Wanaoutaka urais 2015: Yupi anafaa?

CANCER Wewe humjui Magufuli hata kidogo. Mimi kwetu ni Biharamulo, kabla ya kutengwa na kuanzishwa jimbo la Chato tulikuwa na jimbo la Biharamulo likijumuisha Chato na Biharamulo na mwaka 1990 Magufuli aligombea akitokea Chato na mpinzani wake alikuwa marehemu Phares Kabuye, Magefuli alishindwa vibaya na Kabuye kwa kupata kura chache sana Biharamulo, ila tangu hapo akajenga chuki na watu wa Biharamulo.

Mwaka 1995 lilianzishwa jimbo la Chato na yeye kufanikiwa kuwa mbunge na baadae Waziri, ila cha kushanganza amefanya vitimbi vikubwa sana vya kuhakikisha kila project inayoihusu Biharamulo ya Miundombinu haifanikiwi. Barabara ya Mwanza-Bukoba ilikuwa inapita Biharamulo ila yeye kaamua kuipitisha Chato kitu ambacho si kibaya ila kibaya ni kuwa kuna 70km za barabara ya vumbi mpk Biharamulo na ni eneo hatarishi kwa majambazi na jamaa ameapa hatoweka rami kwa sababu watu wa Biharamulo walimkataa (inakuchukua zaidi ya masaa mawili distance fupi km hii).

Sasa huyu jamaa akiwa rais akaamua kulipa visasi kwa watu wote wenye anaofikiri walitofautiana nae unadhani itakuwaje? Huyu nae bado kwani sie tunamjua vizuri na ndo maana alipigana Chato ijitenge na mkoa wa Kagera na akawa anataka makao makuu ya mkoa mpya wa Geita yakae Chato ila imeshindikana. Huyu bwana ni mbinafsi.


Na mnastahili mbaki bila lami hivyo hivyo. Mmewezaje kumwacha mpiganaji kama huyu na kwenda kuchagua watu wasio na uwezo. Huoni kama mmetucheleweshea maendeleo ya Taifa kwa kumchelewesha Magufuli kuja kututumikia..?
 
ninichojua kiongozi mzuri hapimwi kwa uwezo wake wa kujenga hoja majukwaani...ule utaratibu wa zamani wa usalama wa taifa kufuatilia nyendo za vijana tangu wakiwa mashuleni sijui uliishia wapi?? zamani ilikua ukionekana una mashiko kwa jamii kulikua na watu wana trace background yako toka kijijini kwenu , familia yako, umesoma wapi na mambo kama hayo NDIO KILIKUA KIPIMO KIZURI CHA UONGOZI

Sasa hivi umebadilika....shughuli kubwa ni kutoa kucha na kung'oa meno tu
 
Bora umewaambia ndugu yangu, watu wanafikiri kubwabwaja na waandishi wa habari ni Urais. Quote again ''Wazee wa hekina na busara wako kimya kabisa ndio watakaotoa Rais wetu 2015''.:flypig:

Busara yao iliisha kwa kumchagua huyu ******
 
Rais Anatoka kwenye system wanamtandao wenyewe wanakwambia sasa sijui ni yupi yetu macho

Inaekea kuwa mwenzetu bado unaamini kuwa Rais lazima tu atoke CCM ................. hata baada ya kudhihirika wazi kuwa wameshindwa kutuongoza vema.
 
Hafai huyu aliuza nyumba zetu za serikali kwa bei ya kutupa na mpaka leo hataki kukiri kosa lake..mbabe na ana-umimi kama Zito

hivi ukitafuta mtu asiyye na kosa kabisa basi hatutapata kiongozi sababu kila mtu ana mapungufu yake ndio maana tunaangalia mchapa kazi other factors remain constant.
 
