Wanaoongoza kuinyonya Afrika sasa ni Asia, sio wazungu au Magharibi

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,660
46,350
Wazungu wamekuwa wakitupiwa lawama kwa kiasi kikubwa kwamba wanafanya njama za kuinyonya na kuididimiza Africa lakini uhalisia unakataa kwa kuangalia mambo kadhaa.

1. Uagizaji wa magari kutoka nje ndio manunuzi makubwa zaidi katika biashara ya Africa na Serikali za Africa ndizo waagizaji wakubwa zaidi wa magari ya kifahari muuzaji mkubwa wa magari hayo akiwa Japan.

2. Silaha inayotumika zaidi katika vita, migogoro, ugaidi, uasi na mauaji barani Africa ni AK-47 ambayo ni bunduki inayouzwa na Urusi.

3. Muuzaji mkubwa wa nguo japo nyingi ni hafifu kwa ubora hapa Africa kwa sasa ni China. Wakulima wa Bariadi wanaozalisha pamba wanauza kg 1200 ambapo shati moja kutengenezwa halimalizi hata Kg1 halafu wanakuja kuuziwa hilo shati kwa 10,000. Hapo bado hatujazungumiza viwanda vyetu vya nguo kuuwawa kifo cha mende na bidhaa hizo za mchina.

6. Afrika Chakula kingi tunachoagiza ni ngano, sukari na mafuta kutoka Russia, India, Brazil na China.

7. Wajenzi wakubwa waliochukua kandarasi muhimu za ujenzi wa Africa kwa Sasa katika kila sekta ni Wachina. Kama ni 10% za miradi, ubora hafifu wa miondombinu au kudumaa kwa makandarasi wa ndani wao Wachina ndio wa kulaumiwa.

8. Sehemu kubwa ya dawa za Africa kwa sasa zinatoka India. Hata dawa ambazo zingewezwa kutengenezwa Africa zinatoka huko.

9. Biashara kubwa za madawa ya kulevya Africa zinahusisha zaidi nchi za Asia kama China, India, Iran na Pakistan. Pia biashara haramu za ujangili zinahusisha watu kutoka maeneo hayo.

10. Muendeshaji bandari mkubwa zaidi na katika nchi nyingi kwa sasa Africa ni DP World ambao ni Waarabu.

Mataifa ambayo yanalaumiwa sana na kushitumiwa kwa conspiracies za kuikandamiza Africa wanachimba madini tu ambayo angalau hata yanatoa ajira za kueleweka na yana uwazi kiasi. Pia sehemu kubwa ya mapato kupitia Utalii na misaada ni kutoka hayo mataifa na zaidi sana hayo mataifa hata husomesha raia wa kiAfrica katika elimu bora zaidi.
 
Kwa maana hiyo Tuwakatae wa Russia, Wachina na Waasia wengine.

Najiuliza, hivi ikiwa Ak 47 inatengenezwa Katika nchi nyingi, including the U.S.A, Kwanini asingiziwe mrashia pekee?
 
Tukisema hii ni Scramble for Africa, mnakataa.

Sasa tatizo lipo wapi hapa.?

Mashangingi? Mashangingi yanatoka Japan pekee?

Biashara? Biashara na Nchi tajwa ni tatizo?

Nani atakaye faidika kama tukikubali kwamba Warashia, wachina Wajapan "Wanainyonya Afrika?"

Manake tukikataa kufanya nao biashara na kununua nguo au hata chakula, kutoka huko itakuwaje?

Hii rai ya "Diplomasia ya Uchumi" itaishia wapi.

Huko kufungua nchi itaishia wapi? Hata sijui ilifungwa vipi kwa sababu hakuna mtu ambaye ameweza kutufafanulia Nchi ilifungwaje?



Ndio kusema tulime wenyewe au. Tujivike wenyewe?

Sasa kwanini mlikuwa mnakataa njia za Hayati?

Wakala nao.
 
Wazungu wamekuwa wakitupiwa lawama kwa kiasi kikubwa kwamba wanafanya njama za kuinyonya na kuididimiza Africa lakini uhalisia unakataa kwa kuangalia mambo kadhaa.

