mmbangifingi
JF-Expert Member
- Mar 9, 2011
- 2,839
- 559
Kuna habari,, wananchi "wenye hasira kali" Wilayani Chunya wamevamia na kuvunja kituo cha Polisi Lupa Tinga Tinga kisha kuchoma moto nyumba mbili za askari polisi na moja ya raia. Tukio limefuatia baada ya askari polisi hao kumuua kwa kipigo Said Msabaha,mwanafunzi wa kidato cha pili katika Sekondari ya Lupa Tinga Tinga kwa tuhuma za kuiba simu ya mkononi. Aidha wananchi hao wamechoma moto duka la vinywaji linalomilikiwa na askari polisi mmoja kijijini hapo. Mwenyekiti wa kijiji cha Lupa Tinga Tinga William Mbawala amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.
MY TAKE:
Hii ni dalili ya wananchi/raia kuchoshwa sana na ukatili wa wenzetu hawa askari polisi waliotazamiwa kuwa walinzi wa raia na mali zao. Where will it end?
MY TAKE:
Hii ni dalili ya wananchi/raia kuchoshwa sana na ukatili wa wenzetu hawa askari polisi waliotazamiwa kuwa walinzi wa raia na mali zao. Where will it end?