Afrika tuwape wazee Urais, ni hatari kuwakabidhi vijana mamlaka makubwa

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,661
46,349
Naona baadhi ya watu wanashangilia kama jambo jema na kubwa sana kwamba kuna kijana wa miaka 44 kutoka chama cha upinzani huko Senegal anakaribia kutwaa madaraka ya Urais baada ya kupigiwa kura nyingi zaidi na raia wa huko.

Watu wanaoshangilia jambo hili wanasahau kwamba mojawapo ya matatizo makubwa ya watawala wa Africa ni kung'ang'ania madarakani kwa muda mrefu, na wengi wa ving'ang'anizi wa madaraka walianza kutawala wakiwa vijana wenye umri mdogo sana.

Unapomchagua mtu mwenye miaka 44 ina maana akitawala miaka 10 kama zilivyo katiba za nchi nyingi anatakiwa aondoke madarakani akiwa na miaka 54, sasa hapo ndipo sarakasi za kucheza na katiba huwa zinaanza kwa sababu inakuwa bado mapema mno kwake na kwa wapambe wake.

Marais katika nchi nyingi za Africa wanatakiwa waingie madarakani angalau na umri kuanzia miaka 65 ili akitawala miaka 10 inakuwa imefika 75 na anakuwa amechoka kuendelea kutawala na kufanya mapambano ya kisiasa, anamwachia mwingine. Vinginevyo kuwapa madaraka vijana kuna hatari ya kutawailia na mtu mmoja hata miaka 20 au 30 kama ilivyo katika nchi nyingi za Africa.

Zaidi naamini wazee wana uzoefu na busara zaidi za kuongoza katika nafasi kubwa kuliko vijana, pia hata inakuwa rahisi kuwafahamu kutokana na majukumu yao mbalimbali waliyokwisha kupitia.
 
Watu wanaoshangilia jambo hili wanasahau kwamba mojawapo ya matatizo makubwa ya watawala wa Africa ni kung'ang'ania madarakani kwa muda mrefu, na wengi wa ving'ang'anizi wa madaraka walianza kutawala wakiwa vijana wenye umri mdogo sana.
Historia inatabia ya akujirudia ndio maana Combination ya Kiswahili, historia na Isamic knowledge vimewekwa.

Mifano ni mingi lakini kwa uchache ni hivi Madikiteta woote
1. Rwanda
2. Zimbabwe
3. Uganda
4.DRC
Bora aanze akiwa mzee akikataa kuondoka uzee unamwondoa.
 
Una hoja ya msingi, lakini tatizo kubwa ni kuwa na katiba zinazowalinda Marais. Bila kuwa na katiba zinazozipa taasisi nguvu na kumpa mtu nguvu, hata akiingia madarakani na miaka 70, Bado anaweza kufanya uhuni. Mfano Mugabe, Museveni, Paul Biya nk. Hawa wote ni wazee lakini uhuni wao uko wazi peupe.
 
Tatizo siyo umri, Nchi inabid iwe na Katiba ambayo haiwez kuchezewa bila kujali nani raisi na ana umri gani

Kwa maelezo yako Mu7 angesha achia madaraka
Angeachia lini? M7 alianza kutawala miaka ya 1986 wakati mmoja na Mwinyi, yeye M7 alikuwa na miaka 42 wakati Mwinyi alikuwa na 60, ina maana hapo kulikuwa na miaka kama 20 kwanza ya ku cover gap la miaka ya Mwinyi kabla ya kuongeza mingine, Pia ukumbuke kadri mtu anavyokaa madarakani ndio inakuwa vigumu zaidi kuyaachia madaraka.
 
Naona baadhi ya watu wanashangilia kama jambo jema na kubwa sana kwamba kuna kijana wa miaka 44 kutoka chama cha upinzani huko Senegal anakaribia kutwaa madaraka ya Urais baada ya kupigiwa kura nyingi zaidi na raia wa huko.

Watu wanaoshangilia jambo hili wanasahau kwamba mojawapo ya matatizo makubwa ya watawala wa Africa ni kung'ang'ania madarakani kwa muda mrefu, na wengi wa ving'ang'anizi wa madaraka walianza kutawala wakiwa vijana wenye umri mdogo sana.

Unapomchagua mtu mwenye miaka 44 ina maana akitawala miaka 10 kama zilivyo katiba za nchi nyingi anatakiwa aondoke madarakani akiwa na miaka 54, sasa hapo ndipo sarakasi za kucheza na katiba huwa zinaanza kwa sababu inakuwa bado mapema mno kwake na kwa wapambe wake.

Marais katika nchi nyingi za Africa wanatakiwa waingie madarakani angalau na umri kuanzia miaka 65 ili akitawala miaka 10 inakuwa imefika 75 na anakuwa amechoka kuendelea kutawala na kufanya mapambano ya kisiasa, anamwachia mwingine. Vinginevyo kuwapa madaraka vijana kuna hatari ya kutawailia na mtu mmoja hata miaka 20 au 30 kama ilivyo katika nchi nyingi za Africa.

Zaidi naamini wazee wana uzoefu na busara zaidi za kuongoza katika nafasi kubwa kuliko vijana, pia hata inakuwa rahisi kuwafahamu kutokana na majukumu yao mbalimbali waliyokwisha kupitia.