1. Uagizaji wa magari kutoka nje ndio manunuzi makubwa zaidi katika biashara ya Africa na Serikali za Africa ndizo waagizaji wakubwa zaidi wa magari ya kifahari muuzaji mkubwa wa magari hayo akiwa Japan.

2. Silaha inayotumika zaidi katika vita, migogoro, ugaidi, uasi na mauaji barani Africa ni AK-47 ambayo ni bunduki inayouzwa na Urusi.

3. Muuzaji mkubwa wa nguo japo nyingi ni hafifu kwa ubora hapa Africa kwa sasa ni China. Wakulima wa Bariadi wanaozalisha pamba wanauza kg 1200 ambapo shati moja kutengenezwa halimalizi hata Kg1 halafu wanakuja kuuziwa hilo shati kwa 10,000. Hapo bado hatujazungumiza viwanda vyetu vya nguo kuuwawa kifo cha mende na bidhaa hizo za mchina.

6. Afrika Chakula kingi tunachoagiza ni ngano, sukari na mafuta kutoka Russia, India, Brazil na China.

7. Wajenzi wakubwa waliochukua kandarasi muhimu za ujenzi wa Africa kwa Sasa katika kila sekta ni Wachina. Kama ni 10% za miradi, ubora hafifu wa miondombinu au kudumaa kwa makandarasi wa ndani wao Wachina ndio wa kulaumiwa.

8. Sehemu kubwa ya dawa za Africa kwa sasa zinatoka India. Hata dawa ambazo zingewezwa kutengenezwa Africa zinatoka huko.

9. Biashara kubwa za madawa ya kulevya Africa zinahusisha zaidi nchi za Asia kama China, India, Iran na Pakistan. Pia biashara haramu za ujangili zinahusisha watu kutoka maeneo hayo.

10. Muendeshaji bandari mkubwa zaidi na katika nchi nyingi kwa sasa Africa ni DP World ambao ni Waarabu.

Mataifa ambayo yanalaumiwa sana na kushitumiwa kwa conspiracies za kuikandamiza Africa wanachimba madini tu ambayo angalau hata yanatoa ajira za kueleweka na yana uwazi kiasi. Pia sehemu kubwa ya mapato kupitia Utalii na misaada ni kutoka hayo mataifa na zaidi sana hayo mataifa hata husomesha raia wa kiAfrica katika elimu bora zaidi.
Wananyonya kwa kushirikiana na watala wetu wasiokuwa na haya.

Alafu utakuta watala haohao walnawacheka wakina chief mangungu wa msowelo..
 
Tukisema hii ni Scramble for Africa, mnakataa.

Sasa tatizo lipo wapi hapa.?

Mashangingi? Mashangingi yanatoka Japan pekee?

Biashara? Biashara na Nchi tajwa ni tatizo?

Nani atakaye faidika kama tukikubali kwamba Warashia, wachina Wajapan "Wanainyonya Afrika?"

Manake tukikataa kufanya nao biashara na kununua nguo au hata chakula, kutoka huko itakuwaje?

Hii rai ya "Diplomasia ya Uchumi" itaishia wapi.

Huko kufungua nchi itaishia wapi? Hata sijui ilifungwa vipi kwa sababu hakuna mtu ambaye ameweza kutufafanulia Nchi ilifungwaje?



Ndio kusema tulime wenyewe au. Tujivike wenyewe?

Sasa kwanini mlikuwa mnakataa njia za Hayati?

Wakala nao.

Uneongea ujinga gani dogo?!
 
Kiwanda cha nguo Urafiki kimegeuka kuwa magodown yawachina na bidhaa zao.

Maghorofa yake ya Urafiki yamegeuka ofisi za mabus ya wabongo.

Soko lote la nguo Tanzania liko chini ya mchina na mhindi wenyewe tunakuna sharubu tu.

Tumezidiwa maarifa na akili Kila mahala, tuko busy na siasa za CCM na CDM, mipira na udaku wakina Mwijaku na Juma Lokole.
 
Back
Top Bottom