Wanajeshi wa Msumbiji wauawa na Wanamgambo

Wanajeshi wa Msumbiji wauawa na Wanamgambo

Analogia Malenga

Platinum Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,292
Reaction score
10,842
Wanajeshi 25 wa vikosi vya usalama Msumbiji wameuawa huku wengine 15 wakijeruhiwa baada ya kushambuliwa na wanamgambo wa Kiislamu katika kijiji cha Matambalale eneo la Muidumbe.

Kundi la maafisa wa kijeshi lilikuwa linashika doria eneo hilo wakati wa tukio Jumapili, kulingana na vyombo vya habari vya eneo.
Katika moja ya uvamizi, kanali na meja wamefariki dunia, vyanzo vimenukuu vyombo vya habari vya eneo.

Waathirika walikuwa sehemu ya kundi lililotumwa kuimarisha usalama baada mashambulizi ya wiki iliyopita ambapo nyumba zilichomwa moto na wakaazi kuuawa.
Msumbiji


Bado jeshi halijathibitisha au kukanusha taarifa hizo.
1606998546003.gif
1606998545963.gif

Mashambulizi ya miaka mitatu yamesababisha mauaji ya zaidi ya 2,000 na kusababisha wengine 500,000 kutoroka makazi yao katika eneo la Cabo Delgado, kulingana na takwimu rasmi.
 
hao jamaa wasije tu wakapenya huku kwetu aisee
Ndio lengo lao kuu hilo.

Kumbuka walianza mapango ya Amboni Tanga wakafurushwa na Mwamunyange. Walifyekwa kwelikweli.

Wakajikusanya tena Kibiti Pwani, Mabeyo akafanya yake ndipo wakakimbilia Msumbiji.

Sasa lengo lao sio Msumbiji. Ni hapa Tanzania huko ni kama sehemu ya kujipanga tu na wakakuta ulinzi dhaifu.

Naamini kwa kikao cha juzi hapa TROIKA siku zao zinakaribia kuanza kuhesabika.
 
Ndio lengo lao kuu hilo.

Kumbuka walianza mapango ya Amboni Tanga wakafurushwa na Mwamunyange. Walifyekwa kwelikweli.

Wakajikusanya tena Kibiti Pwani, Mabeyo akafanya yake ndipo wakakimbilia Msumbiji.

Sasa lengo lao sio Msumbiji. Ni hapa Tanzania huko ni kama sehemu ya kujipanga tu na wakakuta ulinzi dhaifu.

Naamini kwa kikao cha juzi hapa TROIKA siku zao zinakaribia kuanza kuhesabika.

Nilifika Amboni Caves kutalii. Yule muongozaji nikamuuliza humu ndipo walikuja magaidi? Akajibu hapana, ni sehemu nyingine mbali na hapa. Nikamwambia lakini taarifa zinasema walikuja Amboni, akasema ni kule karibu na Kenya. Nikajua jamaa anajibu kimahesabu ili asiharibu utalii
 
Ndio lengo lao kuu hilo.

Kumbuka walianza mapango ya Amboni Tanga wakafurushwa na Mwamunyange. Walifyekwa kwelikweli.

Wakajikusanya tena Kibiti Pwani, Mabeyo akafanya yake ndipo wakakimbilia Msumbiji.

Sasa lengo lao sio Msumbiji. Ni hapa Tanzania huko ni kama sehemu ya kujipanga tu na wakakuta ulinzi dhaifu.

Naamini kwa kikao cha juzi hapa TROIKA siku zao zinakaribia kuanza kuhesabika.
Mkuu hawa ni wale wa kibiti na Amboni kwani?
 
Imekuwa wimbo ninaoimba kila siku,namuomba Mungu wasije huku maana ulinzi wetu... ila MUNGU tu ndio anayetulinda.
Ulinzi wetu ukoje mkuu.

Tatizo wengi hatuoni kazi kubwa inayofanywa na vyombo vyetu vya ulinzi na usalama. Hawa watu tu kile kitendo cha kuvaa sare za majeshi husika na kuwa na vituo vyao vya kazi huo ni ulinzi tosha.

Hebu chukulia Rais atangaze leo "HAKUNA JESHI LOLOTE NIMEFUTA KUANZIA JESHI LA WANANCHI HADI MGAMBO, KILA AJILINDE YEYE NA MALI ZAKE". Hapo sasa ndio utajua umuhimu wa vyombo hivyo. Kwanza vibaka wote watajaa nyumbani kwako hakuna cha fensi ya umeme wala nini. Wanawake watabakwa hadharani mbele za watu, mitaa itatawaliwa na mateja na majambazi yatashika hatamu, hakuna mtu anaweza kufanya biashara, mabenki yatafungwa. Hata hao wanaolilia kuandamana hawataweza kwani wanaandamana kwa kuwa kuna amani.

Kwa hiyo, kile kitendo tu cha kusema POLISI, tayari inaleta picha fulani kichwani mwa mtu kuhusu usalama na udhibiti wa uharifu.

Jeshi letu ni imara na ndiyo maana liliwadhibiti hao washenzi pale Amboni na Kibiti wakakimbilia huko Copa Delgado Msumbiji
 
Hao jamaa wanavaa ndala lakini moto wao ni nyoko!
Wanajeshi na mafunzo yao, vifaa vyao, magari yao na intellijensia yao wanafyekwa kirahisi namna hiyo?
Kuna mambo mawili makubwa hapo lazima uyaelewe kwanini wanamgambo wa waasi wanaonekana Wana nguvu.

