuta mama na dingi ulaya kwa matembezi, maana baadhi ya watoto wanaishi huko. Dingi anaona hakuna raha huko bora akae shamba anazungukwa na watoto wajukuu...!
Watoto wakamchukua mama ulaya mazima, dingi shamba kukawa shubiri, mafao ya EA yalikata, hela hakuna watoto wadogo wanataka kusoma intanesheno dingi nehi, ila nyumba na mashamba anayo.
Ile kero ya matumizi ya anasa anayodaiwa na watoto kule shamba akaona bora are arejee mji wake mjini, hakuna neno..... yuko pekeyake anaishi mwenyewe....

Sasa huyu katengwa, kajitenga au karma imemtenga na familia japo katengeneza ya uzeeni pia...? Mke huko ulaya hana mpango wa kurudi bongo amenawiri na kuwa bimbi bomba...!

2. Dingi mtumishi wa umma, miradi yote ya serikali yeye ndo anafanya bajeti, anaandikia propozo na ikipita anafanya kazi na makandarasi na kutoa ripoti kwa wakuu wake. Huyu anaondoka nyumbani saa 1 au 12 asubuhi kurudi saa sita usiku.... sii jumapili wala siku za sikukuu yeye ni workaholic, ila familia anaihudumia vyema. Na mara nyingi (watoto 3) anawapa watoto pesa mkononi wanunue wanachotaka na saa ingine anatoka nao kwenda matembezini ila akipotea nyumbani humuoni.
Mkewe mama wa nyumbani anapambana na malezi ya watoto na ndugu wanaokuja kutaka msaada, mume alitumbuliwa...... (uzuri alikuwa na HELA) hivyo maisha hayakubadilika hakuna aliyejua kama dingi hana kazi, alijua kutunza hela zake alizokuwa anazikusanya. Mtoto mdogo keshamaliza chuo saa hii wanasuguana mgongo na mkewe,hawa walioana kabila moja japo mkewe ni chapombe.


3. Dingi alikuwa na kazi shirika binafsi pesa ipo, wanawake kila kona ila mke anavumilia. Safari moja hakurudi nyumbani ambapo si kawaida yake, mama kumekucha anasema ngoja nikanunue vocha anakutana na gari la mumewe limepaki mtaa wa 2, kugonga mlango mumewe anatoka na taulo....!!!

Mke akarudi nyumbani kimyaaaa maisha yakaendelea, hawa walipata watoto 2. Mke nae alikuwa anafanyq kazi UN huko anacheocheo tuu. Sasa baba akaanza kustaafu mama kaendelea na kazi alipogonga 60 nae kastaafu. Muda wote huo mke anavumilia mapichapicha ya mume, kumbe ana hesabu zake.

Wiki 1baadq ya mama kustaafu akawaita mumewe na watoto wao ambao wameshaanza kazi, akawaambia, nilikaa kwenye hii ndoa sio kwa raha ni ilinyie mpate malezi ya baba na mama na mkue vyema. Wajibu huo nimeumaliza, nimewaita hapa nahamia kwangu (mke kajenga kajumba ka vyumba 2 kinachojitegemea hapo Tegeta). Anaacha jumba la kifahari la mumewe na magari yake, pension ya UN sio ya kitoto.
Watoto wako mama kwanini, sasa huu si ndo muda mzeeshane mkae pamoja hakuna tena matatizo, mke akasema nimewaita kuwapa taarifa sio ushauri, hapa naondoka na nguo zangu tuu.
Dingi akaanza kulia, watoto kuita ndugu waingilie kati mke anasema fanyeni mnalotaka hapo sirudi.


Huyu mke alifikwa? Utajiulizana mhehe huyu? Mbona hakujinyonga wakati anapigwa matukio? Dingi bado ana mshiko pia sema uzee, upweke....

Ogopa ama kaa mbali na mtu anayeweka vinyongo na kupanga mipango yake ya baadae bila kukushirikisha hata kama si ya kukudhuru.

Sina jibu la nini kifanyike, ila walau kila mmoja ajue kula na kipofu,hakuna aliyemkamilifu. Funika kombe mwanaharamu apite.

Ukiweza acha mambo yatayoleta doa kwa mwenzano, ukishindwa fanya asijue, akijua omba upate patna anaye react hapohapo, wale wanaokaa kimya wakisubiri muda ukifika wakuachie pira, aahaha unalooo.
Unajikuta uji unaupoozea tumboni.

Kasinde Matata.
 
Back
Top Bottom