Wananchi wenye hasira waua kibaka Yombo Vituka

Wananchi wenye hasira waua kibaka Yombo Vituka

magode

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2014
Posts
2,204
Reaction score
3,339
Nimepita hapo yombo vituka maarufu kwa chande wananchi wamemuua kibaka usiku huu.
Tahadhari;nawasihi police kuimarisha ulinzi eneo hilo baada ya mazishi ya huyo kijana. Mara nyingi kumekuwa na kasumba anapouwawa kibaka,waliobaki hujikusanya na kwenda kumzika kibaka mwenzao. Police waanze kwa kuzuia Uhuru wa vibaka kuzikana maana wanapotoka huko ndipo uhalibifu wa mali za watu hujitokeza.
 
Nimepita hapo yombo vituka maarufu kwa chande wananchi wamemuua kibaka usiku huu.
Tahadhari;nawasihi police kuimarisha ulinzi eneo hilo baada ya mazishi ya huyo kijana. Mara nyingi kumekuwa na kasumba anapouwawa kibaka,waliobaki hujikusanya na kwenda kumzika kibaka mwenzao. Police waanze kwa kuzuia Uhuru wa vibaka kuzikana maana wanapotoka huko ndipo uhalibifu wa mali za watu hujitokeza.

Usitake suluhu kama imara na Mali ziharibiwe sababu hayo ndio mnayoyataka! yaani jicho kwa jicho kiingereza wanasema tit for tat....an eye for an eye. hiyo mlieua sio paka Ni kibaka, kibaka Ni was kushika na kumkabidhi kwa vyombo vya sheria aadhibiwe. wote walioua Ni was kukamata na kufikishwa mbele ya sheria kwa kosa LA kuchukuwa sheria mkononi ma kuua! serikali inashindwa kutimiza wajibu wake watu wanauana kama hakuna sheria au tuko Afghanistan!
 
Usitake suluhu kama imara na Mali ziharibiwe sababu hayo ndio mnayoyataka! yaani jicho kwa jicho kiingereza wanasema tit for tat....an eye for an eye. hiyo mlieua sio paka Ni kibaka, kibaka Ni was kushika na kumkabidhi kwa vyombo vya sheria aadhibiwe. wote walioua Ni was kukamata na kufikishwa mbele ya sheria kwa kosa LA kuchukuwa sheria mkononi ma kuua! serikali inashindwa kutimiza wajibu wake watu wanauana kama hakuna sheria au tuko Afghanistan!

Jeshi La polisi si waaminifu unapopeleka mtuhumiwa hasa kibaka......ndio maana watu uchukua sheria mkononi
 
teh teh

waziunganishe na kupelekea panya
Ngoja tuone baada ya mazishi ya huyu aliyeuawa hali itakuaje! Nnavyowajua panya road hekaheka zao huwa baada ya mazishi ya mwenzao.
 
Ngoja tuone baada ya mazishi ya huyu aliyeuawa hali itakuaje! Nnavyowajua panya road hekaheka zao huwa baada ya mazishi ya mwenzao.

watamzika leo

leo hatumwi mtu dukani
 
Usitake suluhu kama imara na Mali ziharibiwe sababu hayo ndio mnayoyataka! yaani jicho kwa jicho kiingereza wanasema tit for tat....an eye for an eye. hiyo mlieua sio paka Ni kibaka, kibaka Ni was kushika na kumkabidhi kwa vyombo vya sheria aadhibiwe. wote walioua Ni was kukamata na kufikishwa mbele ya sheria kwa kosa LA kuchukuwa sheria mkononi ma kuua! serikali inashindwa kutimiza wajibu wake watu wanauana kama hakuna sheria au tuko Afghanistan!

Wewe lazima utakuwa kibaka...au una maslahi na vibaka au unajifunza ukibaka....moto wa tairi unakusubiri..
 
Sisapoti vibaka ila si vizuri na ni dhambi kumwuua binadamu mwenzakoo.....

Ee Mungu Mlaze pema peponi anaeitwa ni kibaka alie uawa na wananchi wenye hasira kali.

Kwa yeyote itakayo mgusa aseme Aaaamen....
 
