Wananchi tusipopaza sauti zetu kwa nguvu zetu zote hakika Taifa letu linakwenda kuangamia!

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,160
Haihitaji kuwa mtabiri kuliona hili jambo kuwa nchi yetu inapitia katika kipindi cha hatari ambacho hakijawahi kupitiwa tokea nchi yetu ipate Uhuru wake mwaka 1961........

Wasomaji wa mada hii mtakuwa na shauku ya kujua kivipi Taifa letu linapitia katika kipindi cha hatari?

Nitafafanua suala hilo kama ifuatavyo:-

Ingawa Taifa letu lina Katiba ya nchi ambayo ndiyo sheria mama ya nchi yetu, tumeshuhudia tokea Rais wetu wa awamu ya 5 aingie madarakani ni kama vile "ameisuspend" kutumika nchini Katiba ya nchi yetu na matamko yake ya kwenye majukwaa ya kisiasa ameyageuza kuwa ndiyo sheria za nchi hii zinazopaswa kufuatwa!

Hivi ni nani asiyejua kuwa Katiba ys nchi yetu inatamka wazi kuwa nchi yetu ni ya mfumo wa vyama vingi na vyama hivyo vinapaswa kufanya shughuli zake bila kuingiliwa na chombo chochote?

Sasa tujiulize Rais wetu alitumia mamlaka yapi kupiga marufuku mikutano ya kisiasa ya vyama vya upinzani hususani chama kikuu cha upinzani nchini cha Chadema hadi ifikapo mwaka 2020 wakati yeye na chama chake cha CCM wakiendelea kufanya mikutano ya kisiasa nchi nzima bila kuzuiwa na Polisi?

Na je Jeshi letu la Polisi linapata wapi mamlaka ya kuwakamata viongozi wetu wa vyama vya upinzani wanapotekekeleza majukumu yao ya kisiasa kwa mujibu wa Katiba kama siyo kutekeleza maagizo "batili" ya Rais wetu?

Tumeshuhudia wabunge almost wote wa Chadema kwa nyakati tofauti wamekuwa wakikamatwa na Jeshi letu la Polisi kwa ajili tu ya kufanya mikutano ya kisiasa ambayo ni haki yao ya kikatiba lakini serikali hii ya awamu ya 5 na Jeshi letu la Polisi imekuwa ikiichukulia kuwa ni mikutano haramu isiyopaswa kuwepo!

Mwalimu Nyerere katika moja ya hotuba zake alipokuwa hai aliwahi kusema kuwa Rais wetu tunayemchagua ni lazima aitii na kuilinda Katiba ya nchi yetu ambayo aliapa kuilinda kabla hajakabidhiwa madaraka ya kuliongoza Taifa letu.

Mwalimu akaenda mbali zaidi katika hotuba hiyo kwa kusema kuwa anapotokea Rais ambaye hataki kuitii Katiba ya nchi yetu Rais wa aina hiyo HATUFAI....

Mwalimu akamalizia hotuba hiyo ya hekima kubwa kwa kusema atakapotokea Rais wa aina hiyo wananchi tuna wajibu wa kumwambia Rais wa aina hiyo atuachie Urais wetu na yeye akafanye shughuli zake nyingine kama vile kufunga ng'ombe na kadhalika.....

Inashangaza kuona watanzania tukimuona Rais wetu akiisigina waziwazi Katiba ya nchi yetu na sisi wananchi ambao ndiyo Waajiri wa huyo mwajiriwa wetu (Rais) tunaamua kukaa kimya na kuendelea kumshangilia kwa uvunjifu huo wa wazi wa Katiba ya nchi yetu!

Iwapo kweli sisi wananchi bila kujali itikadi zetu za kisiasa kama kweli tunataka kumuenzi Mwalimu kwa vitendo tunapaswa kupaza sauti zetu kwa nguvu zote kumwambia Rais wetu arejee kwenye mstari na aiongoze nchi yetu kwa mujibu wa Katiba yetu, na kama hatataka kuongoza nchi yetu kwa mujibu wa Katiba yetu, wananchi tunapaswa kumuenzi Mwalimu Nyerere kwa vitendo kwa kufuata wosia wake kwa kumwambia Rais wetu kuwa tunakuomba utuachie Urais wetu na wewe nenda kafanye shughuli zako nyinginezo..........

