SolarPower
JF-Expert Member
- Jan 17, 2011
- 223
- 27
Wakuu,
Hali ya ujuzi wa Hisabati kwa vijana wetu inatisha. Hali ni mbaya sana kwa ngazi zote hasa kwa shule ya Msingi na Sekondari. Kwa mfano zaidi ya asilimia 65 ya vijana wanaochaguliwa kuingia kidato cha kwanza huwa wamefeli Hisabati. Kwa upande wa Sekondari, zaidi ya asilimia 85 hupata F katika mtihani wao wa mwisho wa kumaliza kidato cha nne.
Kama moja ya mchango wetu katika kukabiliana na tatizo hili, napendekeza wale wajuzi na magwiji wa Hisabati wajitokeze na tuanzishe taasisi maalum ambayo inapendekezwa ijulikane kama WANAHISABATI WA KUJITOLEA (WAHIKU). kazi kubwa ya taasisi hii itakuwa ni kufanya utafiti na kubaini tatizo linalowakabili vijana wetu na walimu wao katika Hisabati na kisha kubuni na kutengeneza mikakati maalum ya utekelezaji kwa kushirikiana na wizara husika, Chama cha Hisabati Tanzania na Chama cha Walimu Tanzania na Halmashauri zetu.
Bila msingi mzuri wa Hisabati kwa vijana wetu Tanzania itaendelea kubaki nyuma katika nyanja ya maendeleo------HISABATI KWANZA.........
Hali ya ujuzi wa Hisabati kwa vijana wetu inatisha. Hali ni mbaya sana kwa ngazi zote hasa kwa shule ya Msingi na Sekondari. Kwa mfano zaidi ya asilimia 65 ya vijana wanaochaguliwa kuingia kidato cha kwanza huwa wamefeli Hisabati. Kwa upande wa Sekondari, zaidi ya asilimia 85 hupata F katika mtihani wao wa mwisho wa kumaliza kidato cha nne.
Kama moja ya mchango wetu katika kukabiliana na tatizo hili, napendekeza wale wajuzi na magwiji wa Hisabati wajitokeze na tuanzishe taasisi maalum ambayo inapendekezwa ijulikane kama WANAHISABATI WA KUJITOLEA (WAHIKU). kazi kubwa ya taasisi hii itakuwa ni kufanya utafiti na kubaini tatizo linalowakabili vijana wetu na walimu wao katika Hisabati na kisha kubuni na kutengeneza mikakati maalum ya utekelezaji kwa kushirikiana na wizara husika, Chama cha Hisabati Tanzania na Chama cha Walimu Tanzania na Halmashauri zetu.
Bila msingi mzuri wa Hisabati kwa vijana wetu Tanzania itaendelea kubaki nyuma katika nyanja ya maendeleo------HISABATI KWANZA.........