PSALM_1
JF-Expert Member
- Jan 1, 2013
- 289
- 100
Hapo itabidi uwasiliane na huyo jamaa wa india.Mkuu kusiristi naogopa sana kwani NECTA hawatabiriki
Lakini kwa hii kashfa ya kufeli wanafunzi wengi hudhani wizara ya elimu na NECTA wanaweza wakajirekebisha. Wapo waliorudia mitihani na wakafaulu, nina imani utafaulu ukirudia mitihani ya geography au physics hata hesabu.
Mimi naona kama ukiendelea na CBG, ukirudia mtihani wa geography utakuwa na uwezekano mkubwa wa kupata at least C.
Kama ukiendelea na PCB, ukirudia mtihani wa physics utakuwa na uwezekano mkubwa wa kupata C.
Mipango ya kwenda kusoma nje huwa inachukuwa muda, wakati mwingine muda mrefu. Kwa sasa hivi nakushauri fanya vitu viwili kwa wakati mmoja.
Kwanza: jiandikishe A-level ya private, na jiandikishe kurudia mtihani, physics au geography na somo lolote lingine rahisi kwako kufaulu.
Pili: Fuatilia mpango wa kwenda nje ya nchi(wakati unaendelea kupiga A-level yako), safari iki wahi kabla hujamaliza A-level safiri. Safari ikichelewa endelea kula shule yako huku ukisubiri. Usikae nyumbani kusubiri hivihivi, usikubali kupoteza muda.