Mungu libariki Taifa letu la Tanzania
 
Njaa zinasumbua sana!!! Ongeza bidii utaanza kulipwa mshahara

Sent using Jamii Forums mobile app
Njaa ipi Mkuu hebu nifafanulie?

Tena wewe kwa kuwa avatar yako umeweka picha ya Mwalimu, ndiye unayepaswa kuwa mstari wa mbele kumuenzi Mwalimu kwa vitendo kwa kumwambia Rais wetu aongoze Taifa letu kwa mujibu wa Katiba ya nchi yetu.....
 
Njaa ipi Mkuu hebu nifafanulie?

Tena wewe kwa kuwa avatar yako umeweka picha ya Mwalimu, ndiye unayepaswa kuwa mstari wa mbele kumuenzi Mwalimu kwa vitendo kwa kumwambia Rais wetu aongoze Taifa letu kwa mujibu wa Katiba ya nchi yetu.....
Njaa huweza kusababisha itikadi Fulani kutangulizwa na kuacha nyuma maslahi ya Taifa!!! Pengine hoja yako ni dhaifu sana kwakuwa ina mlengo wa kiitikadi na si uchambuzi yakinifu uliojaa taswira ya kuliendeleza Taifa kimaendeleo na si kuendeleza Taifa Kimajungu.

Unapotuletea hoja humu jitahidi kuwa mzalendo halisia usiyeonyesha kulalia upande wwte na Unapotuigizia kuwa ww n mzalendo ili khari unaonyesha dhahiri unachumia tumbo sisi hatuna budi kukutia Moyo uongeze bidii ili tumbo lishibe.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Njaa huweza kusababisha itikadi Fulani kutangulizwa na kuacha nyuma maslahi ya Taifa!!! Pengine hoja yako ni dhaifu sana kwakuwa ina mlengo wa kiitikadi na si uchambuzi yakinifu uliojaa taswira ya kuliendeleza Taifa kimaendeleo na si kuendeleza Taifa Kimajungu.

Unapotuletea hoja humu jitahidi kuwa mzalendo halisia usiyeonyesha kulalia upande wwte na Unapotuigizia kuwa ww n mzalendo ili khari unaonyesha dhahiri unachumia tumbo sisi hatuna budi kukutia Moyo uongeze bidii ili tumbo lishibe.


Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa hiyo kwa maoni yako wewe unamwona hata Baba wa Taifa letu Mwalimu Nyerere kuwa alikuwa "mpuuzi" kwa kutuasa watanzania tuhakikishe Rais wetu anaongoza kwa mujibu wa Katiba ya nchi yetu?

Hebu nikuulize swali jepesi tu wewe unsyejifanya ni mzalendo wa hli ya juu wa Taifa letu.

Hivi kuna maana gani Rais wetu kuapa kuitii na kuilinda Katiba ya nchi kabla ya kukabidhiwa madaraka iwapo wewe unaiona Katiba ya nchi kama si lolote wala chochote?
 
Njaa huweza kusababisha itikadi Fulani kutangulizwa na kuacha nyuma maslahi ya Taifa!!! Pengine hoja yako ni dhaifu sana kwakuwa ina mlengo wa kiitikadi na si uchambuzi yakinifu uliojaa taswira ya kuliendeleza Taifa kimaendeleo na si kuendeleza Taifa Kimajungu.

Unapotuletea hoja humu jitahidi kuwa mzalendo halisia usiyeonyesha kulalia upande wwte na Unapotuigizia kuwa ww n mzalendo ili khari unaonyesha dhahiri unachumia tumbo sisi hatuna budi kukutia Moyo uongeze bidii ili tumbo lishibe.


Sent using Jamii Forums mobile app
Hapa ninachosema ni Rais wetu aongoze kwa mujibu wa Katiba ya nchi yetu.

Sasa sijui hiyo unayoiita njaa yangu inakujaje hapo?

Hebu kuwa mkweli hivi wewe huoni namna Rais wetu anavyoisigina Katiba ya nchi yetu kadri atakavyo?

Na anafanya hivyo kwa kuwa anajua Katiba hiyo hiyo inampa kinga ya kutoshitakiwa kwa makosa ya aina yoyote awapo madarakani na hata pale atakapoondoka madarakani!
 
Hapa ninachosema ni Rais wetu aongoze kwa mujibu wa Katiba ya nchi yetu.

Sasa sijui hiyo unayoiita njaa yangu inakujaje hapo?

Hebu kuwa mkweli hivi wewe huoni namna Rais wetu anavyoisigina Katiba ya nchi kadri atakavyo?

Na anafanya hivyo kwa kuwa anajua Katiba hiyo hiyo inampa kinga ya kutoshitakiwa kwa makosa ya aina yoyote awapo madarakani na hata pale atakapoondoka madarakani!
Ukitaka nikuelewe! Acha kutega watu,eleza ni kwa namna gani Rais anasigina katiba ukibainisha hoja zako moja baada ya nyingine!
Itakusaidia kuwa mtoa hoja mzuri usietiliwa shaka lolote kiitikadi!!! Ila ukija kiitikadi tutajua na tutakuomba ulete hoja za kitaifa na s kikanda!
Nadhani unaelewa haraka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tunachongoja tu na yeye aangamie na nchi ambayo kesha iangamiza na mideni ya kesi Canada,samaki wa magufuli,nyumba za serikali,sasa inabidi maafisa watumie kodi zetu kuwapangishia nyumba / hoteli kwa nchi maskini kama yetu ! na wakati zingine aligawia mchepuko !.Mungu huyu mtu unamjua wewe Mimi nakulilia tu juu yake ili ufanye kinachomstahi,kwa jinsi alivyoingiza nchi pa baya,Amen

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi kwa hii kamata kamata ya mfululizo ya viongozi wa vyama vya upinzani, hususani wabunge wa chama kikuu cha upinzani nchini cha Chadema, hivi Jeshi letu la Polisi unaweza kulitofautisha na lile Jeshi la Polisi la Afrika Kusini la enzi zile za ubaguzi wa rangi?

Tofauti yake itakuwa moja tu kuwa Jeshi la Polisi la enzi zile kule Afrika Kusini lilikuwa linafanya ubaguzi wa rangi na Jeshi letu linafanya ubaguzi wa itikadi za kisiasa.....

Hebu tujikumbushe tena maneno ya hekima kubwa aliyowahi kuyatoa Mwalimu Nyerere enzi za uhai wake katika moja ya hotuba zake.

Mwalimu alisema yafuatayo katika hotuba hiyo "Hatukuwaita wazungu wa Afrika Kusini makaburu kutokana na rangi yao nyeupe, LA HASHA, tuliwaita wazungu wa Afrika Kusini kutokana na tabia zao za kibaguzi, kwa hiyo yeyote anayefanya ubaguzi wa aina yoyote whether ni mweupe au ni mweusi naye ni kaburu tuu" mwisho wa kunukuu

Hivi kwa huu ubaguzi wa itikadi za kisiasa unaofanywa na Rais wetu na Jeshi lake la Polisi hivi kwa mujibu wa hotuba hiyo ya Mwalimu Nyerere hivi sisi wananchi tutakuwa tumekosea kuwaita hao watu kuwa nao ni makaburu tuu?

[HASHTAG]#Hatunyamazi[/HASHTAG] hadi tuwe wafu
 
Mkutano Ĺema alifanya pia juzi ulikuwa wa nini!?

Imebidi nicheke.. miaka hii unaandika hayo na dake ID.. kama unataka yafanyike si uwatie wenzako mluo wavivubn mnaoisoma namba.. uweke jina na picha yako kabisa ili uvutie wengine kwenye huo ushawishi wako au!?
Yote haya ni kukosa mengi na uoga juuu eeeh... muoga chezea kukosa maarifa eeeeh
 
Back
Top Bottom