Wanaodhaniwa TLP wamzomea Mbunge wa Vunjo!

Mpaka Kieleweke

JF-Expert Member
Feb 27, 2007
4,132
1,571
Hivi hawa wapambanaji mbona majimboni mwao wanakumbana na aibu?
Ni kuwa wananchi hawawaelewi ama?
Je? wanaonekana kuwa wasanii?
Je?wamesahau kuhudumia wananchi wao wakijificha kwenye kichaka cha kupambana na mafisadi?



Mbunge Aloyce Kimaro azomewa mkutanoni jimboni kwake
broken-heart.jpg
Daniel Mjema na Rehema Matowo,Moshi
Â
MBUNGE wa Vunjo, Aloyce Kimaro jana alikuwa na wakati mgumu baada ya kuzomewa na kundi la wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika mji mdogo wa Himo ulio kwenye jimbo la Vunjo, Moshi Vijijini.

Kimaro ni mmoja wa wabunge ambao wanaonekana kujitoa mhanga katika vita ya ufisadi, lakini jana alijikuta kwenye hali ngumu wakati akihutubia mkutano wa hadhara.

Kundi la watu takribani 100 wanaodhaniwa kuwa ni wafuasi wa chama pinzani cha TLP ambacho ndicho chenye nguvu eneo hilo, lilipiga kelele likisema "hatukutaki" wakati Kimaro alipokuwa akihutubia mkutano huo.
Â
Kadhia hiyo ilianza wakati Mbunge Kimaro alipozungumza na kuelezea kuwa yuko katika hatua za mwisho za kutatua kero ya muda mrefu ya maji katika eneo hilo lenye uhaba mkubwa wa huduma hiyo.

Baada ya kugusia tu suala hilo, Kimaro alishtukia sauti zikitoka kwenye kundi hilo zikidai kwa kelele kuwa mbunge huyo ni mwongo na kwamba hawamtaki, lakini Kimaro akaendelea kusisitiza kuwa kero ya maji itakuwa historia muda mfupi ujao.

Kelele za wananchi hao zilizidi baada ya viongozi wanne waliojitoa TLP kusimamishwa jukwaani kuwahutubia, wakielezewa kuwa wameamua kujiunga na CCM.

Wananchi walidai kuwa viongozi hao ni wasaliti na kuwatuhumu kupokea Sh500,000 kila mmoja ili waisaliti TLP. Lakini walipopata nafasi ya kuzungumza jukwaani, wenyeviti hao walikanusha tuhuma hizo.
Â
Hali hiyo ilimlazimisha katibu mwenezi wa CCM wilayani Moshi Vijijini,Jamal Hussein kuchukua kipaza sauti na kuwakemea wananchi hao waliokuwa wakizomea, akidai kuwa anawafahamu kwa majina.

Hussein alisema kwa kuwa CCM ni chama cha watu makini na wastaarabu hawana sababu ya kulipiza kisasi kuvuruga mkutano wowote wa kambi ya upinzani kama lilivyofanya kundi hilo.
Â
Tishio hilo lilisaidia kupunguza kelele za sauti hizo na mkutano huo ukaendelea kama kawaida kwa Kimaro kuwaelezea wananchi kampeni yake mpya ya ‘Safisha’ yenye lengo la kuondoa viongozi wabovu.

Naye mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango Malecela alizungumza kwenye mkutano huo na kuwataka viongozi wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) kuwaunga mkono wanawake wanaojitokeza kuchuana na wanaume katika chaguzi, akisema utafiti unaonyesha wanawake ni waadilifu zaidi kuliko wanaume.

Kilango aliwahamasisha wanawake nchini kugombea nafasi mbalimbali za uongozi nchini ikiwamo urais mwaka 2015.

Alisema wanawake wanatakiwa kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi za uongozi katika jamii kwa kuwa waliachwa nyuma muda mrefu na kudharauliwa na sasa ni wakati wao.

"Wanawake sasa ni wakati wetu; tuliachwa nyuma na kudharaulika muda mwingi, sasa ni wakati wetu," alisema Kilango.

Hata hivyo, alipotakiwa baadaye kueleza endapo atakuwa mmoja wa wanawake watakaochukua fomu za kuwania urais mwaka 2015, Kilango alisema: "Aaaaa! ni mapema mno kuzungumzia hili. Mimi nilikuwa nawahamasisha tu... suala la nani atasimama ni juu yao,".

"Isitoshe kusema sasa kwamba kwamba nina mpango wa kugombea urais mwaka 2015 sio sahihi kwa kuwa wakati huo nitakuwa mzee. Hili nawaachia wanawake watakaokuwa vijana wakati huo."

Kilango pia alihutubia mkutano wa hadhara juzi kwenye jimbo la Moshi Mjini ambako alitangaza kupiga kambi hadi mwaka 2010 ili kuhakikisha kuwa CCM inanyakua jimbo hilo, uamuzi ambao unamuingiza kwenye vita kali na mbunge wa sasa, Philemon Ndesamburo.

Katika kuonyesha kuwa Ndesamburo hana nguvu kwenye jimbo hilo, Kilango aliwaambia wanachama na viongozi wa CCM kuwa mbunge huyo kutoka Chadema ameshinda mara mbili mfululizo kutokana na matatizo ya WanaCCM wenyewe na kuwataka wajisafishe.

Lakini jana Ndesamburo alijibu mapigo ya mbunge huyo na kueleza kuwa hatishwi na kitendo chake cha kupiga kambi jimboni humo akisema mpango huo ni sawa na kutikisa kibiriti kilichojaa.

Ndesamburo aliiambia Mwananchi jana kuwa hatishiki na mkakati huo wa Kilango na akakanusha madai ya mke huyo wa makamu mwenyekiti wa zamani wa CCM, John Malecela, akisema hajawahi kumwambia kuwa wengi wanaompigia kura ni WanaCCM.
Â
“Mimi sitishiki... yeye afanye kampeni anavyotaka,” alisema Ndesamburo ambaye anamalizia kipindi cha pili cha ubunge wake tangu alipoingia mwaka 2000 akiwa amelichukua kutoka kwa mbunge wa NCCR Mageuzi, Joseph Mtui ambaye alikuwa mbunge kuanzia mwaka 1995.

Ndesamburo, ambaye liibuka na ushindi wa kura 32,035 katika uchaguzi wa mwaka 2005 akimuacha mbali mgombea wa CCM, Elizabeth Minde (23,773), aliongeza kusema: “Sijawahi kumwambia hata kidogo kuwa wanaonifanya nishinde ni wafuasi wa CCM… WanaCCM hawazidi 5,000, mimi nilipigiwa kura na wananchi 30,000.”
Â
Mbunge huyo wa Moshi Mjini alimwonya Kilango kuwa asijaribu kutingisha kibiriti kilichojaa na kusisitiza kuwa kwa mujibu wa takwimu, wanaompigia kura si CCM pekee, bali wengi ni wale wasio na chama.
Â
“Hapa Moshi Mjini Chadema tuko kama 2,000. Hivi hawajiulizi hizo kura za ziada zilitoka wapi kama sio wananchi ambao hawayumbishwi na propaganda chafu,” alihoji Ndesamburo.
Â
Ndesamburo, ambaye pia ni mwenyekiti wa mkoa wa Chadema, alimtaka Kilango kuimarisha kwanza jimbo jirani la Same Magharibi ambako alikuelezea kuwa si shwari. Jimbo hilo linaloshikiliwa na Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Dk David Mathayo na Ndesamburo alidai kuwa linapwaya hivyo Kilango hana budi kuweka kambi huko ili kulinusuru lisichukuliwe na wapinzani.

Alipoulizwa kuhusu madai hayo ya Ndesamburo, Dk.Mathayo alisema kauli hiyo ni ya kisiasa na kwamba kati ya majimbo yote ya mkoa wa Kilimanjaro, jimbo lake ndilo salama kwa asilimia 100.

“Mambo niliyofanya Jimboni hayajawahi kufanywa na mbunge yoyote tangu uhuru na wewe kama mwandishi unaweza kwenda mwenyewe ukafanya utafiti,” alitamba Dk. Mathayo.  Dk. Mathayo alisema katika kipindi kifupi ametoa mifuko ya saruji kwa ajili ya kujenga vyumba vinne vya madarasa katika kila kata, kutoa darubini nane kwa zahanati nane na kujenga soko la kimataifa.
 
Tusisahau kwamba hivi sasa kuna vita vya 'wenyewe kwa wenyewe' ndani ya CCM kuliko hata vita kati ya CCM na vyama vya Upinzani. Kwa hiyo kuzomewa kwa Wabunge kama Kimaro ni dhahiri kunatokana na vita vilivyoibuka ndani ya CCM kutaka kuwavunja nguvu 'wapiganaji'. Mafisadi wamekwishaelewa kwamba wananchi wanaweza kudanganywa vipi ili wafanye wanachotaka mafisadi hao na wameanza kuutumia kikamilifu udhaifu, unyonge na umaskini wa wananchi kuwaangusha wale wanaoonekana ni kikwazo kwao.
 
