Wanasiasa tambueni kuwa Wananchi tumeshachoka kuvurugwa, kaeni myamalize, habari za huyu kafanya hivi mara yule kafanya vile tumezichoka

Wanasiasa tambueni kuwa Wananchi tumeshachoka kuvurugwa, kaeni myamalize, habari za huyu kafanya hivi mara yule kafanya vile tumezichoka

Pakome

JF-Expert Member
Joined
Dec 8, 2024
Posts
1,541
Reaction score
916
Ifike mahali kelele za kila siku ziishe

Too much is harmful

Wanasiasa tambueni kuwa Wananchi wanafuata maelekezo yenu

Mkisema nchi itulie basi itatulia
Mkisema iwake basi itawaka

Ninyi ndio wenye uamuzi wa mwisho kabla ya matokeo

Twendeni Mataifa makubwa tuone namna yametulia na yanafanya kazi bila kelele

Twendeni China tuone utulivu

Twendeni Japan tuone utulivu

Twendeni Ujerumani tuone utulivu

Wananchi wametulia wanafanya kazi hawana kelele

Tupatwe na wivu mkubwa wa kutulia kama wao

Kila siku kelele za huyu kafanya hivi yule kafanya vile zinaharibu nchi

Dunia itasonga mbele sisi tutachelewa mwisho tutaonekana wajinga kwasababu wenzetu watafanikiwa sisi tutabaki na kelele za kisiasa zisizokwisha
Kaeni mezani fanyieni kazi yote yanayopigiwa kelele
Uzuri ni kuwa yote hayo ni mambo ya kuzungumzika wala sio ya kushikiana visu na mawe

Visu na mawe yalikuwa maisha ya zamani karne ya kwanza
Karne hii tuliyopo sio ya kushambuliana kama fisi kana kwamba sisi ni wanyama

Wanasiasa kaeni chini myamalize kwasababu ninyi ndio wenye uamuzi wa mwisho na Wananchi tunafuata maagizo yenu

Mkieleza Wananchi mambo mema basi watafanya lakini pia mkiwaeleza mabaya watafanya pia
 
Back
Top Bottom