Camp Gilgal
JF-Expert Member
- Dec 13, 2014
- 4,453
- 4,594
Upuuzi!
Waziri wa Viwanda na Biashara Ndugu Charles Mwijage amesema kwamba kuanzia mwakani watu wote wanaovaa nguo za nje watazomewa ili kulinda viwanda vya nguo vya ndani.
Hakutakuwa na wa kumzomea mwenzake kwa sababu tutaendelea tu kuvaa za nje maana hakuna namna!
Watu hukimbilia vya nje kwa kufatana na ubora wake, hivi vya ndani ili vitufae na tuachane na vya nje ni wao na viwanda vyao kuhakikisha ubora usiopingika na ikiwezekana wafikie viwango vile vya nje au zaidi, hapo wala hakutakuwa na haja ya kumzomea mtu, automatically watu tutajikuta tukivaa vya ndani na kuachana na vile vya nje! Nchi ina mikakati ya kuelekea kwenye mapinduzi ya viwanda, ngoja tuendelee kuomba yawe wanayoyakusudia.
Waziri wa Viwanda na Biashara Ndugu Charles Mwijage amesema kwamba kuanzia mwakani watu wote wanaovaa nguo za nje watazomewa ili kulinda viwanda vya nguo vya ndani.
Anayenikera mimi ni Waziri wa Afya, kwa nini naye hatangazi tumzomee kila atakayeenda kutibiwa nje ili kukuza hospitali za ndani?