Wanalima kweli au?


...WoS,...kuna mahala niliwahi soma haya maneno,.."talk is cheap!"...na ukiona mbwa anabweka sana ujue haumi huyo.
Sasa basi, kabla maneno hayajaanza nigeukia mwenyewe naomba niigongelee msumari mwingine hoja yangu...
"kelele za mlango....!"

nitamalizia..'hazimnyimi mwenye nyumba kulala siyo?......
kelele hizi nazo ukizipuuza sana utajikuta unaadhirika ujue!
 
Vijembe vyenyewe butuuuuu aaarrrrrgggg

lol...Gaga weee,..stara basi kidogo lohhh? ha ha ha!
Huwezi jua, labda ardhi yenyewe haisharifiki kwa jua wala mvua!

nitamalizia..'hazimnyimi mwenye nyumba kulala siyo?......
kelele hizi nazo ukizipuuza sana utajikuta unaadhirika ujue!

....WoS, kama pumba na chuya tu,...unapotwanga lazima upepete!
 

lol...Gaga weee,..stara basi kidogo lohhh? ha ha ha!
Huwezi jua, labda ardhi yenyewe haisharifiki kwa jua wala mvua!



....WoS, kama pumba na chuya tu,...unapotwanga lazima upepete!
Sasa si wanoe majembe yao au watumie kilimo cha kisasa?
 
mhhh.. nashindwa hata kushangaa!! Ila kwenye kilimo kwanza Gaga, kuna power tillers... hujazisikia hizi?
Sijui kama zimeboresha kilimo kwa maana ya tija!
Haaaa WOS umeshasahau walipewa mkopo bila kupewa chanzo cha pesa hatimae wamepaki hizo tillers zimeharibika kwa matumizi mabaya, wengi wanaume walikuwa wanaendesha kwendea vijiji vya jirani kwa mahawara zao
 
Haaaa WOS umeshasahau walipewa mkopo bila kupewa chanzo cha pesa hatimae wamepaki hizo tillers zimeharibika kwa matumizi mabaya, wengi wanaume walikuwa wanaendesha kwendea vijiji vya jirani kwa mahawara zao


Kumbe kuna matumizi mabaya hivi ya vitendea kazi jamani!!!?? Hili nalo neno!

Huenda ikawa sababu ya kushindwa kufanikisha kilimo kwanza!
 
duh.. huwa sichanganyikiwi kirahisi lakini leo mmefanikiwa kunichanganya; mwenyewe nimedandia treni kwa mbele nadhhani tunazungumzia zile kazi ambazo wanakijiji tunasifika kuzifanya yaani kulima udongo na kupanda mazao. Kwamba wanawake wanafanya kazi hizi sana ni ukweli wa muda mrefu, wanaume nao wanafanya kazi lakini in relation to overall work ya mwanammke ni wazi kuwa mwanammke anajikuta anafanya zaidi kwani.. wakazi "mzee" bado anakula mto mama atakuwa ameshaamka na kuanza mambo ya usafi na maandalizi ya kifungua kinywa.

Mambo yakiwa tayari ndio mzee anatoka na kwenda bafuni ambako atakuta ndoo ya maji ya moto vinamsubiria kwa raha zake. Wakitoka hapo watoto watakuwa wameshakula kiporo au chai na mihogo na kwenda zao shule ndio baba na mama waende shambani.

Huko shambani pamoja na kulima mama anaokoteza okoteza kuni; wakati wa mchana, japo wote wawili walikuwa wanalima ni mama inabidi ajipikilishe kidogo hapo wanakula na labda watapumzika kidogo (mzee ataenda kuuchapa kidogo chini ya mti kitumbo juu). Saa tisa hivi za mchana ngwe ya mwisho inaanza.. wanalima na kupiga soga na saa kumi na moja hivi kazi imekwisha ya siku na kuanza msafara wa kurudi nyumbani. Well.. at least mama atakuwa anaelekea nyumbani wakati mzee inabidi apitie kwa "Mzee Salum"..

Mama akifika nyumbani watoto wameshatoka shule na wadogo wanahitaji kuogeshwa, mambo ya kusafisha safisha kuanza kuandaa chakula cha watoto cha jioni, n.k n.k watoto wanakula mama anabakia kusafisha vyombo - unajua tena haachi vyombo vichafu vilale. Mida mida mzee anarudi yuko njwii au ndio na hasira zake za kushindwa mchezo wa bao kwa Mzee Salum!

Anajikalisha na chakula kinaletwa, anakula kama ana wazimu. Mama anakuja kutoa vyombo kwenda kussafisha.. Wanaenda chumbani mzee anataka "kula kile chakula kingine". Mama pamoja na kuchoka inabidi akubali kumpa mtu chakula kile roho inatamani. Kesho yake mzunguko mwingine unaanza labda ukiwa na mabadiliko machache.

Mara kuna kikao cha "kilimo kwanza" baba peke yake anaenda kutoa maoni! Of course mama yuko nyumbani "anaanglaia watoto".
 
so swali hapa wababa tufanyaje ili kilimo kwanza kifanikiwe kwa ufanisi??????
labda gaga na wos waanze na ushauri......
 
duh..
huwa sichanganyikiwi kirahisi lakini leo mmefanikiwa kunichanganya;

Nini kimekuchanganya Mzee?

mwenyewe nimedandia treni kwa mbele nadhhani tunazungumzia zile kazi ambazo wanakijiji tunasifika kuzifanya yaani kulima udongo na kupanda mazao. Kwamba wanawake wanafanya kazi hizi sana ni ukweli wa muda mrefu, wanaume nao wanafanya kazi lakini in relation to overall work ya mwanammke ni wazi kuwa mwanammke anajikuta anafanya zaidi kwani.
.

Huoni mgawanyo wa kazi usio wa kuridhisha hupelekea Kilimo kwanza kutokufanikiwa?



Anajikalisha na chakula kinaletwa, anakula kama ana wazimu. Mama anakuja kutoa vyombo kwenda kussafisha.. Wanaenda chumbani mzee anataka "kula kile chakula kingine". Mama pamoja na kuchoka inabidi akubali kumpa mtu chakula kile roho inatamani. Kesho yake mzunguko mwingine unaanza labda ukiwa na mabadiliko machache.

Kwanini mama anamlisha mara mbilimbili?? Baba haoni mama kachoka?

Mara kuna kikao cha "kilimo kwanza" baba peke yake anaenda kutoa maoni! Of course mama yuko nyumbani "anaanglaia watoto"
.
Kwani kabla ya kwenda kikao cha kilimo kwanza, huyu baba asingeweza kufanya kikao kidogo na mkewe kwanza kujua hali halisi? Huoni ingeepusha kuonekana wa ajabu kujadili kitu ambacho mchango wake ni haba? Pengine mama angempa mawazo mazuri ya kuwasilisha kunako husika.

Asante kwa mchango wako.
 
so swali hapa wababa tufanyaje ili kilimo kwanza kifanikiwe kwa ufanisi??????
labda gaga na wos waanze na ushauri......
Mtumie vifaa vya kilimo kwanza ipasavyo, na msiwaachie sana wamama kazi za shambani maana at the end of the day matumbo yenu yanahitaji kula, sasa akishinda shambani nani ataandaa menu home?? na nyie siku hizi hamtaki menu za kitoto.. mtu ugali kama kangumi halafu eti mboga saba lol????
 
Back
Top Bottom