Wanasheria naombeni ushauri kuhusu suala hili

Wanasheria naombeni ushauri kuhusu suala hili

Holoholo

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2023
Posts
8,703
Reaction score
19,589
1. Jamaa ni bodaboda alimzalisha mwanamke mtoto wa kiume nae wakamuita ALEX

2. Hawakuoana hivyo mwanamke alijifungua akiwa nyumbani kwao.

3. Baada ya kujifungua mwanamke ameishi na mtoto kwa taabu sana kama miezi 10 mwanamke akachukua maamuzi ya kumpeleka mtoto kwa huyo jamaa

4. Jamaa hakumkataa akamchukua,ameishi nae gheto siku mbili akaona ni vema zaidi mtoto ampeleke kwa ndugu ili aendelee vzr na boda yake

5. kweli akampeleka kwa ndugu, mtoto alikuwa amekondeana sana,mama yake hajali,yule ndugu akamlea kama mwanae huyo mtoto na afya ikakaa sawa,

6. Imepita miezi kama mitano hivi mama wa mtoto anaenda kwa ndugu huyo akiwa na hasira,anadai mtoto wake, wakamkatalia ndugu wanasema kumtoa mtoto mpaka idhni ya babake nae huyo mwanamke hataki kuwasiliana na ba mtoto

6. Leo tena amekuja anadai mtoto wake,

7. Maswali yananijia je huyo mama apatiwe mtoto bila hata idhni ya mzazi mwenzie? 8. Je hizo huduma zilizokosekana mpaka zikasababisha mtoto apelekwe kwa baba yake zimepatikana? 9. karibuni wanasheria
 
Maswali yananijia je huyo mama apatiwe mtoto bila hata idhni ya mzazi mwenzie? 8. Je hizo huduma zilizokosekana mpaka zikasababisha mtoto apelekwe kwa baba yake zimepatikana? 9. karibuni wanasheria

Wakaliongelee hili suala Polisi Dawati la Jinsia na watoto.

Na Mtoto atatoka baada ya idhini ya mzazi mwenzie.
Na idhini itatoka baada ya makubaliano ya namna gan nzur mtoto atalelewa kwa huyo Mama.

Hapo ndio wataangalia kama zile sababu za kupelekwa mtoto kwa baba zimetatuliwa au bado.

Ila ni vyema mtoto akalelewe na Mama.
Baba atoe matumizi. Wasaidiane kulea.
 
Pale wajinga wawili wanaponyanyasa kiumbe kisicho na hatia!
Ok yeyote Kati yao anaweza kupewa mtoto itategemea na maelezo yao!
1.baba anaweza kudai kuendelea kubaki nae kwa sababu bidada alimtelekezea
2.sheria itamtaka abaki nae yeye na sio kumpeleka kwa ndugu
3.bidada anaweza kutoa sababu zenye mashiko za kwanini alimtelekeza mtoto na Sasa hivi anamtaka!
Nimechoka kutype!
 
Wewe jamaa unaandika sana humu, kwa siku sijui thread ngapi.....

Hata ukiwa na jambo serious huwezi kupata engagement.... most of hizo thread ni mashudu .....

Mda mwingine jifunze kuwa tu msomaji ! Ni hayo

Mtu anaona uzi, kaandika flani tayari anajua hizi ni pumba, anapita kama anaaga maiti
 
Pale wajinga wawili wanaponyanyasa kiumbe kisicho na hatia!
Ok yeyote Kati yao anaweza kupewa mtoto itategemea na maelezo yao!
1.baba anaweza kudai kuendelea kubaki nae kwa sababu bidada alimtelekezea
2.sheria itamtaka abaki nae yeye na sio kumpeleka kwa ndugu
3.bidada anaweza kutoa sababu zenye mashiko za kwanini alimtelekeza mtoto na Sasa hivi anamtaka!
Nimechoka kutype!

Mdada atachambwa sana na wale Polisi wa Kike. Ila mwishon atapewa mtoto. Maana mtoto bado mdogo.

Hata miaka 2 hana.
 
Mdada atachambwa sana na wale Polisi wa Kike. Ila mwishon atapewa mtoto. Maana mtoto bado mdogo.

