DOKEZO Wananchi wa Mbagala walalamikia DAWASA kusitisha huduma ya mwekezaji binafsi

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,986
Wakazi wa Mitaa ya Bughudadi, Kizinga na Moringe, Kata ya Mbagala wameilalamikia Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) wa kutowatimizia mahitaji yao ya maji maeneo yote na kudai kuwa hali hiyo inawalazimu kutumia muwekezaji binafsi kupata huduma hiyo.

Malalamiko hayo yamekuja kutokana na hivi karibuni uongozi wa DAWASA Kata ya Mbagala kutoa notisi ya kumtaka mwekezaji binafsi kusitisha usambazaji wa maji ndani ya siku 30 kwa kuwa anafanya kazi kinyume cha utaratibu.

Sehemu ya malalamiko hayo ambayo Wananchi wameyawasilisha kwa Diwani wa Kata hiyo kwa njia ya maandishi tarehe 24 Oktoba 2022 wamedai kuwa wamesikitishwa na maamuzi hayo kwa kuwa wameshatoa ushauri wao kwa DAWASA lakini haujafanyiwa kazi.

Katika malalamiko hayo wananchi hao wa mitaa hiyo mitatu wameeleza kuwa kabla ya zoezi la kusitishwa kwa huduma ya mwekezaji binafsi waliomba kikao cha DAWASA na Wananchi ili watoe dukuduku lao kuhusu huduma za DAWASA lakini hilo halijafanikiwa.

Pia wameeleza kuwa hofu yao ni kuwa mwekezaji huyo ambaye amekuwa akitoa huduma hiyo ya maji tangu mwaka 2008 hata kabla ya DAWASA kuanza kutoa huduma eneo hilo, amemuwa msaada kwao wakati huu ambao kuna shida ya maji na Serikali imeto tamko juu ya uhaba wa maji.

Alex Mgala, Mjumbe wa Serikali ya Mtaa wa Bughudadi amesema: "Ni kweli malalamiko yapo kutoka kwa wananchi, tulipata barua kutoka DAWASA na sisi tukawaomba kwa mdomo kukutana nao tushauriane kuhusu uhalisia wa tatizo la maji lakini hawakutupa nafasi hiyo.

"Tumeshapeleka malalamiko yetu kwa Diwani wa Mbagala, Mwenyekiti wetu anashughulikia suala hilo, sisi hatua lengo baya na DAWASa, tunachohitaji ni huduma nzuri ya maji, kumuondoa mwekezaji binafsi wakati wao hawajajipanga ni sawasawa na kurejesha tatizo la maji kwetu."
Barua.jpg

Akizungumzia kuhusu malalamiko hayo, mmoja wa viongozi wa DAWASA Mbagala alisema: “Mimi siyo msemaji wa DAWASA, lakini kwa ufupi niseme tu hatujapata malalamiko rasmi kutoka kwa wananchi kuhusu sisi kutokidhi mahitaji.

“Tukipata malalamiko yoyote tutayafanyia kazi, kuhusu mwekezaji binafsi wa Bughudadi ni kweli amekuwa akifanya kazi kinyume cha sheria na ameeleweshwa juu ya hilo hata kama amekuwa akiuza maji kwa kusaidia wananchi.

“Tupo naye katika mazungumzo na tunaendelea vizuri.”

Hata hivyo, kutokana na kupungua kwa maji katika Mto Ruvu ambao unatumika kusambaza maji katika baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Pwani na Dar es Salaam, Waziri wa Maji Jumaa Aweso ameshatoa maelekezo kwa kuagiza DAWASA kushirikiana na wenye visima vya maji kutoa huduma hiyo ili kupunguza madhira yanayowapata wakazi wa mikoa hiyo.
 
Mbagala hawana Kabisa tatizo la Maji kwakuwa Walikuwa wakitengwa na gvt waliamua kuanzisha miradi yao hivyo hayo matangazo ya mgao wa Maji Wala hayawahusu Kabisa ukifika Mbagala Maji ni mengi Sana unatumia upendavyo na Kuna Maji baridi na chumvi utauziwa kwa Unit .
Sasa DAWASA inataka hao wenye miradi binafsi wastopishe, hapo ndipo hoja inapoanzia, siyo kwamba wana shida ila ni kwa kuwa wanahisi mamlaka zikiondoa wawekezaji hao binafsi ndipo mziki utakapoanza kwa kile wanachoona DAWASA hawajitoshelezi kutoa huduma kwa watu wote.
 
Sasa DAWASA inataka hao wenye miradi binafsi wastopishe, hapo ndipo hoja inapoanzia, siyo kwamba wana shida ila ni kwa kuwa wanahisi mamlaka zikiondoa wawekezaji hao binafsi ndipo mziki utakapoanza kwa kile wanachoona DAWASA hawajitoshelezi kutoa huduma kwa watu wote.
Hivi hao Dawasa inaongozwa na watu wenye akili timamu kweli??

Yaani huyo jamaa asitishe kusambaza maji kisa upuuzi wao,halafu wananchi wakose maji wafe
 
Kuna vitu vya ajabu, kule toangoma maskani nilichimba kisima nikagawa upendo, serikali inanifungia mwaka ule wa mwendazake
 
Maji ya Bomba ni ANASA. Watanzania tusiendekeza na kupenda anasa. Kwani usipotumia maji ya bomba utakufa?
 
Watu wana vichwa, halafu wanatumia makalio kufikiri.

Dawasa wanataka kukuza tatizo la maji, malalamiko yakiwa mengi watajidai serikali inatoa suluhisho 😂
 
Tayari nimeshakuwini kisaikolojia Ndo hicho haswa nilikuwa nang'ang'ania na kusumbuka kutafuta. Nimekuvutaa wee hadi umeingia kimiani mwenyeweee.

Inflicting pain and annoyance without physical altercation.

Leaving the victim helpless and hopeless. What he can do to defend and comfort himself is to hurl insults.

While me on the other side jumping and punching the air profusely, relentlessly, aggressively and violently with Jubilation!

Maamaee JF!

Unadhani alielewa kama umewakejeli DAWASA? Watu walishachanganyikiwa hata kujua hii ni sarcasm hakuna
 
Kuna vitu vya ajabu, kule toangoma maskani nilichimba kisima nikagawa upendo, serikali inanifungia mwaka ule wa mwendazake
Sijui tuna mifumo gani, kiasi kwamba alienacho abaki nacho na asie nacho atajuta kutokua nacho
 
Tanzania ni moja kati ya nchi nisizozipenda duniani kwasababu hizo hapo juu.. kuanzia rais mpaka watenda kazi wake hawajui kutumia akili, uongozi ni dhamana, kuongoza watu kunahitaji hekima ya juu sana bila Mungu utakufa na laana za watu uliowatesa.
 
Kama hata wao hawana maji wanazuiaje watu binafsi kuwasaidia kutoa huduma kwa wananchi? hii nchi ngumu sana aisee, kimsingi watanzania wanatakiwa kuamka na kuanza kujichukulia sheria mkononi vinginevyo viongozi wataendelea kuwaingizia vidole sehemu nyeti , maana wanawaona mazuzu sana kwa kukaa kimya wakati wana matatizo lukuki
 
Back
Top Bottom