Wanaorusha Video YouTube, Facebook, Periscope n.k Wawe na Leseni Ati?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991


Kuna taarifa zinasambaa kuwa TCRA imetaka kina Millard Ayo na Michuzi na bila ya shaka wengine ambao wanarusha video mbalimbali ambazo zinaonekana kama habari au produced kama habari wawe ne leseni za kutangaza.

Hivi ni genius gani huko ndani amekuja na wazo muflisi kama hili? Na wanaotumiana video wenyew kwa wenyewe au kuonekana "live" siyo kwambba watatakiwa wawe na leseni? au wanaotumia mitandao kurusha "live" training kutoka sehemu moja kwenda nyingine nao watatakiwa wawe na leseni?

Ni wakati gani mawasiliano yatachukuliwa kama yako kwenye "private" realm na siyo "public" realm? Je, watu wote walioko Tanzania wanaoposti vitu mbalimbali (ambavyo vinaweza kuangukia kwenye 'electronic communication') watahitaji kuanzia sasa kuwa na leseni? Hii ikiwemo ni wanamuziki, bloggers n.k?

========

Barua iliyosainiwa na Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Mhandisi James Kilaba ya tarehe 30 Januari 2017, imevitaka vyombo hivyo kuacha mara moja kutoa huduma za TV mtandaoni.

“Kwa mujibu wa kifungu 13 (1) cha Electronic and Postal Communications Act Cap 306, sheria za Tanzania zinahitaji watoa huduma zozote za aina hiyo wawe leseni kutoka mamlaka ya mawasiliano,” imesema barua hiyo.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Jamii Media, Mamlaka ya Mawasiliano ilizitembelea Ofisi za kampuni hiyo mwishoni mwa mwaka jana(2016) ili kujiridhisha na Programu mpya ya JamiiLeo inayorushwa kwa mtindo wa Video katika YouTube, Instagram na Facebook kisha kuwekwa JamiiForums ikichambua habari kuu 3 za siku na maoni ya wananchi kutoka mitandaoni.
 
Hii nchi maajabu hayaishi!!! Leseni kwa ajili ya kuupload video youtube?

Basi kila raia atakaeupload video yoyote yenye kuonekana kama habari atatakiwa kuwa na Lesseni inamanisha wataishiwa karatasi za Lesseni kwa sababu itabidi watengeneza Millionis and Millionis za Leseni!! Halafu media inayotumika haina usajili Tanzania sasa Leseni ya nini?

Hii nchi werevu wako pembeni NANGA ndio zinaongoza
 
Lengo la huu utawala ni kuzuia watu wasizungumze nakupashana habari. Hii ndiyo kauli mbiu yao......inaenda sambamba na hapa kazi tu.

Lakini wewe Mwanakijiji si ulikuwa una-support sana hii serikali? Leo unaona ajabu wakifanya haya? Na wala hawataishia hapo wataendelea tu kubana uhuru wa habari.
 
Yani watu bado hamjafumbuka macho duh mimi ninachijuona wanaona bado kama uhuru wa habari upo sasa wanabana kabisaaa hata kale kaupenyo uje uangalie tbc hahahahahaha
 
Yani watu bado hamjafumbuka macho duh mimi ninachijuona wanaona bado kama uhuru wa habari upo sasa wanabana kabisaaa hata kale kaupenyo uje uangalie tbc hahahahahaha
Mkuu kinachotakiwa ni kuombea tuu na sio vingine. ukitaka weka sala ya malaika mlinzi kesi huna na huhitaji leseni!
 
Back
Top Bottom