Hata miaka 2 hana.
dah kuna sheria zingine bhana, hata wewe ungemuona huyo mtoto alivyokuwa amekondeana,mbavu,uti wa mgongo nje yaani unaweza kujamlaani mama japo ni mama mzazi wa huyo mtoto,mtoto amelelewa kanawili eti now mama mzazi anajitokeza tena anamtaka,
 
1. Jamaa ni bodaboda alimzalisha mwanamke mtoto wa kiume nae wakamuita ALEX

2. Hawakuoana hivyo mwanamke alijifungua akiwa nyumbani kwao.

3. Baada ya kujifungua mwanamke ameishi na mtoto kwa taabu sana kama miezi 10 mwanamke akachukua maamuzi ya kumpeleka mtoto kwa huyo jamaa

4. Jamaa hakumkataa akamchukua,ameishi nae gheto siku mbili akaona ni vema zaidi mtoto ampeleke kwa ndugu ili aendelee vzr na boda yake

5. kweli akampeleka kwa ndugu, mtoto alikuwa amekondeana sana,mama yake hajali,yule ndugu akamlea kama mwanae huyo mtoto na afya ikakaa sawa,

6. Imepita miezi kama mitano hivi mama wa mtoto anaenda kwa ndugu huyo akiwa na hasira,anadai mtoto wake, wakamkatalia ndugu wanasema kumtoa mtoto mpaka idhni ya babake nae huyo mwanamke hataki kuwasiliana na ba mtoto

6. Leo tena amekuja anadai mtoto wake,

7. Maswali yananijia je huyo mama apatiwe mtoto bila hata idhni ya mzazi mwenzie? 8. Je hizo huduma zilizokosekana mpaka zikasababisha mtoto apelekwe kwa baba yake zimepatikana? 9. karibuni wanasheria

Kama wanamjua ni Mamaake nini kinawazuia kumpatia mtoto wake?

Mambo mengine hayahitaji kesi. Mtoto ni Mali ya Mwanamke. Kisha anafuata Baba, kisha ndugu, ndio wengine wanafuata.

Mpigieni ndugu yenu mwambieni Mama wa motto kaja kumchukua mtoto wake.
 
Kuna jamaa najua lazima atakuja na maneno"mambo yao mwaachie mwenywe"hapend kujitesa kutype
 
Wewe jamaa unaandika sana humu, kwa siku sijui thread ngapi.....

Hata ukiwa na jambo serious huwezi kupata engagement.... most of hizo thread ni mashudu .....

Mda mwingine jifunze kuwa tu msomaji ! Ni hayo

Mtu anaona uzi, kaandika flani tayari anajua hizi ni pumba, anapita kama anaaga maiti
Unaona kama nilivyoona mimi yani jamaa sijui mda wa kuanzisha nyuzi hata kumi kwa siku sijuagi anapataga wapi aise yan huwezi ingia jamiiforum kwa siku bila kukuta uzi wake mpya wa siku inakela sana tafuta kazi uwe busy
 
Unaona kama nilivyoona mimi yani jamaa sijui mda wa kuanzisha nyuzi hata kumi kwa siku sijuagi anapataga wapi aise yan huwezi ingia jamiiforum kwa siku bila kukuta uzi wake mpya wa siku inakela sana tafuta kazi uwe busy
Kila saa thread, ilimradi nae kapost !!! Ujinga
 
dah kuna sheria zingine bhana, hata wewe ungemuona huyo mtoto alivyokuwa amekondeana,mbavu,uti wa mgongo nje yaani unaweza kujamlaani mama japo ni mama mzazi wa huyo mtoto,mtoto amelelewa kanawili eti now mama mzazi anajitokeza tena anamtaka,
Sheria siyo hisia. Huyo baba hakumchukuwa mtoto kisheria ndipo shida ilipoanzia. Angempeleka mtoto ustawi wa jamii, wamune halafu wampe idhini ya kukaa naye.
 
Depending on how the father can defend his position.. Tafuteni ushahidi wa mtoto kuteswa na kuteseka akiwa kwa mama yake. Hiyo ni sababu kubwa ya kutokumrudishia mtoto mama Mzazi. Kuzaa tu sio sababu ya kupewa custody. Anaweza kupewa visitation right ila sio custody kama tayari ashaonesha poor judgement. Mtoto Bado anatakiwa kunyonya ila mama alimkatili akamwachisha. Hiyo tu ni strong reason ya kumyima mtoto.
 
Back
Top Bottom