Wanairaimba: Dkt. Mwigulu hatununuliagi hata pombe

Kuna hotuba ya kaburu wa Africa kusini, yule rais wa pili kutoka mwisho wa Makaburu, alisema sie watu weusi tunawezaga kucheza ngoma, kua na wanawake wengi, kunywa pombe; akaendelea zaidi kwamba mtu mweusi mwenye akili sana anauwezo wa ku plan jambo kwa miezi 12 tu, hakuna mwenye uwezo wa zaidi ya hapo. Ni matusi kwetu lakini sasa ukisoma ujumbe hu wa wana Iramba, hivi yule Kaburu unamkatalia wapi? Simkubali sana Mwigulu, lakini hoja yao mbona ipo shallow namna hiyo? Yaani mtu awanunulie pombe baasi then? Mi nilidhani kwakua kijana wao kwa sasa ni waziri wa fedha, wangeanza kufanya robbing ili wapate maji, biashara ya vitunguu waanze kuvisafirisha kwenda nje, wawe na maisha mazuri ili iwashawishi hata vijana wao waliopo mjini watamani kurudi nyumbani wakiwa likizo, mabinti zao waache kuchukuliwa kwenda kuuza bar Mwanza, Arusha, Dodoma nk; wao wanataka kununuliwa pombe, wanataka akija wanywe nae pombe? Tumelogwa sisi, sio siri
 
Baada ya kuwa Mwanza kwa takriban miezi mitatu, juma lililopita nikarejea na kuamua kukusanya ndengu Jimbo la Iramba na hivyo kunilazimu kutembelea vijiji ambavyo wanalima ndengu.

Ndengu ni mojawapo ya zao tunalolima sana Iramba, ukiacha alzeti na zamani vitunguu.

Katika pitapita zangu huko na kuulizia wajihi na umuhimu wa Mbunge wetu wa sasa Dr. Mwigulu. Kwa sasa anatajwa kwa kutokuwa na tabia ya ukarimu kama watangulizi wake akina Shango na Kiula.

Juma Kilimba amabye kwa sasa ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa alikuwa ni mtaalamu wa kuhonga lakini hakuwa mkarimu na ndiyo maana ilipofika 2010 alishindwa kiurahis sana na Dk. Mwigulu.

WanaIramba wanadai Mzee Shango alikuwa akiwakuta kwenye klabu anakaa nao na anawanunulia pombe yote pale kwenye Klabu wanainywa wanafurahi na wanaendelea na maisha yao.

Shango na Mzee kiula ndiyo tabia zao zilikuwa zinalandana ingawa Shango alikuwa mkarimu kwa watu wa namna zote.

Upande wa Mwigulu wanadai anajidai sana. Akifika msibani anabaki kwenye gari mpaka aongozwe kushuka na Mlinzi/Msaidizi wake. Kula hivyo hivyo mpaka Mlinzi wake atangulie kula ndiyo naye ale.

Dkt. Mwigulu hatoi fedha kiholela na inaonesha anadaharau sana maisha yao - wakiwa wanakunywa pombe Klabuni anapita tu na ligari lake na kuna wakati aliwahi kuwatimulia vumbi. Wao wanadai kama hanywi angeshuka tu basi anagalau awasalimie na kuwanunulia pombe awaache waendelee kwa furaha zao.

Shango hakuwa mnywaji lakini alikuwa anachukua jagi anazuga kama naye kanywa kwa kuweka mdomoni ilimradi tu achanganyike nao. Sasa Dk. Mwigulu kama yupo hivyo je akija kuwa Rais si ndiyo atakuwa anaishia Singida mjini.
Wanyiramba mtaendelea kuwa masikini sn sababu ya Mwigulu
 
Kuna hotuba ya kaburu wa Africa kusini, yule rais wa pili kutoka mwisho wa Makaburu, alisema sie watu weusi tunawezaga kucheza ngoma, kua na wanawake wengi, kunywa pombe; akaendelea zaidi kwamba mtu mweusi mwenye akili sana anauwezo wa ku plan jambo kwa miezi 12 tu, hakuna mwenye uwezo wa zaidi ya hapo. Ni matusi kwetu lakini sasa ukisoma ujumbe hu wa wana Iramba, hivi yule Kaburu unamkatalia wapi? Simkubali sana Mwigulu, lakini hoja yao mbona ipo shallow namna hiyo? Yaani mtu awanunulie pombe baasi then? Mi nilidhani kwakua kijana wao kwa sasa ni waziri wa fedha, wangeanza kufanya robbing ili wapate maji, biashara ya vitunguu waanze kuvisafirisha kwenda nje, wawe na maisha mazuri ili iwashawishi hata vijana wao waliopo mjini watamani kurudi nyumbani wakiwa likizo, mabinti zao waache kuchukuliwa kwenda kuuza bar Mwanza, Arusha, Dodoma nk; wao wanataka kununuliwa pombe, wanataka akija wanywe nae pombe? Tumelogwa sisi, sio siri
Ndiyo maana Iramba imejaa nyumba za tembe
 
Ndiyo maana Singida huko kumedumaa,kama akili zenywewe ndiyo hizi,bado sana kama kujunuliwa Pombe ni hitaji la msingi,basi kina Mwigulu watatawala milele maana wanaongoza vilaza sana
 
Huu ni ujinga, na hao wapumbavu wanao omba pombe badala ya mambo muhimu kwa maendeleo ya maisha yao.
Ndio Wapiga kura hao, unafikiri wenye uwezo wa kuhoji ya msingi wakiingia site tutakuwa na Wabunge hawa?.

Hapo wamesahau tu kuulizia Tshirt na Kofia...au huenda hizo walizipata.
 
Back
Top Bottom