Kama umejituma basi you are a let down in the first place. Kwanini unakubali kujikomba kana kwamba huna la kufanya la maana kwa ajili yako, familia yako na taifa lako? Think twice.
 
ninichojua kiongozi mzuri hapimwi kwa uwezo wake wa kujenga hoja majukwaani...ule utaratibu wa zamani wa usalama wa taifa kufuatilia nyendo za vijana tangu wakiwa mashuleni sijui uliishia wapi?? zamani ilikua ukionekana una mashiko kwa jamii kulikua na watu wana trace background yako toka kijijini kwenu , familia yako, umesoma wapi na mambo kama hayo NDIO KILIKUA KIPIMO KIZURI CHA UONGOZI


Siku hizi wakijua unakipawa chauongozi wanang'oa meno kaka we acha tu
 
kwa Dr Magufuli kuna vijineno viwili VITATU tu dhidi yake!
1.NYUMBA ZA SERIKALI akiwa Waziri wa Ujenzi awamu ya Pili
2.VISASI kuna mtu kaelezea viiiiiiiizuri hapo juu
3.Peter's PRINCIPLE:KUNA HATARI YA KUMPANDISHA MAGUFULI HADI TAIFA ZIMA LIKATAMBUA UBINAFSI,UBABE, UDHAIFU WAKE>ANAHITAJI KUONGOZWA PIA MAANA NI MPENDA SIFA-OPPORTUNIST!

Ngoja nikusaidie kidogo tu ndugu yangu inaonekana uelewa wako ni mdogo juu ya nyumba za serikali na kazi za mawaziri ni kwamba Waziri humshaauri Rais juu ya jambo analoliona kwa uelewa wake kuwa halifai, lakini ni hiari ya Rais kukubali ushauri au kuukataa ushauri wa Waziri wake yeyote, hapo dhambi ya Magufuli iko wapi? Magufuli kama alivyo binadamu yoyote ukiwemo wewe na mimi tunamapungufu yetu tunachoangalia ni ni advantage na disadvantage ya huyo mtu percent ikizidi kwenye faida unamchukua na ikizidi kwenye hasara unamwacha ila kamwe dhambi ya nyumba ni ya Mkapa. Dr. Pombe hakuwa na uwezo wa kuuza nyumba yoyote ya serikali bila idhini ya Ben, na hatatokea duniani binadamu atakayewaridhisha watu wote, hata ukipewa wewe uongozi utalaumiwa tu, wameshindwa mitume na manabii wakaambulia kuuawa itakuwa Magufuli!!! Dr. Magufuli hana chema hata angetoa roho yake mtasema anapenda sifa ndiyo maana kajitoa roho. Mungu anajua nani atatuongoza baada ya JK hatuna sababu ya kulumbana kwa kuwasema watu vibaya wakati kazi wanazofanya zinaonekana. Kwa mfano ni waziri gani katika historia ya nchi hii alishakataa barabara iliyojengwa kwa msaada wa nchi yoyote kwa maelezo kwamba ina kasoro tofauti na Magufuli? Pale TANROAD alikuwepo Mrema aliyeshindikana mpaka kwa wabunge walishindwa Dr. Shukuru kwawambwa pia alimshindwa lakini Magufuli aliporudi Ujenzi Mrema mwenye ajira na sifa zenye utata yuko wapi? Tatizo kubwa kwetu watanzania tumezoea kubembelezwa na kudanganywa kama watoto tunafurahi sana. Lakini tukiambiwa ukweli inakuwa tatizo na tatizo la Magufuli ni kusema ukweli na kusimamia anayoamini ni ya kweli hana kasoro nyingine. Na mwajiri wake anajua kuwa ni mchapa kazi ndiyo maana kila baraza la mawaziri likivunjwa yumo huo ni uthibitisho tosha kwamba anafaaa ni mawaziri wangapi wameshaachwa toka JK aingie madarakani angalia wengine hata mwaka hawakumaliza mfano Waziri Maige, (Simon Mbilinyi, Juma Ngasongwa Enzi ya BWM) na wengineo kuingia tu uwanjani wakapewa kadi nyekundu tena kwa mambo ambayo hawakuyafanya.
 
Kama mtu asiyekuwa na akili ameuweza urahis magufuli atashindwa vipi?

Santo huogopi kung'olewa kucha na meno kusema baba riz1 hana akili? shauri yako watafuatilia modemu yako mpaka ulipoiweka siajabu hutaonekana tena hapa JF maana Mabwepande iko shughuli kama hujui muulize zombe na ulimboka watakuambia mimi huyoooooooooooooooooooooooooooooooooooooooo vichakani.
 
kunakijana aliyesoma UDOM mwasisi wa kikundi cha class struggle na aliyewahi kuwa waziri wa chakula na uwekezaji anaitwa Richard Mtui naona huyo anafaa kuwa rais wa Tanzania tumtafute tumuombe anatufaa.

Richard Mtui nimwsoma naye anafaa kuwa waziri wa chakula jinsia na wanawake
 
Wadau;
Watu wenye dhamira ya dhati kabisa kabisa ya kuifanya nchi hii kuendelea Ki- Viwanda na Ki- Uchumi wamebakia kuwa Madereva taxi na Vinyozi tu, Wengine woote ni wachumia tumbo. Period !

Mimi nilishasema, wanaojulikana hawafai, wanaofaa hawajulikani.

Kwa sababu ili kujulikana inabidi uanze chini kwenye ubunge ubunge huku.Na huko kumejaa rushwa tupu na dirty party politics.

Kwa hiyo watu wenye uwezo na integrity wanashindwa.

Wanaoweza mikiki hiyo na kuja kuibuka kwenye national politics wanakuwa wachafu tayari na kwa hivyo hawafai.
 
Ni magufuli aliyesimamia uuzwaji wa nyumba za serikali kwa bei ya kutupa. Nyingine alimgawia mchumba na mdogo wake. HAFAI KUWA RAIS
 
Kwa hali inayoendelea hivi Tanzania inatia shaka bado miaka mitatu kufika uchaguzi mkuu wa uraisi na wabunge 2015, lakini kila kukicha mapya yanajitokeza kwa watu kutaganza nia ya watu kujitangazia kuwa na sifa za kuutaka uraisi, mmoja alisema anasubiri Mungu amuoteshe na kudhihirisha akasema ana maadui 11 ambao 2016 mara baada ya kuoteshwa watakibiria kenya, hiyo inaonyesha dhamira iliyojificha na ulipaji visasi, bado kuna magwinji mengine ambayo yalishaanza harakati zamani kama EL, SS, FS, ambao wanamitandao ndani ya chama chao cha chukua chako mapema.

Ukija kwa upande wa CDM nako mambo yameanza kupamba moto mara nina sifa za kuwa amri jeshi mkuu wa nchi ili hali hata familia hana , mara kiongozi mkuu wa chama anataka, mara mheshimiwa Dr. Slaa, vile vile inetokea wengine wanasema tangu uhuru hatujatoa raisi wakati tuna uwezo, mara tunataka mwislam.

Hizi sio ishara nzuri vile vile kiongozi ambaye nimzuri sio lazima ajipe sifa mwenyewe kuwa anaweza kusema hivyo vyote alivyokuwa anafanya ni unafiki , vile kiongozi kuweza kumpita na kusema ni mwadilifu na mzalendo lazima awe amefanya kazi na kudhibitisha hilo bila shaka na sio kuongea na kukosoa tu, mfano bunge lililopita kilango, mwakembe, ole sendeka, sita tulifikiri ni wazalendo wanatetea watanzania lakini leo hii sio, vile vile zito kasi yake sio ile.

kwa hali hiyo tusidanganyike na porojo za kuwa naweza ili hali ni njaa tu. Kwa hali tuliyonayo na kuangalia ukomavu wa siasa Dr. Magufuli anafaa kuwa raisi ila sio kupitia CCM. Anasifa na amedhihilisha kwa kuwa na misimamo akiwa serikalini , sio mdini, mkanda wala mjenga mitandao.
mkuu hapo kwenye blue pana husika!!! mimi huyu jamaa nampenda sana,ila shida ndo hiyo yuko kwenye kile chama kileee...sio siri akibadili chama hata mimi kura ntampa mana uwezo anao na amedhiirisha hilo kwa misimamo yake tofauti na huyu DHAIFU!!
 
Kuna jambo huwa nadhani watu wengi huwa hawajiulizi kabla ya kufanya maamuzi ya kujitangazia kuwa wanautaka urais. Watu hawa huwa fikra zao huishia kuwa kuwa rais ni kula bata na starehe za kufa mtu. Kumbe lah. Nadhani mkimuuliza JK kwa sasa hamasa aliyokuwa na mawazo aliyokuwa nayo wakati anautafuta urais kwa udi na uvumba atakupa jibu tofauti ingawa kwa sasa hali ilivyo ni siri yake. Naelewa kuwa mtu yeyote anao uhuru wa kukitafuta kiti hicho lakini.....sidhani kama wengi huwa wanajiuliza unyeti wa nafasi hiyo.
 
Back
Top Bottom