Wanandoa mnawezaje kuvumiliana kwenye hii hali?

Wanandoa mnawezaje kuvumiliana kwenye hii hali?

Mkuu kile kiapo cha siku ya ndoa ...kuishi kwa shida na raha.....moja ya misingi yake ni kama hicho unachokizungumzia.....na sio shida na raha za kulala na njaa tu....kuna wakati mwenzio anaweza ugua akashindwa hata kwenda chooni au bafuni....ni wewe ndio wakumsaidia kwa kila kitu....anajisadia na kuoga kitandani.....je utaacha kumsadia kwa kuogopa harufu! ....ukifanya hivyo utakuwa umevunja kiapo cha ndoa....lakini vile vile kwenye ndoa....mke pia ni mama....na mme ni baba... hivyo kila mtu ni mtoto kwa mwenzie na mzazi wa mwenzie...na siku zote mzazi huwa haoni kinyaaa kwa mtoto wake....haya yote yanawezekana Kama tu mlioana kwa mapenzi ya dhati la sivyo sio rahisi kiivyo.
Dah.... Maneno yako yamejawa na busara sana ndani yake. Watoto wa siku hizi wanajifanya mapenzi wanayojua ni ya bata tu. Kuchaguana kwaajiri ya swaga za kupost mtandaoni wakijishebedua kwa kubenua midomo kama nyani anakula ubuyu, kubedua tako moja na kupiga picha za kufanana maflana na nguo za vitenge.

Wanasahau kuwa ndoa ni zaidi ya hayo, hakuna kitu muhimu katika maisha kumtunza na kumpenda mwenzako kwa hali zote.

Nimefeel sana huo mstari uliposema kuwa MCHUKULIE MTOTO WA MWENZAKO KAMA MTOTO WAKO HALAFU WEWE KUWA KAMA MZAZI KWAKE.

Ukitazama kiuhalisia katika mapenzi usipomchokulia mwenzako kama mtoto wako hautakuwa na huruma nae pale anapokosea kwasababu wazazi huwa wanahuruma sana na watoto wao hata wakosee kosa gani watawapokea kwa mikono miwili. Watawachapa, watawasema ila mwisho wa siku watawapokea tena na kuishi nao kwa upendo na ndio maana watoto ni ngumu sana kuwaacha wazazi nyakati za matatizo au hali ngumu na wakati wa raha huwa nao pia.

The same kwenye mahusiano, mtoto wa mwenzako huyo wazazi wamekukabidhi uishi nae, ana tabia au mwenendo mbaya usimuache akateseke au akataabike mbeleni, muonyeshe upendo kwa kumjali zaidi na kumfunda taratibu. Ni kweli samaki mkunje angali mbichi, ila hata akishakaushwa pia unaweza mnyoosha taratibu akanyooka.

Mwenzako anafanya ulevi unamuacha, anakuwa mvivu unamuacha, hajui kutunza pesa na kufanya maendeleo unamuacha hayo sio maisha, hebu jitume katika kuweka mambo sawa na kumsaidia aache upuuzi kwa juhudi na bidii zote unless awe anakubishia na kukuonyesha hataki huo. Msaada wako.

Pia katika kuwa kama mzazi kwa mwenzako, hilo jambo ni kuhimu sana. Mpenzi wako (girlfriend/mchumba/mke) anapokuwa na shida unampa msaada kwa kujali au unampotezea. Je unahakikisha anapata mahitaji yake. Anapoumwa unakuwapo kwaajiri yake kumhudumia kwa upendo na kumfariji na kumdekeza ajiskie yupo na baba yake au mama yake?! Unapomuona amekata tamaa unampa maneno ya lawama au unamkumbatia na kumbembeleza na kumjaza nguvu kama vile wewe ulivyojazwa nguvu kipindi ukiwa mdogo pale ulipokosa tumaini na kujiamini?! Je siku akiwa na furaha na mood yake haipo sawa unampa attention yako yote au unasema wanawake ukiwaendekeza watakupelekesha au unasema mwanaume msumbufu ana visa sana?!

Je, inapotokea mwenzako anataka kukumbatiwa tu na kuambiwa its okay am here for you, huwa unampa hiyo kitu?!

Upendo unanguvu sana ndio maana kwa nguvu ya upendo makahaba hugeuka kuwa mke mwema mara tu atakapokutana na mtu anaemjali na kumpenda na kumtreate kama mzazi.

Upendo unamfanya mwanaume mvivu kujikuta anabadilika nakuwa mchapa kazi kwa bidii ili kutomdisappoint mtu aliyempenda.....

Kupenda, kupendwa na kupendana ni raha sana pale unapokutana na copy yako. Usikate tamaa na matukio ya ujana, endelea kumtafuta zing wako.
 
Nawafundishaga watu wanabisha..mavi pale tuu yakifika mlangoni tayar kwa kunyewa unatakiwa unye mda uleule..wala hayatanuka na ukijamba ushuzi haunuki pia.
Ha ha ha ha ha ha ha ha ha we unaonekana ni mtaalamu wa kukata gogo na ni experienced gogo personnel.

Kimsingi ile kitu huwa inazunguka katika njia yake tokea inatoka katika mfuko wa chakula hadi kufika katika discharge door area. Kitendo cha watu kupata mlo m'moja kwa siku inapelekea chakula kuchuka taratibu sana na digestion process inafanyika kwa muda mrefu sana. So, jinsi inakwenda taratibu, plus kufyonzwa maji, inakauka sana na hatimae inakuwa ngumu na mwili unakuwa unavyonza toxic wastes.