Mosi, jeshi la Msumbiji ni dhaifu kwa Sasa.
Pili, waasi wanashirikiana na raia huku wakiishi miongoni mwa raia wa kawaida hivyo wanawafuatilia kirahisi jeshi la serikali bila kujulikana ni adui.

Hapo inatakiwa operesheni ya chini ya zuria nyumba kwa nyumba, sinagogi kwa sinagogi, unyama kwa unyama ....hapa nadhani umenielewa...
 
Nilifika Amboni Caves kutalii. Yule muongozaji nikamuuliza humu ndipo walikuja magaidi? Akajibu hapana, ni sehemu nyingine mbali na hapa. Nikamwambia lakini taarifa zinasema walikuja Amboni, akasema ni kule karibu na Kenya. Nikajua jamaa anajibu kimahesabu ili asiharibu utalii
Ni kweli mkuu, walikuwa mwambao wa Kenya huko mlipokuwa walikuwa wanaambaa kufuata mahitaji kwa wanananchi na kwenda hadi Tanga mjini. Aisee walikiona kilichomtoa Kanga manyoya shingoni.

Wengine walijaribu kujikusanya pori la Udzungwa maeneo ya Kidatu, usiombee njaa bhana si wakashuka na wananchi wakawashtukia wakatiwa mbaroni.

Kwa ujumla hawa watu ni shida sana.
 
Ulinzi wetu ukoje mkuu.

Tatizo wengi hatuoni kazi kubwa inayofanywa na vyombo vyetu vya ulinzi na usalama. Hawa watu tu kile kitendo cha kuvaa sare za majeshi husika na kuwa na vituo vyao vya kazi huo ni ulinzi tosha.

Hebu chukulia Rais atangaze leo "HAKUNA JESHI LOLOTE NIMEFUTA KUANZIA JESHI LA WANANCHI HADI MGAMBO, KILA AJILINDE YEYE NA MALI ZAKE". Hapo sasa ndio utajua umuhimu wa vyombo hivyo. Kwanza vibaka wote watajaa nyumbani kwako hakuna cha fensi ya umeme wala nini. Wanawake watabakwa hadharani mbele za watu, mitaa itatawaliwa na mateja na majambazi yatashika hatamu, hakuna mtu anaweza kufanya biashara, mabenki yatafungwa. Hata hao wanaolilia kuandamana hawataweza kwani wanaandamana kwa kuwa kuna amani.

Kwa hiyo, kile kitendo tu cha kusema POLISI, tayari inaleta picha fulani kichwani mwa mtu kuhusu usalama na udhibiti wa uharifu.

Jeshi letu ni imara na ndiyo maana liliwadhibiti hao washenzi pale Amboni na Kibiti wakakimbilia huko Copa Delgado Msumbiji
Maelezo yako nayakubali kwa asilimia 90.

Lakini kwenye suala la "Wanaolilia kuandamana" Ukisema amani, sisi hatuna amani ya ndani, tuna uoga. Uoga wetu ndio unatufanya tushindwe kuanzisha chokochoko.

Ulinzi upo, kuanzia ulinzi wa Raia na Mali zao hadi Mipaka ya nchi.

HAKUNA AMANI YA KWELI PASI NA HAKI.. HAKI NA AMANI HAVITENGANI ABADANI.
 
Hao jamaa wanavaa ndala lakini moto wao ni nyoko!
Wanajeshi na mafunzo yao, vifaa vyao, magari yao na intellijensia yao wanafyekwa kirahisi namna hiyo?
Huko kulikuwa na watu wanaitwa Bandido, hao jamaa walikuwa hatari sana wakiingia kwenye kijiji ni balaaa, hawana viatu mguuni Serikali ya Msumbji iliwashindwa. nakumbuka tulipambana nao sana, japo tuliwashinda lakini watu wetu wengi walilala kaburini. Nadhani msumbiji ijiangalie namna inavyoongoza watu wake hasa kuhusu haki na usawa kiuchumi,kisiasa, ajira n.k
 
Kuna mambo mawili makubwa hapo lazima uyaelewe kwanini wanamgambo wa waasi wanaonekana Wana nguvu.

Mosi, jeshi la Msumbiji ni dhaifu kwa Sasa.
Pili, waasi wanashirikiana na raia huku wakiishi miongoni mwa raia wa kawaida hivyo wanaowafuatilia kirahisi jeshi la serikali bila kujulikana ni adui.

Hapo inatakiwa operesheni ya chini ya zuria nyumba kwa nyumba, sinagogi kwa sinagogi, unyama kwa unyama ....hapa nadhani umenielewa...
There you are, you nailed it. Ukitaka wengi wapone inabidi hizo hatua mbili hapo zizingatiwe. Hasa hiyo namba mbili kwani hata kama utakuwa na kikosi imara namna gani hauwezi kushinda.

Kumbuka kwa mfano, yale magaidi ya Westgate pale Kenya mara baada ya kufanya unyama, yalijibadili na kuwa raia wanaohitaji kuokolewa na yakatoka salama kabisa kwenye mstari wa wahanga. Imposters au mapandikizi ni adui namba moja na mbaya sana
 
Back
Top Bottom