Kosa kubwa alilolifanya huyu ndugu ni lile la kumfedhehesha Mheshimiwa Rais wa awamu ya Tatu wa Nchi yetu.

Hadi hapo atakapomuomba radhi hadharani atasafishika.
 
Tusisahau kwamba hivi sasa kuna vita vya 'wenyewe kwa wenyewe' ndani ya CCM kuliko hata vita kati ya CCM na vyama vya Upinzani. Kwa hiyo kuzomewa kwa Wabunge kama Kimaro ni dhahiri kunatokana na vita vilivyoibuka ndani ya CCM kutaka kuwavunja nguvu 'wapiganaji'. Mafisadi wamekwishaelewa kwamba wananchi wanaweza kudanganywa vipi ili wafanye wanachotaka mafisadi hao na wameanza kuutumia kikamilifu udhaifu, unyonge na umaskini wa wananchi kuwaangusha wale wanaoonekana ni kikwazo kwao.

Hata kama kuna mkono wa mtu ila kwa mtu kama mbunge kunyooshewa vidole na wananchi wa Jimbo lako tena hadharani ni hali mbaya.
Mbona Mkuchika naye alizomewa kwani na yeye ni mafisadi walituma wananchi?

Huyu jamaa ni mzembe tuu , na ni haki yake kuzomewa , yeye jana kawanunua wenyeviti 4 wa vijiji wa TLP na eti wamerudisha kadi zao na kujiunga na CCM na yeye bila aibu anajisifia kuwa hiyo ni operesheni safisha wapinzani , sasa yeye na mafisadi wana tofauti gani?
 
Hata kama kuna mkono wa mtu ila kwa mtu kama mbunge kunyooshewa vidole na wananchi wa Jimbo lako tena hadharani ni hali mbaya.
Mbona Mkuchika naye alizomewa kwani na yeye ni mafisadi walituma wananchi?

Huyu jamaa ni mzembe tuu , na ni haki yake kuzomewa , yeye jana kawanunua wenyeviti 4 wa vijiji wa TLP na eti wamerudisha kadi zao na kujiunga na CCM na yeye bila aibu anajisifia kuwa hiyo ni operesheni safisha wapinzani , sasa yeye na mafisadi wana tofauti gani?

- Mkuu heshima mbele, mngekuwa mnajaribu kuwa balanced na analysis zenu kuhusu uchaguzi na hayo majimbo, huwa mnaamsha hisia za wananchi hapa kwamba Chadema itashinda, halafu matokeo yakija inakuwa sivyo halafu inakuwa very dis-appointing na kuishia kulia kuibiwa kura, kumbe hamkuwa fair kwenye hizi political analysis mwanzoni.

- Jaribuni kuripoti fairly, ili unapokuja ukweli kusiwe na kukata tamaa maana huwa inasikitisha sana mnapotutabiria tofauti na yanayokuja kutokea na tena ni all the times, kumbuka Busanda na Biharamulo.

- Kuweni fair huu sio mpira wa Yanga na Simba, tupeni ukweli kama ulivyo bila kuufinyanga!

Respect.


FMEs!
 
Niliyoweka hapo juu ni matokeo ya 2005 , na sio analysis zangu.
Tembelea tovuti ya tume utayakuta hayo matokeo.
 
Tatizo watu wamekomalia kula siku ufisadi, ambapo hamna hatua yoyote inayochukulika na kusahao mambo muhim majimboni mwao kama maji na afya.
 
Tatizo watu wamekomalia kula siku ufisadi, ambapo hamna hatua yoyote inayochukulika na kusahao mambo muhim majimboni mwao kama maji na afya.
Na hiki ndio kinammaliza Kimaro, kwani yeye akienda Jimboni kwake taarifa ni kuwa anaenda kufanya mikutano nyumbani kwa watu haswa marafiki zake kama Zadock, Harry Kitilya et al.
Yeye huwa hana PR hata waliomsaidia kuupata ubunge amegombana nao wote kuanzia kwa Shayo wa kingsize, mmoja yupo Arusha n.k.
 