Wewe lazima utakuwa kibaka...au una maslahi na vibaka au unajifunza ukibaka....moto wa tairi unakusubiri..
Afadhali mkuu umenisaidia,kuna watu wanashangaza,ukikabwa na hawa kibaka huwezi kuongea ----- namna hiyo.
 
Safi sana bora wauliwe tunalala saa mbili siku hizi kwa vitisho.
 
Baadae ndungu zangu ntatoa namba za tigo pesa ili tuwezeshane kumzika ndugu yetu...asanteni...!!
 
Hapa hata mimi huwa sielewi hizi hasira kali huwa zinapotelea wapi kwa panya road!?

Kweli ndugu yangu.

Uwezo huo wanao,nia wanayo na sababu pia wanayo. Kwanini hasira hizo kali za wananchi hao zisielekezwe kwa "panya road".
 
Intelegensia ya polisi Tanzania ni kwa ajili ya vyama vya upinzani tu. Huko ndio hawalali. Wapo macho saa 24!
Kuzuia uharifu haipo kwenye orodha ya kazi zao labda itokee tu.
 
Kweli ndugu yangu.

Uwezo huo wanao,nia wanayo na sababu pia wanayo. Kwanini hasira hizo kali za wananchi hao zisielekezwe kwa "panya road".
Kuna maandalizi yamefanywa hapa na wananchi kukabiliana na panya road km watakuja kumzika huyu kibaka. Kwa jinsi hali ilivyo,tuombe Mungu panya road wasijitokeze,km watajitokeza kuna uwezekano mkubwa tukashuhudia mauaji ya kutisha ktk eneo hili.
 
Kuna maandalizi yamefanywa hapa na wananchi kukabiliana na panya road km watakuja kumzika huyu kibaka. Kwa jinsi hali ilivyo,tuombe Mungu panya road wasijitokeze,km watajitokeza kuna uwezekano mkubwa tukashuhudia mauaji ya kutisha ktk eneo hili.

Umefanya vizuri sana kuwa na jicho la kiinteligensia.
Ni wapi hapo mkuu?
Hao wananchi nimeufurahia ushirikiano wao.
Mwanzo mzuri kwa utekelezaji dhana ya ulinzi shirikishi.
 
Umefanya vizuri sana kuwa na jicho la kiinteligensia.
Ni wapi hapo mkuu?
Hao wananchi nimeufurahia ushirikiano wao.
Mwanzo mzuri kwa utekelezaji dhana ya ulinzi shirikishi.
Huku ni yombo vituka. Taarifa jioni hii zinasema kesho ndo mazishi na panya road wameahidi kuja kuzika. Kulikuwa na mtu wa baiskeli pale leo alikuwa ananoa shoka,mapanga na sime za wananchi. Me kesho sifungui kabisa biashara! Mchana kulikuwa na mkutano kwa ajili ya patrol wenye biashara za usiku wameambiwa mwisho saa 4 usiku.
 
Yombo vituka eneo linalofahamika km"kwa chande" jana usiku wananchi walimuua kibaka ambae siku 2 kabla ya jana alimkaba Dada mmoja akampora simu kisha akamchoma bisibisi kichwani mara 2,yule dada aka-bleed bila msaada na alipofikishwa hospital ya wilaya ya temeke akafariki dunia!..

Police walifika na kuuchukua mwili wa kibaka kwa uchunguzi na taratibu za ki-police. Inasemekana police wameruhusu mwili wa huyo kibaka kesho uzikwe..
Zipo taarifa kwamba panya road wamejiandaa kuzika wenyewe na baada ya kuzika wamepanga kulipa kisasi!

Baada ya wananchi kupata taarifa hizo,wamejiandaa kikamilifu kupambana na panya road,wamekusudia kuteketeza kabisa hilo kundi. Toka mchana hadi usiku huu,wamefanya maandalizi ya kutisha,na km police chang'ombe watapuuza bandiko hili,na panya road kweli watekeleze azima yao,kesho huenda jiji likashuhudia mauaji ya kutisha!! Wito wangu kwa police,wasiruhusu hao wahuni hata kwenda kuzika. Narudia tena wananchi wamechoka na haya matukio. Km police hawaamini waende pale kwa chande wakathibitishe nilichoandika hapa.

Nawasilisha..!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom