Wanahitajika business partners

Wanahitajika business partners

Mateja M.G Yango

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2013
Posts
613
Reaction score
1,097
COMPANY NAME: MUGETA FARMS
TRADEMARK/BRAND NAME: VICTORIA FINEST

KUHUSU BIASHARA:
Mugeta Farms co. ltd ni kampuni changa (startup company), kwa sasa inajihusisha na value addition ya dagaa, refer picha zilizoambatanishwa. Tuna-operate kutokea Mwanza, japo mauzo makubwa tunafanyia DSM. Nature ya biashara yetu inatulazimu kuuza bibdhaa kwenye supermarkets on credit basis, ambapo huchukua siku 30 hadi 60 kuweza lipwa.

MAHITAJI:
Tunanuia kupata project partners wataosaidia tuweze zalisha bidhaa ya kutosha, tukaiingiza sokoni, tukakusanya malipo, baada ya hapo ni makubaliono either ela irudi kwenye cycle ya uzalishaji au partner alipwe ela yake na faida yake. Kwa sasa tunahitaji ku-raise in total 10mil, Kiwango cha chini kikiwa TSh 500,000/=.

Ikumbukwe kwamba hii sio ununuzi wa hisa, bali ni pre-financing ya operations zetu which includes production, distribution & collection of funds. Bidhaa yetu ina increment ya bei kwa wateja wa jumla (mini markets & supermarkets) tunapokuwa tunawauzia bidhaa on credit basis. Mfano, Kama tunakuuzia kwa jumla on cash basis kwa TSh 3,500/=, on credit basis tutakuuzia kwa TSh 4,000/=. Tofauti hapo ni TSh 500/=, around 15%, na hii ndio profit utayopata mwekezaji. 15% profit in 60 days.

UBORA WA BIDHAA:
Naweza sema kwa sasa dagaa wetu ndio dagaa bora kabisa unaoweza pata kwenye supermarkets and mini-markets.
1. Hawana michanga kabisa, 100% guarantee.
2. Wana radha ya kuvutia sana, Wamekaangwa kwa mafuta masafi, Plus wamechanganywa na limao, tangawizi, chumvi na kitunguu saumu.
3. Wametengenezwa kwenye mazingira masafi.
4. Package yake ni safi sana compared to the rest in the market.

Tayari kuna outlets zaidi ya 50 kwa dsm pekee ambazo tayari tushaanza peleka mzigo, with enough funds tunataka fikisha outlests zaidi ya 400 kwa dsm pekee ifikapo december 2018, pia mzigo unasambazwa Kilimanjaro, Arusha na Dodoma. Japo distribution concentration kwa sasa ipo dsm, tuta replicate tunachokifanya kwa dsm kwa mikoa mingine pia muda muafaka utapofika.


Kama upo interested unaweza nipigia kwa namba 0713752285 au 0767777491. Pia unaweza tuma message whats app 0713752285 na email mateja@mugetafarms.com (Contact Name: Mateja Mugeta Geriga Yango)

Unaweza uliza maswali yako hapa pia, japo mengine ntalazimika kuyajibu in private, maana si kila kitu kuhusu biashara kinatakiwa kuwekwa hadharani.

Detailed information can be shared to your email.
Thanks.


32558005_1668055679896718_1376982178843328512_n (1).jpg


FB_IMG_1520182974161.jpg


20180420_130313.jpg
 
Boss nimependa wazo,nataka kujua yafuatayo,kwanza je utaraibu ukoje,tunaingia mkataba wa aina gani?Kwa sababu sio hisa je ni mkopo?Je meme nitakuwa mechandiser kwenye maduka kwa maana kwamba nitaingia mkataba na duka na supermarkets kisha ninyi mnapeleka mzigo supermarket ikishathibitisha imepokea mzigo mimi nawalipa ninyi cash kisha nasubiri baada ya 60 days napokea malipo plus profit ama inakuwaje?Nalipa wakati gani?
 