Huyu mbunge aliuliza swali tarehe 30/10/2009 kuhusiana na mashamba ya kawaha , eti yeye alitaka mashamba hayo wapewe matajiri kwa ajili ya kuyaendeleza , huku akijua kuwa wanachi wake ni masikini na hawana ardhi, mpakia pale Ndesamburo alipoingilia na kuhiji iweje wapewe matajiri?
 
Wawekezaji Mkoani Kilimanjaro
MHE. ALOYCE BENT KIMARO aliuliza:-

Kwa kuwa, katika Mkoa wa Kilimanjaro kuna mashamba makubwa ya kahama yanayosimamiwa na Vyama vya Msingi vya Ushirika lakini mengi yameshakodishwa kwa wawekezaji:-

(a) Je, Serikali inaweza kuyataja mashamba hayo na yameingiza faida ama hasara kiasi gani kwa Taifa?

(b) Kama kuna mashamba yenye utata na hayaleti faida kwa nchi;Serikali haioni kuwa ni vema kuyagawa kwa Watanzania wenye uwezo hasa wakati huu Serikali inapohimiza kilimo?


NAIBU WAZIRI WA KILIMO CHAKULA NA USHIRIKA (MHE. MATHAYO D. MATHAYO) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Aloyce Bent Kimaro, Mbunge wa Vunjo, lenye sehemu (a) na (b) kama ifutavyo:-

(a) Mashamba yasiyosimamiwa na Vyama vya Ushirika vya Msingi Mkoani Kilimanjaro ni 41. Kati ya hayo, mashamba 27 yanazalisha kwa tija na faida. Mashamba 14 hayazalishi kwa faida kutokana na mogogoro kati ya wamiliki na waliokodisha, na uzalishaji mdogo wa wakodishaji. Katika mashamba ynayozalisha kwa faida sehemu ya mapato ya ukodishaji wa mashamba hutumika kuimarisha huduma za jamii ikiwemo shule, zahanati, barabara, na kusaidia malipo ya karo za shule kwa watoto wasiojiweza. Aidha, wananchi wanapata ajira katika mashamba hayo. Mazao yanayozalishwa katika mashamba hayo ni, mboga mboga na nafaka. Mazao hayo yanapouzwa huwapatia wakulima na Taifa mapato zikiwemo fedha za kigeni kwa mazao yanayouzwa nje ya nchi kama kahawa, mauwa na mboga mboga. (Makofi)

(b) Mheshimiwa Spika, kutokana na baadhi ya mashamba kuzalisha chini ya uwezo, uongozi wa Mkoa wa Kilimanjaro uliteua kamati maalum ambayo ilifanya tathmini ya mashamba yote 41 na kubaini viwango vya maendeleo ya uwekezaji na kutoa taarifa kwa uongozi wa Mkoa wa Kilimanjaro. Taarifa hiyo iliwasilishwa kwenye uongozi wa mkoa na kamati ya ushauri ya Mkoa (RCC). RCC kwenye kikao chake cha tarehe 11 Mei 2009, imeushauri uongozi ufanye upya mapitio ya mikataba ya mashamba hayo ili kubaini mapungufu yaliopo na kuchukua hatua zitakazowezesha mashamba hayo yazalishe kwa tija na faida.


Mheshiiwa Spika, kutokana na maelezo hayo ni vyema kabla Serikali haijafikia hatua ya kuyagawa mashamba hayo kwa Watanzania wenye uwezo kama alivyopendekeza Mheshimiwa Mbunge, ni vema tukasubiri matokeo ya juhudi zilizoanza kuchukuliwa na uongozi wa mkoa wa Kilimanjaro.


MHE. ALOYCE B.KIMARO: Mheshiiwa Spika,pamoja na majibu ya Mheshimiwa ya Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshiiwa Spika,lengo la kuuliza swali hili ni kutaka kujua Serikali ina mpango gani kambambe wa kufufua zao la kahawa katika Mkoa wa Kilimanjaro kwa kutumia mashamba haya ili wakulima wadogowadogo waweze kuiga. Sasa maswali mawili. Katika majibu ya serikali Naibu Waziri amesema kati ya mashamba 41, 27 yanafanya kazi na faida inayopatikana ina hudumia shule ,zahanati, barabara na kusaidia watoto wasiojiweza. Naomba Naibu Waziri atutajie kwa majina shule ngapi, zahanati ngapi, barabara ngapi na watoto wangapi wamefaidika.