Tatizo la wazee hawana busara zaidi ya udikteta. Raisi wa Senegal alitaka kuongea muda yupo toka 1980. Museveni anataka kumwachia mtoto wake! Sasa ndiyo maana vijana wamechoka. Vijana amsheni kwenye katiba
 
Sikuungi mkono kwa sababu:

1. Ukiwa na katiba mbovu haijalishi ni mzee au kijana atataka kuichezea tu. Kwa logic yako, wazee ndio hawachezei katiba ili kubaki madarakani? Rudia kufatilia historia ya Afrika ujifunze upya.

2. Wazee wengi hawana jipya. Kwa Ulimwengu wa sasa unahitaji akili za ujana kuthubutu na kusonga mbele.
 
Historia inatabia ya akujirudia ndio maana Combination ya Kiswahili, historia na Isamic knowledge vimewekwa.

Mifano ni mingi lakini kwa uchache ni hivi Madikiteta woote
1. Rwanda
2. Zimbabwe
3. Uganda
4.DRC
Bora aanze akiwa mzee akikataa kuondoka uzee unamwondoa.
Tatizo la wazee moja tu wakishika utawala hujiona kama machifu wanaotakiwa kutawala milele wakipewa nafasi yeyote ya utawala iwe serikalini, mahakamani au bungeni au kampuni zao binafsi za biashara wamefungua au uongozi wa misikiti au kanisa hawaamini kupisha damu mpya au kizazi kipya wanaamini wao ndio wanajua kila kitu na wanatakiwa kuendelea kutawala milele wawe CCM au upinzani akina Mbowe ,Lisu nk
 
Una hoja ya msingi, lakini tatizo kubwa ni kuwa na katiba zinazowalinda Marais. Bila kuwa na katiba zinazozipa taasisi nguvu na kumpa mtu nguvu, hata akiingia madarakani na miaka 70, Bado anaweza kufanya uhuni. Mfano Mugabe, Museveni, Paul Biya nk. Hawa wote ni wazee lakini uhuni wao uko wazi peupe.
Tatizo ni kwamba Kiongozi anavyozidi kukaa madarakani muda mrefu ndio inakuwa vigumu kuondoka, ni kama vicious circle.
Kiongozi anaingia katika Urais akiwa mdogo sana ndani ya miaka 10 au 15 anakuwa amekwapua mali nyingi sana na wale waliomzunguka, anakuwa na maadui wengi sana kutokana na mauaji, kupoteza watu au kuharibu biashara zao n.k, akiangalia haoni tena usalama wake,familia yake na wa wale wanaomzunguka, hapo lakini tayari anakuwa ameshika mifumo yote ya nchi kisawasawa anaamua tu kubadilisha katiba na kuendelea kusalia madarakani...
 
Tatizo ni kwamba Kiongozi anavyozidi kukaa madarakani muda mrefu ndio inakuwa vigumu kuondoka, ni kama vicious circle.
Kiongozi anaingia katika Urais akiwa mdogo sana ndani ya miaka 10 au 15 anakuwa amekwapua mali nyingi sana na wale waliomzunguka, anakuwa na maadui wengi sana kutokana na mauaji, kupoteza watu au kuharibu biashara zao n.k, akiangalia haoni tena usalama wake,familia yake na wa wale wanaomzunguka, hapo lakini tayari anakuwa ameshika mifumo yote ya nchi kisawasawa anaamua tu kubadilisha katiba na kuendelea kusalia madarakani...
unalazimisha tatizo lionekane kuwa ni umri
Kila Nchi inahitaji Katiba inayounda taasisi imara
 
Vijana wengi ni majangili na wajinga wajinga
Wazee wengi wakishika vyeo wagumu kutoka wana vichwa vigumu mno huwa na u chifu mentality kuwa wao tu ndio wanajua vijana hamna kitu ndio maana hata kampuni kubwa za biashara za kiswahili hufa kizee kinang'ang'ania tu kuwa ohhh mimi najua vijana hamuniambii kitu tofauti na wahindi na wapemba mfano Tanzania Mzee Dewji uzee ulipoingia akampisha mwanawe Mo Dewji ashike uongozi wa kampuni
Pia Bakheresa alivyoona kazeeka kapisha wanawe ndio wanaoendesha kampuni zote za Azam Group

Sisi waswahili vizee vyetu viwe bungeni,serikalini ,mahakamani au taasisi za kidini au kampuni binafsi au vyama vya siasa vinakomaa tu kubaki kwenye uongozi vinajiona kama vichifu kuwa ni vyenyewe tu ndio vinajua na ndivyo vinastahili kuwa kwenye nafasi hadi vifie kwenye hizo nafasi

Hili ndilo tatizo kubwa la kuweka vikomgwe kwenye utawala iwe Afrika au Marekani

Vikongwe vizee kama Biden na Trump unakuta vipo tu vinataka kuhombea uraisi Marekani haviamini vijana vizee choka mbaya Trump na Joe Biden na vikongwe vigombea Afrika viafrika vyenzetu vikiongozwa na kile Kibabu choka mbaya kizee kiraisi cha Nigeria Tinubu
 
Back
Top Bottom