Supermarket zote mzigo unapatikana?
Si supermarket zote, baadhi unaweza pata mzigo, kwa mfano unaweza kwenda A-Z Supermarket ya posta, Imalaseko Supermarket ya Dar free market, na mini markets nyingi bagamoyo za bagamoyo road na tabata. Bado tuna jukumu la kufikia zaidi ya outlets 350 kwa dsm pekee kabla mwaka haujaisha, cash-flow is an issue, ndio maana kwa sasa tunataka source cash kutoka kwa watu wengine kwa kipindi kifupi kipindi tunaangalia long term solutions.
 
FACTS:
Dagaa inachukuatakribani 70% ya samaki wote wanaovuliwa toka Ziwa Victoria, which is around 130,000/= to 160,000/= tons annually.
Kwa hesabu za haraka haraka kwa bei ya un-processed dagaa ya sh 8,000,000/= kwa tani, mzunguko wa dagaa unazalisha kati ya 1 to 1.3 trillion kwa mwaka. mzunguko huu ni wa un-processed product. Ambapo kuna nchi kama Zambia, Congo, Malawi, Kenya, Rwanda na Burundi ni wanunuzi wazuri tu wa dagaa toka ziwa Victoria.
 
Si supermarket zote, baadhi unaweza pata mzigo, kwa mfano unaweza kwenda A-Z Supermarket ya posta, Imalaseko Supermarket ya Dar free market, na mini markets nyingi bagamoyo za bagamoyo road na tabata. Bado tuna jukumu la kufikia zaidi ya outlets 350 kwa dsm pekee kabla mwaka haujaisha, cash-flow is an issue, ndio maana kwa sasa tunataka source cash kutoka kwa watu wengine kwa kipindi kifupi kipindi tunaangalia long term solutions.
Mkuu nimeuliza terms za malipo,nikitaka kuwekeza nalipa kwenu kabla ya mazigo au namlipia mwenye supamaketi deni upfront baada ya nyinyi kumpa mzigo?
 
Mkuu nimeuliza terms za malipo,nikitaka kuwekeza nalipa kwenu kabla ya mazigo au namlipia mwenye supamaketi deni upfront baada ya nyinyi kumpa mzigo?
Unalipa kwetu mzigo.
Tunachoweza share nawe ni weekly production vs sales report.
 
Dagaa ni dagaa tu hata ukiwapack vipi.But nimependa idea yenu
 
FACTS:
Uvuvi wa Dagaa mostly hufanyika siku 14 katika mwezi, hizi ni zile siku za giza. Mwezi una siku 14 za mbalamwezi na siku 14 za giza. Uvuvi wa dagaa hutegemea mvuto wa mwanga (light attraction), hivyo kwa kutumia taa ni rahisi kufanya uvuvi wa dagaa wakati wa giza sababu taa itamulika zaidi, wakati wa mbalamwezi, intensity ya illumination inakuwa ndogo. Japo baadhi ya wavuvi huendelea vua wakati wa mbalamwezi, wakivuacho huwa kidogo in quantity.
 
Dagaa ni dagaa tu hata ukiwapack vipi.But nimependa idea yenu
Karibu sana ndugu dagaa ni dagaa tu. Tunachofanya sisi ni value addition na usafi wa bidhaa kabla haijakufikia wewe mtumiaji wa mwisho.
Almost 100% ya dagaa wanaoletwa mjini wanaanikwa chini kwenye michanga, tofauti na sisi wachache tunaoanika kwenye chanja ambao we are almost negligible kwenye biashara ya dagaa, we are dealing with very small quantities.

Pia kuwakaanga dagaa wakiwa wabichi husababisha dagaa kutokuwa na radha ya uchachu.
 
Mbona inaeleweka, umesema sio hisa ni partnership, swali langu partner unayemuhitaji awe na pesa kihasi gani??.
kuanzia laki 5 na kuendelea, kama nilivyosema, in this cycle inahitajika 10mil pekee ku-boost cash flow.
Karibu sana boss.
 
Back
Top Bottom