Mheshiiwa Spika, swali la pili. Mashamba 14 hayazalishi kwa faida ama hayazalishi kabisa. Lengo la serikali ya awamu ya nne ni kufufua kilimo cha kahawa kutoka uzalishaji wa tani 40 mpaka tani 120 kwa mwaka. Sasa Waziri kusema kwamba tusubiri matokeo ya mkoa ni kama kukwepa wajibu wa kujibu swali langu. Naomba sasa Waziri anieleze, wizara inashiriki vipi katika kutatua mgogoro huu na wizara inategemea itaisha lini ili mashamba haya yaanze uzalishaji kwa faida?

SPIKA: Swali la kwanza la Mheshimiwa Kimaro ni hakika linadai takwimu. Kusema watoto wangapi wamefaidika sidhani kama Wizara ya Kilimo itakuwa nazo hizo takwimu. Labda itakapo zipata kutoka Elimu waweze kuwasilisha tu kwa maandishi. Kwa hiyo, nitmwomba Naibu Waziri ajibu kwa kifupi hili la pili.
NAIBU WAZIRI WA KILIMO CHAKULA NA USHIRIKA (MHE. MATHAYO D. MATHAYO): Mheshimiwa Spika, serikali hii ni moja kama nilivyoeleza sasa hivi uongozi wa Mkoa wa Kilimanjaro unashughulikia suala hili, basi ngoja watoe taarifa na sisi tutaona kama wizara tutaingia vipi. Lakini shughuli hii inashughulikiwa na Mkoa wa kilimajaro na ni suala ambalo wanalichukua serious kabisa. Kwa hiyo, nadhani tusubiri chombo hicho kwanza kimalize kazi yake halafu ndipo tujue kwamba tunachukua hatua gani.

MHE. PHILEMON NDESAMBURO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali fupi la nyongeza. Katika majibu ya serikali amesema wanangojea Kamati ya mkoa ifanye pitio ili waweze kujua watagawa lini hayo mashamba kwa watu wenye uwezo na mwenye kuuliza swali anataka mashamba haya wapewe watu wenye uwezo. Kilio cha wakazi wa Kilimanjaro ni ardhi hakuna na wangependa ardhi hii igawiwe kwa wakulima wadogo wadogo ili waweze nao kufaidika.

Je, serikali inataka kuzidi kuwazidishia wenye kipato na kuwasahau wale wadogo wasiokuwa na kipato?

WAZIRI WA KILIMO, CHAKULA NA USHIRIKA: Mheshiiwa Spika, aliyependekeza kutoa mashamba haya kwa wenye uwezo ni Kimaro sio serikali. Sisi tulichosema katika jibu letu kwamba tunasubiri Mkoa umalize kufanya tathmini halafu tushirikiane na mkoa tuone namna gani tunaweza kumaliza tatizo hilo. Mashamba haya yalipewa watu wadogo kupitia Ushirika. Hiyo ndiyo msingi na msingi huo unaweza ukaendelea kuendelezwa bila kujali Kimaro anatakaje au anataka vipi. (Makofi)

huyu anawakilisha matajiri bungeni hivyo masikini ni lazima wamzomee kwani hawawakilishi.
 
WAZIRI WA KILIMO, CHAKULA NA USHIRIKA: Mheshiiwa Spika, aliyependekeza kutoa mashamba haya kwa wenye uwezo ni Kimaro sio serikali. Sisi tulichosema katika jibu letu kwamba tunasubiri Mkoa umalize kufanya tathmini halafu tushirikiane na mkoa tuone namna gani tunaweza kumaliza tatizo hilo. Mashamba haya yalipewa watu wadogo kupitia Ushirika. Hiyo ndiyo msingi na msingi huo unaweza ukaendelea kuendelezwa bila kujali Kimaro anatakaje au anataka vipi. (Makofi)

Huyu anawakilisha matajiri bungeni hivyo masikini ni lazima wamzomee kwani hawawakilishi.

Huyu naye ni mbunge inaonyesha dhahiri yuko bungeni kwaajili ya watu wenye uwezo tu,ndio maana yuko tayari kutoa 500,000/= kununua wenyeviti wa TLP !!!!!!!!!!!!!!!.
 
WAZIRI WA KILIMO, CHAKULA NA USHIRIKA: Mheshiiwa Spika, aliyependekeza kutoa mashamba haya kwa wenye uwezo ni Kimaro sio serikali. Sisi tulichosema katika jibu letu kwamba tunasubiri Mkoa umalize kufanya tathmini halafu tushirikiane na mkoa tuone namna gani tunaweza kumaliza tatizo hilo. Mashamba haya yalipewa watu wadogo kupitia Ushirika. Hiyo ndiyo msingi na msingi huo unaweza ukaendelea kuendelezwa bila kujali Kimaro anatakaje au anataka vipi. (Makofi)

Huyu anawakilisha matajiri bungeni hivyo masikini ni lazima wamzomee kwani hawawakilishi.

Huyu naye ni mbunge inaonyesha dhahiri yuko bungeni kwaajili ya watu wenye uwezo tu,ndio maana yuko tayari kutoa 500,000/= kununua wenyeviti wa TLP !!!!!!!!!!!!!!!.

NAYE anajiita mpambanaji dhidi ya Ufisadi
 
NAYE anajiita mpambanaji dhidi ya Ufisadi

Mpaka Kieleweke,

Angalia sana, ukimshambulia mpiganaji wa ufisadi utaambiwa ni fisadi na umepewa bilioni moja na RA na Lowassa.

Watanzania ni wadanganyika na tutaendelea kudanganywa mpaka tutakapoelewa maana ya mapambano kwa dhati na sio ngonjera za kwenye majukwaa.
 
Niliyoweka hapo juu ni matokeo ya 2005 , na sio analysis zangu.
Tembelea tovuti ya tume utayakuta hayo matokeo.
Inawezekana wengine hawamjui, sasa ni huyu hapa.
 

Attachments

  • CA8L6FC1.jpg
    CA8L6FC1.jpg
    3.1 KB · Views: 50
  • CAGXEVKN.jpg
    CAGXEVKN.jpg
    2.5 KB · Views: 49
mie nilikuwa simjui bora mmeweka picha yake zeroooo acha tu raia wamzomee kama hana la maana alilolifanya
 
Huyu ndiye Aloyce Bent Kimaro.

GENERALSalutationHonourableMember picture
1374.jpg
First Name: AloyceMiddle Name: BentLast Name:Kimaro

Member Type:Constituency MemberConstituent: VunjoPolitical Party: CHAMA CHA MAPINDUZI

Office Location: P.O.Box 105, Marangu-MoshiOffice Phone: +255 754 544544Ext.: Office Fax: Office E-mail: akimaro@parliament.go.tzMember Status: Current MemberStart Date: 28 December 2005 End Date:27 December 2010 Date of Birth 24 June 1953

EDUCATIONS
School Name/Location Course/Degree/Award Start DateEnd DateLevelLyasongoro Primary Education19621969
PRIMARYOldMoshi Secondary SchoolO-Level Education

19701973SECONDARYMkwawa High SchoolA-Level Education19731975HIGH SCHOOLKleruu College of National EducationDiploma in Education

1977=-1978DIPLOMAInstitute of Development Management- MzumbeAdvanced Diploma in Business Education19801983ADV DIPLOMACERTIFICATIONS Certification Name or TypeCertification No. </SPAN>IssuedExpires</SPAN>No items on list

EMPLOYMENT HISTORY Company Name Position From
DateTo DateMinistry of TradeBusiness Officer 1984-1988
Ministry of Education - Azania Secondary SchoolTeacher
1979-1980Ministry of Education- Minaki Secondary SchoolTeacher 19781979
 
