Taarifa ambayo imenifikia muda huu kutoka huko nchini Sudan jimbo la Darfur.Kuwa askari wawili wa jeshi la wananchi wa Tanzania wamekufa kwa kuzolewa na maji wakati wakivuka mto kwa kifaru na gari lingine la kivita. Askari hao kwa ujumla wao walikuwa wanne. Tukio hilo limetokea jana majira ya saa moja usiku na kwa bahati nzuri mmoja alipatikana akiwa taabani usiku huo. Wengine wawili miili yao imepatikana leo mchana na mwingine mwenye cheo cha Captain bado hajapatikana. Aliyepatikana hai anaendelea vizuri. Helcopter za Umoja wa mataifa bado zinaendelea na kazi ya kumtafuta huyo mmoja ambaye bado ni kitendawili cha aidha yu hai au ameshafariki. Utaratibu wa kusafirisha miili ya hao wawili kuja nyumbani zinafanyika na majinayao yatatangazwa baada ya ndugu na jamaa zao kujulishwa. Mungu alaze roho za marehemu mahali pema peponi. AMEN.