Wanamazingaombwe kina Profesa Singira, Muhindi Mchafu etc

Wanamazingaombwe kina Profesa Singira, Muhindi Mchafu etc

asee! nimekumbuka mbali kwenye mazingaombwe tulikuwa tunaingia na ndimu na sindano au tunageuza viatu cha kulia kipo kushoto na kushoto kinakuwa kulia eti ndo tunaharibu mazingaombwe yao, hahahah!
mazingaombwe yalikua kwenye shule za kidumu ma mfagio tu, shule za magari ya njano hawajui izi mambo, yani darasa limepigwa pazia mnajazana kwenye darasa joto nyuzi 99 hahahahah!
 
Wale WANA MAZINGAOMBWE waliokua wanageuza MAKARATASI kuwa HELA tukiwa PRIMARY SCHOOL wapo Wapi? Huu ndio Muda Sahihi sasa mimi nina RIM PAPER Kama 3 hivi Hazina Matumizi.
Wewe jamaa umifurahisha, nimejikuta nacheka! Eti una ream nzima wataka igeuzwe hela! Jamaa walikuwa wanatafuna sindano vinatokea vitambaa!
 
asee! nimekumbuka mbali kwenye mazingaombwe tulikuwa tunaingia na ndimu na sindano au tunageuza viatu cha kulia kipo kushoto na kushoto kinakuwa kulia eti ndo tunaharibu mazingaombwe yao, hahahah!
mazingaombwe yalikua kwenye shule za kidumu ma mfagio tu, shule za magari ya njano hawajui izi mambo, yani darasa limepigwa pazia mnajazana kwenye darasa joto nyuzi 99 hahahahah!
Si walikuwa wanatutisha ukigeuza viatu vyako ukirudi nyumbani unakuta wazazi wako wamekufa...basi hakuna aliethubutu
 
Wale WANA MAZINGAOMBWE waliokua wanageuza MAKARATASI kuwa HELA tukiwa PRIMARY SCHOOL wapo Wapi? Huu ndio Muda Sahihi sasa mimi nina RIM PAPER Kama 3 hivi Hazina Matumizi.
Sasa hivi kuna mateja wanafanya hizo mambo kwenye vituo vya daladala, wanawapiga sana wanawake kwa vitisho, ukikanyaga tu ule unga wao waliozungushia wanaanza kukubabaisha kwa mtu asiyewajuwa
 
Hawa jamaa ndio walioeneza story za kwamba Zeruzeru hawafi
Nkumbuka kuna mmoja alikujaga akawa anasema kama mnabisha hawafi tumwoneshe Kaburi alilozikwa Zeruzeru, baada nilikuja kugundua kumbe kulikuwa na ushirikina wa kutumia viungo na mifupa ya Albino kwenye shughuli zao.
 
Sasa hivi kuna mateja wanafanya hizo mambo kwenye vituo vya daladala, wanawapiga sana wanawake kwa vitisho, ukikanyaga tu ule unga wao waliozungushia wanaanza kukubabaisha kwa mtu asiyewajuwa
Wale watakuwa Na vipaza sauti wanasema atatengeneza nyoka, mnasimama masaa matatu huoni alichofanya
 
Hawa jamaa ndio walioeneza story za kwamba Zeruzeru hawafi
Nkumbuka kuna mmoja alikujaga akawa anasema kama mnabisha hawafi tumwoneshe Kaburi alilozikwa Zeruzeru, baada nilikuja kugundua kumbe kulikuwa na ushirikina wa kutumia viungo na mifupa ya Albino kwenye shughuli zao.
Kweli kabisa tulisadikishwa kuwa wanayeyuka, hawafi
 
hahahahha looong time aisee,jamaa sijui alipotelea wapi yule,kuna mwingine power mabula.... later on akatokea na jamaa wa kupaa na pikipiki...
Alikuwa anaruka magari zaidi ya matatu, nakumbuka alijaza uwanja wa Sokoine, enzi hizo ukiitwa Uwanja wa Mapinduzi
 
Back
Top Bottom