Kimaro akalia kuti kavu Vunjo


na Edward Kinabo


amka2.gif

IKIWA imebakia miezi 11 kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu wa rais, wabunge na madiwani mwakani, joto la kisiasa linaonekana kupanda kwa kasi katika Jimbo la Vunjo, mkoani Kilimanjaro, huku Mbunge wake, Aloyce Kimaro (CCM), akionekana kukabiliwa na upinzani mkali.
Uchunguzi wa hali ya kisiasa uliofanywa na Tanzania Daima kwa zaidi ya miezi mitatu sasa, umebaini kuwapo kwa ushindani mkubwa wa kisiasa kati ya Kimaro na wagombea watarajiwa; Augustine Lyatonga Mrema wa Chama cha Tanzania Labour (TLP) na John Mrema wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ambao wote wamekuwa ama wakijichimbia au kufanya ziara za mara kwa mara jimboni humo, wakilenga kujitengenezea mazingira ya kufanya vizuri mwakani.
Kimaro anayetajwa kuwa mmoja wa wabunge wanaopambana na ufisadi, hivi karibuni amekuwa akitoa ahadi kemkemu kwa wakazi wa jimbo hilo, akijaribu kujijengea mvuto mpya wa kisiasa, hasa baada ya harakati zake za kukemea ufisadi wa viongozi wa kitaifa kuonekana kutowagusa moja kwa moja wananchi wa jimbo hilo.
Wakati wa kampeni za uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji uliofanyika Oktoba 25, mwaka huu, Kimaro aliwaahidi wakazi wa mji mdogo wa Himo ulio kitovu cha siasa za jimbo hilo, kwamba angewapatia msaada wa gari la kubebea wagonjwa mahututi (ambulance), ahadi aliyoitimiza baada ya uchaguzi huo.
Mkakati huo sasa unaonekana kumtokea puani mbunge huyo, baada ya juzi kuzomewa na wananchi wa mji huo wa Himo, mbele ya mbunge mwenzake machachari, Anne Kilango Malecela, alipoahidi kwamba yuko katika hatua za mwisho za kutatua kero ya maji inayolisumbua eneo hilo kwa muda mrefu.
“Hatukutaki”, walisikika vijana takriban 100 wanaodhaniwa kuwa wafuasi wa TLP ama CHADEMA, baada ya Kimaro kutoa ahadi yake hiyo.
Aidha, matokeo ya uchaguzi huo wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji pia yanathibitisha upinzani mkali uliopo baina ya wagombea hao, ambao wote walijichimbia jimboni humo kabla na wakati wa kampeni za uchaguzi huo, wakiratibu mikakati ya ushindi na kunadi wagombea wa vyama vyao waliowania nafasi mbalimbali katika vijiji na vitongoji.
Matokeo ya uchaguzi huo yanaonyesha kuwa vyama vya TLP na CHADEMA, vikiongozwa na wagombea wake hao watarajiwa, vilitoa upinzani mkali katika uchaguzi huo hata kufanikiwa kupata ushindi wa vijiji 38 dhidi ya vijiji 37 vilivyochukuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Katika matokeo hayo, TLP ilijinyakulia vijiji 20 na CHADEMA vijiji 18, hali inayoashiria kuwapo kwa nguvu inayokaribiana baina ya vyama hivyo vya upinzani dhidi ya CCM.
Watu wanaoaminika kumuunga mkono Kimaro, wanadaiwa kuanza kutumia ushawishi wa fedha kuwanunua baadhi ya wenyeviti wa vijiji kutoka katika vyama hivyo vya upinzani, hususan wale wa TLP.
Akizungumzia matokeo ya uchaguzi huo, siku moja baada ya kutangazwa, Augustine Lyatonga Mrema ambaye ni mwanasiasa mkongwe na Mwenyekiti wa taifa wa TLP, alikaririwa akisema: “Nimepata nguvu, nimeonyesha umma kuwa bado watu wananihitaji na ninatakiwa kutumikia wananchi, sasa ninaanza mapambano.”
Alisema katika Kata ya Kilema Kaskazini ambako aliyekuwa diwani wa kata hiyo kwa tiketi ya TLP alinunuliwa na CCM na kukihama chama hicho, TLP imenyakua viti vitatu na CHADEMA kimoja na kufanya vijiji vyote vya kata hiyo kuwa kwa wapinzani.
Hata hivyo, pamoja na TLP kujivunia vijiji 20 ilivyopata, matokeo yanayoshitusha ni yale ya CHADEMA kupata vijiji 18, kwani ilifanya maandalizi ya muda mfupi, ikilinganishwa na maandalizi ya Mrema wa TLP aliyekuwa amejichimbia jimboni kwa zaidi ya miezi minne kabla ya uchaguzi huo.
Mafanikio hayo ya CHADEMA yaliyopatikana ndani ya kipindi kifupi, yalichangiwa kwa kiasi kikubwa na kampeni zilizoendeshwa na mgombea wake mtarajiwa wa ubunge, John Mrema, ambaye pia ni Mkurugenzi wa masuala ya Bunge na Halmashauri wa chama hicho. Uwezo mkubwa wa kujenga hoja, kubuni, kuratibu na kusimamia mikakati ya ushindi, ulioonyeshwa na Mrema wa CHADEMA, pamoja na uhamasishaji mzuri wa wananchi kujiandikisha kupiga kura, uliofanywa na kada huyo kijana katika kipindi chote cha kampeni hizo, ndivyo hasa vinavyoonekana kuvutia wananchi wa vijiji 18 kukipa ushindi wa ghafla chama hicho, huku kukiwa na taarifa za kunyimwa ushindi katika vijiji vingine zaidi ya tisa, kwa madai ya kuwapo kwa mbinu haramu zilizoipa CCM ushindi katika vijiji hivyo. Pamoja na kutoa upinzani mkali dhidi ya Kimaro na kuishinda CCM kwa ushindi wa jumla katika uchaguzi huo wa serikali za vijiji na vitongoji, bado wagombea hao wa upinzani, Mrema wa TLP na Mrema wa CHADEMA, kila mmoja anakabiliwa na changamoto ya kuvutia wananchi wengi zaidi upande wake, ili kuondoa uwezekano wa kila mmoja kushindwa katika kinyang’anyiro cha ubunge mwakani, kwa kugawana kura na kumuacha mgombea wa CCM akishinda.


