Dr Adam Francis
JF-Expert Member
- Aug 12, 2011
- 478
- 711
Kama kuna kitabu ningeshauri kila mwananchi akisome kwa sasa ni tamthilia ya "Animal Farm" ya George Orwell (1945)
Hii ni simulizi ya wanyama walioamua kuuasi na kuupindua utawala wa mkulima katili ili waishi maisha ya kijamaa yanayozingatia usawa walioyaita Animalism wakiwa na kauli mbiu ya "All animals are equal."
Baada ya kufanikisha mapinduzi na kuanza kujitawala wakawachagua nguruwe kuwa viongozi wao. Nguruwe waalipotwaa madaraka tu, wakaanzisha propaganda kueleza kuwa nguruwe ni bora kuliko wanyama wengine, mwishowe wakaanza kutenda mambo yale yale mkulima katili aliyokuwa akiwatendea wanyama. Wanyama walipowauliza nguruwe kulikoni, mbona hatuwaelewi? Wakawaeleza "All animals are equal, but some animals are more equal than others." Mwisho hakukuwa na tofauti kati ya mkulima katili na nguruwe.
Hii ni tamthilia yenye mafunzo mengi yanayoakisi hali halisi ya Afrika baada ya madai ya uhuru kutoka kwa wakoloni. Ni tamthilia iliyojaa masomo ya propaganda, power, na political systems. Mwisho inatuasa kuwa waangalifu na madaraka tunayowapa viongozi wetu kwani "Power corrupts, but absolute power corrupts absolutely."
Siku hizi kumeanza kusikika mwananchi mmoja akiwaambia wananchi wenzake kuwa nchi ina wenyewe, au mtatufanya nini, au mtake msitake, au ole wenu! Haya ni maneno yanayofikirisha sana! Hivi ni kweli nchi ni ya wananchi wote? Hivi ni kweli kuna usawa kati ya wanajiita wenyenchi na wanaoitwa wananchi? Au ndio wenye nchi are more equal than wanachi, kama ilivyokuwa kwenye animal farm?
Ni dhana inayokubalika kuwa haitoshi tu kusema tuna haki na usawa, ni muhimu pia haki na usawa kuonekana kwa wazi ikitendeka.
Ubaguzi na uonezi ni jambo la kawaida kama anayeonewa sio wewe wala mtu unayehusika naye, itakapotokea wewe kuwa kwenye kundi la kuonewa na kubaguliwa ndio utakapoiona ladha yake.
Rai yangu tusitoe majibu mepesi kwa maswali magumu yahusuyo ubaguzi, unyanyasaji, ukandamizaji na dhuluma katika nchi zetu. Mambo haya yanaua umoja wa kitaifa. Kama nchi ni yetu sote, ni jukumu letu sote kuona kuwa kila mmoja anapata haki sawa kwa mujibu wa sheria.
Hii ni simulizi ya wanyama walioamua kuuasi na kuupindua utawala wa mkulima katili ili waishi maisha ya kijamaa yanayozingatia usawa walioyaita Animalism wakiwa na kauli mbiu ya "All animals are equal."
Baada ya kufanikisha mapinduzi na kuanza kujitawala wakawachagua nguruwe kuwa viongozi wao. Nguruwe waalipotwaa madaraka tu, wakaanzisha propaganda kueleza kuwa nguruwe ni bora kuliko wanyama wengine, mwishowe wakaanza kutenda mambo yale yale mkulima katili aliyokuwa akiwatendea wanyama. Wanyama walipowauliza nguruwe kulikoni, mbona hatuwaelewi? Wakawaeleza "All animals are equal, but some animals are more equal than others." Mwisho hakukuwa na tofauti kati ya mkulima katili na nguruwe.
Hii ni tamthilia yenye mafunzo mengi yanayoakisi hali halisi ya Afrika baada ya madai ya uhuru kutoka kwa wakoloni. Ni tamthilia iliyojaa masomo ya propaganda, power, na political systems. Mwisho inatuasa kuwa waangalifu na madaraka tunayowapa viongozi wetu kwani "Power corrupts, but absolute power corrupts absolutely."
Siku hizi kumeanza kusikika mwananchi mmoja akiwaambia wananchi wenzake kuwa nchi ina wenyewe, au mtatufanya nini, au mtake msitake, au ole wenu! Haya ni maneno yanayofikirisha sana! Hivi ni kweli nchi ni ya wananchi wote? Hivi ni kweli kuna usawa kati ya wanajiita wenyenchi na wanaoitwa wananchi? Au ndio wenye nchi are more equal than wanachi, kama ilivyokuwa kwenye animal farm?
Ni dhana inayokubalika kuwa haitoshi tu kusema tuna haki na usawa, ni muhimu pia haki na usawa kuonekana kwa wazi ikitendeka.
Ubaguzi na uonezi ni jambo la kawaida kama anayeonewa sio wewe wala mtu unayehusika naye, itakapotokea wewe kuwa kwenye kundi la kuonewa na kubaguliwa ndio utakapoiona ladha yake.
Rai yangu tusitoe majibu mepesi kwa maswali magumu yahusuyo ubaguzi, unyanyasaji, ukandamizaji na dhuluma katika nchi zetu. Mambo haya yanaua umoja wa kitaifa. Kama nchi ni yetu sote, ni jukumu letu sote kuona kuwa kila mmoja anapata haki sawa kwa mujibu wa sheria.