Jenerali Ambamba
JF-Expert Member
- Sep 8, 2014
- 3,344
- 2,537
Kuna Kisa kimoja nataka niwashirikishe.
Mkabala na Nyumba niliyohamia hivi karibuni baba mwenye nyumba alifariki dunia, baba huyu aliacha mke na watoto kadhaa, aliacha na mali zikiwemo Nyumba, sasa huyu baba ni mjita na mke wake ni mkerewe, Mama huyu baada ya mume kufariki ndugu walikuja na kugawa urithi kwa "watoto", wa marehemu, mama yao akapewa chumba kimoja tu, na watoto wakapewa chumba kimoja kimoja katika nyumba hyo, Nyumba ina vyumba 6, kila mtoto alipewa chumba kimoja na mama yao akapewa chumba kimoja, sasa watoto wamishaoa, na kuolewa lakini vyumba vyao wamepangisha wapangaji, na pesa zinazopatikana kwa kupangisha mama yao anawatumia huko walipo, Sasa unakuta kwa mfano nyumba au choo/bafu linahitaji ukarabati, pesa za kufanyia ukarabati hakuna, mama yao anaishi maisha ya shida, na anasema kuwa hizo ndo mila za wajita!! ebo.
Hivi kuna aja gani ya kugawa urithi kwa watoto wakati mzazi mmoja bado yu hai?
Vijana ambao hadi tunaoa bado tunang'ang'ania urithi wa wazazi wetu ni sahihi?
Kwa nini wanaume hata wanawake tusiandae wosia mapema hata wa mdomo tu?
Mkabala na Nyumba niliyohamia hivi karibuni baba mwenye nyumba alifariki dunia, baba huyu aliacha mke na watoto kadhaa, aliacha na mali zikiwemo Nyumba, sasa huyu baba ni mjita na mke wake ni mkerewe, Mama huyu baada ya mume kufariki ndugu walikuja na kugawa urithi kwa "watoto", wa marehemu, mama yao akapewa chumba kimoja tu, na watoto wakapewa chumba kimoja kimoja katika nyumba hyo, Nyumba ina vyumba 6, kila mtoto alipewa chumba kimoja na mama yao akapewa chumba kimoja, sasa watoto wamishaoa, na kuolewa lakini vyumba vyao wamepangisha wapangaji, na pesa zinazopatikana kwa kupangisha mama yao anawatumia huko walipo, Sasa unakuta kwa mfano nyumba au choo/bafu linahitaji ukarabati, pesa za kufanyia ukarabati hakuna, mama yao anaishi maisha ya shida, na anasema kuwa hizo ndo mila za wajita!! ebo.
Hivi kuna aja gani ya kugawa urithi kwa watoto wakati mzazi mmoja bado yu hai?
Vijana ambao hadi tunaoa bado tunang'ang'ania urithi wa wazazi wetu ni sahihi?
Kwa nini wanaume hata wanawake tusiandae wosia mapema hata wa mdomo tu?