Wanamtwara mmesahau kuliwa na Simba?

Wanamtwara mmesahau kuliwa na Simba?

Barbarosa

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2015
Posts
22,584
Reaction score
27,837
Ningekuwa ni mwana Mtwara ile kumuona tu Bw.Makongoro Nyerere ningeweza hata kuzimia huyu Bwana na anavyofanana na Baba yake Mlm.Nyerere (,,Apumzike kwa Amani") ingenikumbusha mambo mabaya sana yaliyowahi kutokea nchini mwetu chini wa Utawala wa Baba yake!

Kuhamishwa watu kutoka vijijini kwao na kupelekwa vijiji vipya ambavyo vilikuwa havijaandaliwa ipasavyo hali iliyopeleka Wananchi wengi wa Mtwara kupoteza Maisha kwa kuliwa na Simba ni ajabu jamaa yule yule ambaye wakati mnaliwa na Simba yeye alikuwa Magogoni na Msasani anakula bata leo anaomba idhaa kwenu mmpe urais!

Ningekuwa mimi ningemfukuzilia mbali!
 
Ccm yote shida ukiwemo wewe,lakini ninavuojua wtu Wa ukanda Wa pwani na akili Yao ya kuoa watoto wenye umri Wa miaka 8 kama Masai ni shida nchi hii !
 
Mtwara ya leo siyo ya jana mkuu,ccm kwa mtwara ishaaga kitambo na wao wanalijua vizuri sana.
 
Mkuu Barbarosa, hapo kosa la Mako ni lipi? Au tatizo ni kukulia Magogoni?

Kama kosa alitenda Mwl na sio Mako,Mtwara ya Mwalimu ni tofauti na Ya Kikwete.

Je, unajua dhumuni la mwalimu kuwahamisha wanamtwara baadhi na kuwapeleka huko?

Je, unajua kuwa vijiji vingi vya Mtwara na Lindi miaka ile havikuwa salama kutokana na uwepo wa wanyama wakali kama simba lakini bado watu waliweza kuishi?

Je, unajua mpaka sasa kuna vijiji Mtwara na Lindi wananchi bado wanaliwa na Simba? Unajua kuwa ikifika jioni wanajifungia ndani au kutembea kwa tahadhari katika makundi?

Acha kulalamika kaka, mpime Mako kwa hoja zake na sio maisha aliyoishi baba yake.
 
Last edited by a moderator:
Ccm yote shida ukiwemo wewe,lakini ninavuojua wtu Wa ukanda Wa pwani na akili Yao ya kuoa watoto wenye umri Wa miaka 8 kama Masai ni shida nchi hii !

Me nilikuwa najua huko bara wote ni UKAWA na mna maisha mazuri. Nilivyofika nimekuta mashimo wanaume washaondoka na dhahabu, halafu mbunge wa CCM....Hehehe njooni Mtwara muone wanaume wanavyodai rasimali zao zisitoke ovyo ovyo. Watu wa bara ovyo sana, porojo nyingiii...
 
Mtwara ya leo siyo ya jana mkuu,ccm kwa mtwara ishaaga kitambo na wao wanalijua vizuri sana.

Anaongea ushabiki huyo. Muulize anakujua hata huko Mtwara.
 
Mwaka 2009 April kijana aliliwa na Simba kijiji cha Namambi kuelekea Mnima wakati Nyerere akiwa teyari hayati

Pia mwaka huo huo mama moja aliliwa na samba watatu kijiji cha Mkahala Mwl Nyerere akiwa teyari hayati

Ndani ya miaka 10 ya utawala wa Mh. Kikwete watu wawili wameliwa na simba Mtwara sasa je siku akija mtoto wake Ridhiwan kuomba udhamini tumfukuze?
 
Barbarosa

kumbuka Makongoro anatetea sisi wanyonge,ccm imetekwa na vibaka by makongoro
 
Last edited by a moderator:
Barbarosa hii nyuzi wote wanaikimbia.

Hawataki kuyakubali hayo, "saint" aweje hivyo?

Hapo sasa!
 
Last edited by a moderator:
Nyerere alikuwa na nia nzuri sio kuwakomoa eti waliwe na samba. Wananchi wawe karibu ili serikali iweze kuwafikishia huduma muhimu kama maji, zahanati, shule, masoko na nyumba za ibada.

Nyerere kuwa mwenye heri kuna vitu vingi vinaangaliwa!
 
Barbarosa

Yaani kwa wanamtwara sio Makongoro tu kwa Wana Mtwara CCM ni tatizo ni janga inapaswa wasiisahau,ni juzijuzi tu wameonja shida wameishi kama wapo enzi za ukoloni wa Mjerumani,Mtwara kulikuwa hakuna uhuru,hakuna kukaa katika vikundi vya mijadala kwa kweli nakusapoti Asilimia mia Moja wakiona mtu yeyote wa CCM inabidi wapaze sauti kubwa ya kumkataaa.wana Mtwara Say No to CCM
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom