Wanajeshi wa Msumbiji wauawa na Wanamgambo

Wanajeshi wa Msumbiji wauawa na Wanamgambo

Kuna mambo mawili makubwa hapo lazima uyaelewe kwanini wanamgambo wa waasi wanaonekana Wana nguvu.

Mosi, jeshi la Msumbiji ni dhaifu kwa Sasa.
Pili, waasi wanashirikiana na raia huku wakiishi miongoni mwa raia wa kawaida hivyo wanaowafuatilia kirahisi jeshi la serikali bila kujulikana ni adui.

Hapo inatakiwa operesheni ya chini ya zuria nyumba kwa nyumba, sinagogi kwa sinagogi, unyama kwa unyama ....hapa nadhani umenielewa...
Hii kauli ya kusema jeshi la mzumbiji ni dhaifu mlianza kuitoa baada ya hili kundi kuteka vijiji na baadae bandari.
Sasa hebu tupe ufafanuzi jeshi hilo ni dhaifu kivipi wakati nchi yote imetulia isipokuwa hapo Cado Delgado?
Unasema wanamgambo wanajificha miongoni mwa raia kauli ambayo sio kweli! Wanamgambo hao wanaua raia wa maeneo wanayoyateka na kuwajumlisha kundini wale wanaokubali kuungana nao

Hebu fafanua ni vipi wanajificha kwa raia na ni vipi jeshi la Mozambique ni dhaifu. Tumeona kule Nigeria boko haram nao wanavamia maeneo ya raia na kukimbia, kwanini jeshi la Nigeria limeshindwa kuwamaliza boko haram wakati jeshi hilo sio dhaifu kama la mzumbiji? Siku wakiteka vijiji na wilaya huku kwetu mtaanza kusema jeshi letu ni dhaifu
 
Shida ya hao jamaa wanafanya ambush halafu wanapotea maporini humo.

Kwa hiyo kuwapata tena kwa jeshi kama la Msumbini bado sana na ukiangalia kisaikolojia jeshi na serikali ya Msumbiji hawajui wafanye nini yani kiufupi wamewashindwa.

Na hili kundi lisipoangaliwa vizuri litakuja kuwa tishio sana ukanda huu wa southern Africa maana kwenye chimbuko ambapo ni Msumbiji wamefanya uzembe uliopitiliza yani wanawapa attention ambayo hata hawastaili na hawa jamaa ukishawapa tu attention tayari umeharibu kila kitu na wakisambaa utakuta hata wanakuja kujitolea muanga Kariakoo Dsm, mfano ukiangalia ISIS wametapakaa IRAQ, SYRIA, LIBYA, ALGERIA na n.k, ukija West Africa kuna BOKO HARAM ambapo limetapakaa nchi kama NIGERIA, NIGER, CAMEROON, na CHAD. Kwa East Africa lilikuwa AL SHAABAB ila ndo hivyo Kenya walijitoa kweli kweli mwisho Southern Africa ndo hili sasa la Msumbiji

Nawapongeza Kenya kwa kweli kwenye kupigana na hawa wahuni, huwezi amini Kenya aliwafata mpaka huko huko Somalia, Tanzania tuliingia mpaka maporini kuwafata hawa watu mpaka wakapoteana yani inahitaji jeshi lenye nidhamu ya hali ya juu na kwa Askari anayejua anafanya nini sasa Askari wa Msumbiji anajiuliza mara mbili mbili kuingia front kwanni jamaa wasiwapige!

Shida hapa ni jeshi la Msumbiji ila mda bado wanao kabla halijawa janga zaidi na zaidi
 
Huko kulikuwa na watu wanaitwa Bandido, hao jamaa walikuwa hatari sana wakiingia kwenye kijiji ni balaaa, hawana viatu mguuni Serikali ya Msumbji iliwashindwa. nakumbuka tulipambana nao sana, japo tuliwashinda lakini watu wetu wengi walilala kaburini. Nadhani msumbiji ijiangalie namna inavyoongoza watu wake hasa kuhusu haki na usawa kiuchumi,kisiasa, ajira n.k
Hata kwetu kuna hali mbaya ya ubaguzi wa kisiasa ambapo kukitokea makundi ya namna hii yataungwa mkono kwa kiwango kikubwa
 
Shida ya hao jamaa wanafanya ambush halafu wanapotea maporini humo.

Kwa hiyo kuwapata tena kwa jeshi kama la Msumbini bado sana na ukiangalia kisaikolojia jeshi na serikali ya Msumbiji hawajui wafanye nini yani kiufupi wamewashindwa.

Na hili kundi lisipoangaliwa vizuri litakuja kuwa tishio sana ukanda huu wa southern Africa maana kwenye chimbuko ambapo ni Msumbiji wamefanya uzembe uliopitiliza yani wanawapa attention ambayo hata hawastaili na hawa jamaa ukishawapa tu attention tayari umeharibu kila kitu na wakisambaa utakuta hata wanakuja kujitolea muanga Kariakoo Dsm, mfano ukiangalia ISIS wametapakaa IRAQ, SYRIA, LIBYA, ALGERIA na n.k, ukija West Africa kuna BOKO HARAM ambapo limetapakaa nchi kama NIGERIA, NIGER, CAMEROON, na CHAD. Kwa East Africa lilikuwa AL SHAABAB ila ndo hivyo Kenya walijitoa kweli kweli mwisho Southern Africa ndo hili sasa la Msumbiji

Nawapongeza Kenya kwa kweli kwenye kupigana na hawa wahuni, huwezi amini Kenya aliwafata mpaka huko huko Somalia, Tanzania tuliingia mpaka maporini kuwafata hawa watu mpaka wakapoteana yani inahitaji jeshi lenye nidhamu ya hali ya juu na kwa Askari anayejua anafanya nini sasa Askari wa Msumbiji anajiuliza mara mbili mbili kuingia front kwanni jamaa wasiwapige!

Shida hapa ni jeshi la Msumbiji ila mda bado wanao kabla halijawa janga zaidi na zaidi
Acha uongo hao jamaa hawafanyi ambush na kukimbia bali wameweka ngome mkoa wa cado Delgado na bandari ya mkoa huo waliiteka na wanaiendesha wao.
Wanajeshi pamoja na serikali kwa ujumla walifurushwa eneo hilo na kila wakitaka kulikomboa wanaishia kupata hasara
 
Hii kauli ya kusema jeshi la mzumbiji ni dhaifu mlianza kuitoa baada ya hili kundi kuteka vijiji na baadae bandari.
Sasa hebu tupe ufafanuzi jeshi hilo ni dhaifu kivipi wakati nchi yote imetulia isipokuwa hapo Cado Delgado?
Unasema wanamgambo wanajificha miongoni mwa raia kauli ambayo sio kweli! Wanamgambo hao wanaua raia wa maeneo wanayoyateka na kuwajumlisha kundini wale wanaokubali kuungana nao

Hebu fafanua ni vipi wanajificha kwa raia na ni vipi jeshi la Mozambique ni dhaifu. Tumeona kule Nigeria boko haram nao wanavamia maeneo ya raia na kukimbia, kwanini jeshi la Nigeria limeshindwa kuwamaliza boko haram wakati jeshi hilo sio dhaifu kama la mzumbiji? Siku wakiteka vijiji na wilaya huku kwetu mtaanza kusema jeshi letu ni dhaifu
Hauhitaji kuwa na elimu ngazi ya shahada kujua jeshi la Msumbiji ni dhaifu..
Soma habari utaona wakienda kukodi vifaa na Askari toka nchi za nje.
Pili uimara wa jeshi ni pamoja na nidhamu, juzi tu umeona video za matukio ya ajabu wanafanya adharani.

Tatu, kuhusu Boko Haram na kwingineko au makundi mengine kama hayo shida kubwa utokea pale ukichelewa kuchukua hatua ngumu nilizo sema mwanzo za operesheni ya chini ya zuria tena kwa mtindo wa 'eye for an eye...'.
Kama vile nchi jirani na Msumbiji walivyofanikiwa.

Ipo mifano ya kufanikiwa kwa njia hiyo ambayo si vema kuielezea hapa.

Njia hizo ndizo zilimpa nguvu hata Saddam Hussein kutawala Iraq, ndizo zimewapa nguvu utawala wa kijeshi wa Misri miongo mingi.

Hizo ndiyo zimewapa nguvu Israel kubakia hai kama taifa.
Hizo ndiyo .....
 
Hivi unadhani hao jamaa wangekuwa wanajulikana walipo unadhani wangekuwa hai hadi sasa!

Hiyo bandari unayoisemea serikali imeshaichukua kwa kuwapiga hao vibaka!

NB: popote duniani hawa jamaa kujua wameweka kambi sehemu flani ni ngumu sana utasikia tu wapo jimbo flani lakini specific area hutajua ng'o.
Acha uongo hao jamaa hawafanyi ambush na kukimbia bali wameweka ngome mkoa wa cado Delgado na bandari ya mkoa huo waliiteka na wanaiendesha wao.
Wanajeshi pamoja na serikali kwa ujumla walifurushwa eneo hilo na kila wakitaka kulikomboa wanaishia kupata hasara
 
Hivi unadhani hao jamaa wangekuwa wanajulikana walipo unadhani wangekuwa hai hadi sasa!

Hiyo bandari unayoisemea serikari imeshaichukua kwa kuwapiga hao vibaka!

NB: popote duniani hawa jamaa kujua wameweka kambi sehemu flani ni ngumu sana utasikia tu wapo jimbo flani lakini specific area hutajua ng'o.
Mbona hii habari ya bandari kukombolewa sijaisikia mkuu wakati nipo macho kwenye vyombo vya kimataifa?
 
Hii kauli ya kusema jeshi la mzumbiji ni dhaifu mlianza kuitoa baada ya hili kundi kuteka vijiji na baadae bandari.
Sasa hebu tupe ufafanuzi jeshi hilo ni dhaifu kivipi wakati nchi yote imetulia isipokuwa hapo Cado Delgado?
Unasema wanamgambo wanajificha miongoni mwa raia kauli ambayo sio kweli! Wanamgambo hao wanaua raia wa maeneo wanayoyateka na kuwajumlisha kundini wale wanaokubali kuungana nao

Hebu fafanua ni vipi wanajificha kwa raia na ni vipi jeshi la Mozambique ni dhaifu. Tumeona kule Nigeria boko haram nao wanavamia maeneo ya raia na kukimbia, kwanini jeshi la Nigeria limeshindwa kuwamaliza boko haram wakati jeshi hilo sio dhaifu kama la mzumbiji? Siku wakiteka vijiji na wilaya huku kwetu mtaanza kusema jeshi letu ni dhaifu
Umewahi kujiuliza kwanini hao Boko Haram hawana nguvu sana maeneo ya kusini mwa Nigeria ambako hakuna watu wengi wa imani yao?
Au kwanini kusini kwa Msumbiji hawana nguvu?
 
Hauhitaji kuwa na elimu ngazi ya shahada kujua jeshi la Msumbiji ni dhaifu..
Soma habari utaona wakienda kukodi vifaa na Askari toka nchi za nje.
Pili uimara wa jeshi ni pamoja na nidhamu, juzi tu umeona video za matukio ya ajabu wanafanya adharani.

Tatu, kuhusu Boko Haram na kwingineko au makundi mengine kama hayo shida kubwa utokea pale ukichelewa kuchukua hatua ngumu nilizo sema mwanzo za operesheni ya chini ya zuria tena kwa mtindo wa 'eye for an eye...'.
Kama vile nchi jirani na Msumbiji walivyofanikiwa.

Ipo mifano ya kufanikiwa kea njia hiyo ambayo si vema kuielezea hapa.

Njia hizo ndizo zilimpa nguvu hata Saddam Hussein kutawala Iraq, ndizo zimewapa nguvu utawala wa kijeshi wa Misri miongo mingi.

Hizo ndiyo zimewapa nguvu Israel kubakia hai kama taifa.
Hizo ndiyo .....
Huyu jamaa kijana @wa jana hajui asemacho mtu akisema kuhusu jeshi kuwa dhaifu, Jeshi ni nidhamu na jeshi bila nidhamu ni dhaifu hata kama unamiliki f35 2000 ebu imagine Wanajeshi wa Msumbiji wanaingia Kwenye vilabu vya pombe kulewa wakiwa na silaha haya huo ni nini kama sio utovu wa nidhamu!

Jeshi lisipokuwa na nidhamu ina maana hata kwenye vita unaweza kumkatalia mkubwa kuingia front lakini kwa majeshi yenye nidhamu hutasikia kitu kama hicho
 
Maelezo yako nayakubali kwa asilimia 90.

Lakini kwenye suala la "Wanaolilia kuandamana" Ukisema amani, sisi hatuna amani ya ndani, tuna uoga. Uoga wetu ndio unatufanya tushindwe kuanzisha chokochoko.

Ulinzi upo, kuanzia ulinzi wa Raia na Mali zao hadi Mipaka ya nchi.

HAKUNA AMANI YA KWELI PASI NA HAKI.. HAKI NA AMANI HAVITENGANI ABADANI.
Una kiu ya kuandamana? Lissu si aliwaambieni muandamane ili kumsaidia kuvuruga nchi yetu,ulijitokeza?

Lakini piaa lissu alisema maandamano yake hayatakuwa na ukomo ,kama una hamu na maandamano we kaandamane tu,ila usishinikize wengine

Mpuuzi makubwa wewe
 
HAKUNA KITU KIGUMU KATIKA SUALA LA ULINZI NA USALAMA, HUSUSANI MKIINGIA KWENYE MEDANI YA MAPIGANO (VITA) KAMA KUPIGANA NA WATU WASIO NA SARE.

CHUKULIA MFANO, UKO ZAMU YA ULINZI KATIKATI YA JIJI LA ISLAMABAD, UNAPISHANA NA MZEE KAVALIA KANZU YAKE YA KUDARIZI, IMEMKAA HASWA ANAELEKEA YALIPO MADUKA NA MKUSANYIKO WA WATU. AKIFIKA PALE GHALFA KUNA TOKEA MLIPUKO, WANAKUFA RAIA 100, ASKARI 1 NA MUASI 1. HAPA VYOMBO VYA HABARI VIKITOA HABARI JESHI LINAONEKANA KAMA NI DHAIFU SANA LAKINI SIO KWELI.

WAASI WENGI HUWA HAWANA MAKAO MAALUM, NA HII HUZIDISHA UGUMU SANA WA KUPAMBANA NAO. WAO WANAO UWEZO WA KUISHAMBULIA KAMBI KWA SILAHA WAKIWA MBALI KWASABABU KAMBI NI WELL-DEFINED GEOGRAPHICALLY.. LAKINI PIA NI RAHISI WAO KUVAMIA MAKAZI YA WATU NA KUFANYA UNYAMA, WAKIJA HUJA KAMA WEMA MWISHO HUONDOKA KAMA MWEWE.

KUPAMBANA NA WASIOJULIKANA INAHITAJI JUHUDI NA INTEL KUBWA NA SIO KUWA TU NA SILAHA ZA KISASA.

MIMI NAAMINI, JESHI LA MSUMBIJI HALIJASHINDWA, NA IKITOKEA LIKASHINDWA, WATU WA MSAADA TUKO FITI.
 
Umewahi kujiuliza kwanini hao Boko Haram hawana nguvu sana maeneo ya kusini mwa Nigeria ambako hakuna watu wengi wa imani yao?
Au kwanini kusini kwa Msumbiji hawana nguvu?
Kumbe yawezekana wanakuwa na wapelelezi wao ambao kwa yale maeneo ambako kuna watu wa imani yao wapelelezi hao wanafanya kazi kwa urahisi zaidi
 
Una kiu ya kuandamana? Lissu si aliwaambieni muandamane ili kumsaidia kuvuruga nchi yetu,ulijitokeza?

Lakini piaa lissu alisema maandamano yake hayatakuwa na ukomo ,kama una hamu na maandamano we kaandamane tu,ila usishinikize wengine

Mpuuzi makubwa wewe
KHUMA TU WEWE[emoji41]
 
Kumbe yawezekana wanakuwa na wapelelezi wao ambao kwa yale maeneo ambako kuna watu wa imani yao wapelelezi hao wanafanya kazi kwa urahisi zaidi
Wanakuwa miongoni mwa raia, wanatua taarifa kwa wenzao kila kinachoendelea za askari wa serikali kuhusu mahali walipo.
Wanaojua sasa wanajeshi wanafanya nini.

Wanamgambo wanavaa nguo kama raia, wanaficha silaha majumbani mwa raia au nyumba za ibada za raia.

Wanatumia usafiri wa raia wa kawaida, wanapewa mahitaji yao muhimu na raia.

Wavae sare za kijeshi na kukaa kambi rasmi za kijeshi uone itakuwaje.

Ina maana hata wanapoteka eneo serikali inapotuma askari wao wanaambiwa na raia watoa taarifa kila hatua walipo Askari wa serikali. Waasi wanavaa kiraia kisha wanashambulia ghafla, wakishafanikisha kuwadhibiti Askari wa serikali wanavaa rasmi kanzu, kombati ya juu au suruali za kijeshi, na kuanika bunduki hadharani wanafanya propaganda online na kwenye media zingine.
 
Mbona Hata wa kwetu wanafyekwa tu sema mpambano unaendeleaj kimya kimya. Hata mme wa shagazi yangu amepangwa kwenda huko awamu inayofuata Sasa alikuwa anawaza ila Hana namna. Anasema walishapeleka vikosi Mara kadhaa majamaa yanafyekelea mbali
hao jamaa wasije tu wakapenya huku kwetu aisee
 
Back
Top Bottom