h.sep3.gif


juu
blank.gif
 
Date::11/25/2009Mbunge Kimaro atoboa siri kuzomewa jimboni kwake
broken-heart.jpg
Na Waandishi Wetu

MBUNGE wa Vunjo, Aloyce Kimaro ametoboa siri ya kuzomewa kwenye mkutano wa hadhara juzi na kuweka wazi kwamba ukiritimba wa CCM katika michakato ya uchaguzi ni moja ya sababu ya kuzomewa.

Akizungumza katika ofisi za gazeti hili jana Kimaro alisema ukiritimba, ubinafsi na uchoyo uiliokidhiri ndani ya chama hicho, ni sababu kubwa ya kuzomewa baada ya viongozi wanne waliokuwa CCM kukihama chama na kwenda chama cha Tanzania Labour Part (TLP) na kurudi tena CCM juzi.

â&#8364;&#339;Kimsingi hata mimi sipendi vitendo vilivyofanywa na vinavyofanywa na viongozi wa CCM, katika jimbo langu, hivyo nimeanzisha â&#8364;&#732;Operation safishaâ&#8364;&#8482; ambayo hii itasafisha viongozi wote wanaoendeleza biashara ya ukiritiba nje ya chama na ndani ya chama. Lazima watakubwa na operation hii.

â&#8364;&#339;Kundi lilozomea liliandaliwa na Augustino Mrema lililetwa kwenye mkutano wangu na daladala kutoka eneo la Njia Panda, wao waendelee kuzomea mimi sitishiki na siachi ngozi yangu ngumu nitapambana nao mpaka kieleweke,â&#8364; alisema.

Alisema mbinu zilizotumiwa na Mrema za kuandaa kundi kwa ajili ya kuzomea zinaonyesha kuwa ameishiwa kisiasa, sasa anatapatapa kutafuta pakuangukia.

â&#8364;&#339;Kunatetesi kuwa Mrema analitaka jimbo langu ambalo yeye aliliongoza kwa zaidi ya miaka ishrini bila mafanikio na kulikimbia sasa nakuja kufanya nini, mimi nasubiri kwa sababu hanitishi, hanibabaishi nitamgalagaza,â&#8364; alisema.

Katika hatua nyingine wenyeviti wawili wa vijiji ambao juzi Kimaro alidai waliandika barua za kujiuzulu kutoka chama cha Tanzania Labour (TLP) na kujiunga na CCM, wamekanusha kwamba hawajawahi barua hizo.
Â
Mbunge huyo aliwataja wenyeviti hao kuwa ni Abel Shirima wa kijiji cha Kilema chini, Stephen Tumbo wa kijiji cha Makame chini,Donacian Mahoo wa Kijiji cha Kiou waliokuwepo kwenye mkutano na Michael Kessi wa Kijiji cha Makame Juu ambaye katika hakuwepo mkutano huo.
 Â
Jana Mahoo na Kessi walifika ofisi za Mwananchi mjini Moshi wakisisitiza kuwa hawajawahi kujiuzulu uenyekiti wala kuandika barua na kwamba tayari wamemuandikia Mkurugenzi wa Halmashauri ya Moshi kulalamikia matamshi ya kujiuzulu yaliyotolewa na Mbunge wao.
Â
Hata hivyo akiwa na nakala za barua hizo mkononi, Kimaro jana alisisitiza kuwa wenyeviti hao waliandika barua na kama wameamua kukanusha hawezi kuwazuia kwa kuwa wako huru kufanya hivyo. Â Habari hii imeandaliwa na Daniel Mjema na Rehema Matowo,Moshi, Mussa Mkama na Boniface Meena
 
Back
Top Bottom