Wananchi wanasemaji kambi ya upinzani Bungeni?

Dingswayo

JF-Expert Member
May 26, 2009
4,019
2,923
Naomba kufahamishwa kuwa baada ya uchakachuaji wa ccm kuhusu kambi ya upinzani Bungeni, huko mitaani wananchi wanasemaje? Nauliza hili kwa vile hatima ya nchi hii ipo mikononi mwa wananchi, kama jambo hilo si leo, hakika linakuja.
 
CCM imetumia wingi wa wabunge ilionao bungeni kuwezesha kambi ndogo ya upinzani, ambayo mpaka jana haikuwa rasmi kupindua kambi rasmi ya upinzani. Kwakuwa jambo hilo ni kwenda kinyume na maamuzi ya wananchi, CDM INAPASHWA ILIPELEKE suala hilo kwa umma wa watanzania kwa uamuzi wa mwisho.
 
Tunawaangalia tu CCM, wanaonekana wapo out of touch na wananchi wao.....wakicheza vibaya itakula kwao vibaya sana....CHADEMA ni tochi na ina mwanga mkali na inamulika, na wananchi tunaangalia kila inapomulika.....CCM beware!
 
Huyu mama kaanza vibaya na wananchi watamuhukumu yeye na chama chake!!
 
Shillingi ina pande mbili hivyo hivyo Bungeni kuna pande mbili - Upande wa Chama kinachounda Serikali na Upande wa vyama visivyo serikalini (Upinzani); hivyo maamuzi ya Bunge ya kutengua kanuni yako sahihi. Ambacho hakitakuwa sahihi ni ONE MAN POLITICAL PARTY kupewa jukumu la kuongoza kamati nyeti zinazosimamia matumizi ya rasilimali za nchi.

Kama kweli CCM wanamapenzi mema na nchi hii, wangeongezea kwenye hiyo kanuni isomeke kwamba "Uchaguzi wa wenyeviti wa kamati zinasopaswa kuongozwa na kambi ya upinzani utafanywa na wabunge wa upinzani pekee".
 
....kwa kuwa hata mimi ni mwananchi na pia wa mtaani,,,,sikubaliani kwa asilimia 101% kuhusu uundwaji wa kambi ndogo ya "CCM_B", bungeni!!!
 
....kwa kuwa hata mimi ni mwananchi na pia wa mtaani,,,,sikubaliani kwa asilimia 101% kuhusu uundwaji wa kambi ndogo ya "CCM_B", bungeni!!!

Hakuna kambi ndogo, kilichoamuliwa ni kuwa na kambi mbili - Ya Chama tawala na ya Vyama vya upinzani
 
Kwa pande za Arusha, Majority ya watu wanaifagilia CHADEMA tu. Na hiyo issue ya jana ndio story kila pande. Watu wanaona kama CHADEMA wanaonewa hivyo hasira kwa ccm ndio imezidi. Masela wangu wa porini (mererani) wamenipigia simu kutaka kujua kuhusu ilivyotokea jana ingawa nawajua huwa hawafuatiliagi siasa kabisa. Kwa sasa hivi kuna bonge ya tension na watu wana link hii na yanayotokea misri na tunisia. Mi naona kama atakuja mtu influential akasema watu waingie street, yanayotokea misri itakua cha mtoto kwa comparison. Mimi mwenyewe nawatamani sana hawa wadosi. Wanatukatia umeme karibia daily halafu pande za uzunguni hata hawajui kama kuna mgao.

Halafu kwa hizi siku za karibuni, Landcruiser mkonge za polisi mpya zimekua nyingi hadi zinashindana na daladala kwa wingi. Kila kona ukipita unazikuta. kama wamezileta hizi kutokana na intelijensia yao ilivyowatuma, then, this time wako right! Ingawa kwa sasa polisi washakua mashemeji zetu hivyo hatuwaogopi.
 
Back
Top Bottom