Wanaoutaka urais 2015: Yupi anafaa?

Wanaoutaka urais 2015: Yupi anafaa?

hivi wana jf kati ya hayo majina yote kuna mtu ambaye amefikia hatua ya kuwaongoza watanzania kwa kipindi cha miaka mitano uchaguzi utakapo malizika 2015?
Au ni nani mwenye sifa za kusimama na kuwa eleza watanzania kuwa akiwa raisi atatuletea maendeleo na kuwafungulia kesi mafisadi wote..au ambaye atakubali mdahalo na mgombea kutoka upinzani.
Kwa maoni yangu sijaona hata mmoja kwa sababu wote baba yao ni mmoja na mama yao ni mmoja...naona kama chadema wataingia ikulu bila vikwazo vya aina yeyote cha msingi ni wao kumteua mgombea ambaye atakubalika kwa watanzania na atakaye leta matumaini makubwa kwa watanzani.

Achana Na majina kila Mwaka mmebadili majina lakini mambo watanzania wanazidi kuwa masikini ms kukosa hata huduma muhimu na mafisadi wanazidi kuneemeka!

Achana Na CCM kama unataka maendeleo ya wote
 
Angalia kwa jicho la 3,ccm inamiliki hati ya nchi,na nchi inakopesheka,wako tayari kukopa mpk kiwango cha mwisho ili wactoke madarakani(wagawe rushwa hadi kwa watoto wa umri chini ya miaka18) Tuendeleeni kuwaelimisha wananchi tu kuhusu haki zao nakuwazuia kuuza haki zao kwa kipande cha khanga,

kweli kabisa mkuu masanjasb elimu inahitajika zaidi kwa wananchi wetu kabla ya kujadili majina
 
We Mleta hii hoja hujamsikia Dkt Slaa mchana huu kwenye Thread iliyoanzishwa na 'gamba'kawakataza kujadili huu Upuuzi jengeni chama kuanzia ngazi ya shina badala ya kushinda humu kuanzisha habari za kujipendekeza. Mnakera sana kwa hili nipo pamoja na Babu!


Wewe Songoro kuna wakati unaweka point za maana kwenye hizi thread. Lakini somewhere unajikuta huyo, tayari usharudi kutetea chama chako. Hapa kwa mfano, madai yako kuwa kuna watu wanashindahumu kuanzisha habari za kujipendekeza. Maudhui ya sentensi hii ni kukatisha watu tamaa kuweka mawazo yao humu kwa hofu watakuwa wanajipendekeza. Hii sentensi yako imekaa kipropaganda sana ujue. Waache watu watoe mawazo yao bila hofu ya kujipendekeza. Kwanza hata wakijipendekeza kuna tatizo gani. Kujipendekeza ni sehemu ya siasa, and its OK.

Wewe mwenyewe hapo ulipo unajipendekeza Makao Maku Madogo Lumumba wakutoe ngazi ya wilaya labda pengine wakupe Mkoa.

Now back to the Issue: CCM ina mtandao mkubwa sana wa matawi, kwa hiyo ni tishio kwa yeyote atayetafuta nafasi ya Urais. Nani atafaa watajua wao. Lakini ukweli utabaki palepale yeyote watayemchagua atakuwa jiwe gumu kwa sababu wana uzoefu katika mambo haya, wana fedha--halali na haramu, wana dola. Hata wakimweka Wasira bado itabidi vyama vya upinzani vijipange vizuri kumkabili.

Kwa upande wa pili, tatizo la CHADEMA halitakuwa kwenye nafasi ya Urais. Watu wamekichoka sana CCM atayewekwa na CHADEMA kwenye nafasi ya Urais hatakuwa na tatizo sana. Kazi kubwa kwa upande wa CHADEMA itakuwa kwenye Ubunge. Huwezi kuunda Serikali bila Wabunge wa kutosha. Kwa hiyo chama hiki cha Ushindani kina kazi kubwa sana kuandaa serikali kwa maana ya kuandaa wabunge.

CCM wameliona hili wanakipunguzia CHADEMA kasi ya kuunda serikali imara 2015 kwa njia ya kukipunguzia kasi vijijini. Kwani kwa kufanya hivyo watakosa wabunge wa kutosha, na hivyo itakuwa vigumu kuunda serikali yenye nguvu.

Tukio la kumpiga bomu mwandishi pale Iringa, kulifungia Mwanahalisi na haya matukio ya Mabwepande na kukataza maandamano vimeleta hofu sana miongoni mwa wananchi. Wanai slow down CHADEMA kupata wabunge 2015 and therefore kushindwa kuunda serikali imara wakati huo.

Songoro, nakuhakikishia wakati huu ni mwafaka kwa CHADEMA kuidhibiti hofu ya polisi, TISS na JW kama wanataka kupata idadi ya kutosha ya wabunge 2015. M4C ni lazime isidumazwe na kitu chochote. Ukumbuke msemo huu: The most fearful enemy of any man or woman is fear itself.

CHADEMA MUST OVERCOME FEAR kuunda serikali 2015.
 
Ijapo siipendi CCM. Ninawakubali sana Mwakyembe na Magufuli. Hawa jamaa ni tunu ya taifa wanaweza kazi ya kuliongoza taifa. Lakini kwa kuwa watu wana maslahi yao binafsi hawawezi kuwapa hawa jamaa urais waingoze nchi hii kwa sababu madili yao yatafutika.
 
Wewe Songoro kuna wakati unaweka point za maana kwenye hizi thread. Lakini somewhere unajikuta huyo, tayari usharudi kutetea chama chako. Hapa kwa mfano, madai yako kuwa kuna watu wanashindahumu kuanzisha habari za kujipendekeza. Maudhui ya sentensi hii ni kukatisha watu tamaa kuweka mawazo yao humu kwa hofu watakuwa wanajipendekeza. Hii sentensi yako imekaa kipropaganda sana ujue. Waache watu watoe mawazo yao bila hofu ya kujipendekeza. Kwanza hata wakijipendekeza kuna tatizo gani. Kujipendekeza ni sehemu ya siasa, and its OK.

Wewe mwenyewe hapo ulipo unajipendekeza Makao Maku Madogo Lumumba wakutoe ngazi ya wilaya labda pengine wakupe Mkoa.

Now back to the Issue: CCM ina mtandao mkubwa sana wa matawi, kwa hiyo ni tishio kwa yeyote atayetafuta nafasi ya Urais. Nani atafaa watajua wao. Lakini ukweli utabaki palepale yeyote watayemchagua atakuwa jiwe gumu kwa sababu wana uzoefu katika mambo haya, wana fedha--halali na haramu, wana dola. Hata wakimweka Wasira bado itabidi vyama vya upinzani vijipange vizuri kumkabili.

Kwa upande wa pili, tatizo la CHADEMA halitakuwa kwenye nafasi ya Urais. Watu wamekichoka sana CCM atayewekwa na CHADEMA kwenye nafasi ya Urais hatakuwa na tatizo sana. Kazi kubwa kwa upande wa CHADEMA itakuwa kwenye Ubunge. Huwezi kuunda Serikali bila Wabunge wa kutosha. Kwa hiyo chama hiki cha Ushindani kina kazi kubwa sana kuandaa serikali kwa maana ya kuandaa wabunge.

CCM wameliona hili wanakipunguzia CHADEMA kasi ya kuunda serikali imara 2015 kwa njia ya kukipunguzia kasi vijijini. Kwani kwa kufanya hivyo watakosa wabunge wa kutosha, na hivyo itakuwa vigumu kuunda serikali yenye nguvu.

Tukio la kumpiga bomu mwandishi pale Iringa, kulifungia Mwanahalisi na haya matukio ya Mabwepande na kukataza maandamano vimeleta hofu sana miongoni mwa wananchi. Wanai slow down CHADEMA kupata wabunge 2015 and therefore kushindwa kuunda serikali imara wakati huo.

Songoro, nakuhakikishia wakati huu ni mwafaka kwa CHADEMA kuidhibiti hofu ya polisi, TISS na JW kama wanataka kupata idadi ya kutosha ya wabunge 2015. M4C ni lazime isidumazwe na kitu chochote. Ukumbuke msemo huu: The most fearful enemy of any man or woman is fear itself.

CHADEMA MUST OVERCOME FEAR kuunda serikali 2015.

aliyesema hataki ujipendekeze kwake ni slaa, songoro amemnukuu tu..... Kama we unaona kuna umuhimu wa kujigonga go on ila siku ya mwisho utadharaulika tu
 
Najadili nadharia ya kujigonga katika siasa. Hiyo ndiyo jadi ya taaluma hiyo. Wanasiasa huwa wanatangaza CV zao kujipendekeza, wanapewa mafunzo ya public speaking wajue jinsi ya kuji-market bora zaidi. Kujipendekeza ndiyo hasa jadi ya siasa. Kwa hiyo sijali nani katumia neno hilo kujipendekeza kwa maana ya kukataza watu waliopo katika siasa kujipendeza. Kujipendekeza hakuna tatizo lolote katika siasa. In fact kujipendekeza hakuna tatizo lolote katika kitu chochote unataka--iwe kazi fulani au binti fulani unataka kumdo. Katika biashara hiyo inaitwa personal selling. Na ni kitu poa kabisa. Au wewe ulisikia wapi mtu anakatazwa kuji market? Mimi nashindwa kujadili comment ya Slaa kuhusu kujipendekeza kwa sababu sijui context ya neno hilo katika hoja yake. Nimemjibu Songoro hivyo kwa sabu nimeelewa context ya post yake hiyo niliyoijibu.

aliyesema hataki ujipendekeze kwake ni slaa, songoro amemnukuu tu..... Kama we unaona kuna umuhimu wa kujigonga go on ila siku ya mwisho utadharaulika tu
 
Back
Top Bottom