So ikija toka balaa lake ni kubwa sana....... Choo kinakuwa na harufu kali sana isiyovumilika, lakini pia hata aina ya vyakula watu huwa wanakula vinachangia sana harufu kali ya choo, imagine mtu kala maharage, mtindi na mayai ya kuchemsha balaa lake huwa si la nchi hii.

Ila cha msingi especially kwa watoto wa kike nawashauri sana ili kujilinda na hii aibu wawe wanatumia sana mboga za majani kwa wingi sana, sana sana mchicha, spinach,majani ya maboga, majani kunde na figiri. Pia wawe wanakula sana matunda kama maembe, mananasi, machungwa unatafuna hadi lile ganda jeupe, fenesi ukipata sio mbaya, na mapapai yaliyoiva vizuri hii inasaidia sana kulainisha choo na kutoa choo haraka na mapema na waende kwa wakati chooni.

Pia tende ni nzuri sana ukiwa haupati choo kwa wakati na kizuri. Ukila tende hata peke sita kila baada ya nusu saa utaona zinakuzaidia..... Zabibu pia ni nzuri sana.

Maji ya moto pia husaidia kusukuma choo. Ukipata nusu lita ya maji ya moto ukinywa yanasaidia kustimulate mshuko wa choo katika njia ya utumbo na kukusaidia kutoa haraka taka zile zinazoshuka taratibu.

Lakini muhimu zaidi ni kutokukosa chakula kuanzia mara tatu kwa siku inasaidia kupata choo kwa msukumo mzuri.

Haya mswala huwa watu hawafunzwi shule.....

Watoto wa kike wapo radhi kununua wigi la laki mbili ila sio kula chakula cha afya.
 
U js flush 'during' and 'after' the poop...muda unatoka washroom hamna harufu yoyote

Weka na air freshener humo
 
Kwa mfano mume na mke mnalala kwenye chumba cha self, choo humo humo ndani, mkeo au mmeo akienda kukata gogo mnavumilia vipi hiyo harufu mbaya? Mwenzi akitoka chooni?

Au mnalala kitanda kimoja, mmoja wenu ajambe usiku half uko macho, hio harufu mbaya mnaivumiliaje?
ukikuwa utayaweza tu..unakunya,yeye yuko kwenye sink anapiga mswaki.
 
Mbona hayo mambo ya kawaida kabisa,
Tunashindana kujamba kwenye neti sembuse harufu ya toilet, hakuna kitu kizur kwenye mahusino kama kuzoeana na mpenzi wako au mume/mke yaan raha raha tu, hakuna kujibana bana.

Kuna siku Mr alingia toilet kumbe maji yamekatika, akajisaidia akaniambia nichotee maji kwenye ndoo nioge niwah kazini bas mwanamke nikampelekea akaoga kamaliza kuvaa ananiaga ananiambia bby nimeflash mzigo haujaenda wote hembu mwaga maji tena basi tukacheka nikaenda kuflash maisha fresh kabisaaaaa
 
Ushuzi wa bae haunuki.

Kama unapuu nnya inanuka sana hapo ni wewe tu na matatizo ya mlo wako usifikiri binadamu wote tuko sawa...
Na ukishasikia harufu tuu ya mwenzako ujue upendo umeanza kupungua.
 
Sasa asipokujambia wewe akamjambie nani?
Ila aseeh nadhani haya mambo ni wale mboga saba.
Hawa black mamba wetu kina sikujua ukute kala miguu ya kuku ,tembele kapiga na kande.
Aaeeh
Akiachia hiyo itakuwa mass weapon destruction ...
 
Kwa mfano mume na mke mnalala kwenye chumba cha self, choo humo humo ndani, mkeo au mmeo akienda kukata gogo mnavumilia vipi hiyo harufu mbaya? Mwenzi akitoka chooni?

Au mnalala kitanda kimoja, mmoja wenu ajambe usiku half uko macho, hio harufu mbaya mnaivumiliaje?

Weww na matatizo yako usifikiri kila mtu ni hivyo vya kunuka lol
 
Hii inaonesha experience yko ilivyo, sio kila binadam mavi yake yananuka sana, experience yko ni ya patner wako au wewe kwa maji yenu kuwa na harufu sana, ushauri tu, kunywa maji mengi na pia nenda choo mara kwa mara, itakusaidia sana

Umesema kula kitu mtu asiekua na shida ya kupata choo mara nyingi poo hazinuki hivyo anavyosema kabisa
 
Nawafundishaga watu wanabisha..mavi pale tuu yakifika mlangoni tayar kwa kunyewa unatakiwa unye mda uleule..wala hayatanuka na ukijamba ushuzi haunuki pia.

Ukweli kabisa na pia ukiwa huna matatizo ya kupata choo ukiwa mtu wa kula mboga mboga sana na maji
 
Kwa mfano mume na mke mnalala kwenye chumba cha self, choo humo humo ndani, mkeo au mmeo akienda kukata gogo mnavumilia vipi hiyo harufu mbaya? Mwenzi akitoka chooni?

Au mnalala kitanda kimoja, mmoja wenu ajambe usiku half uko macho, hio harufu mbaya mnaivumiliaje?
Labda mazingira ya choo chenu sio masafi/mazuri. Yaan mtu ajambe au anye we usikie
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom