Wanafunzi waliochaguliwa kidato cha kwanza kufanya mtihani mwingine

mimi wasiwasi wangu ni sehemu Mbili,moja kuna baadhi ya watoto na wazazi wao wanalazimishwa tu kwenda sekondari sasa wakipata fursa hii ndo watafurahi kwani mwanafunzi ataamua kufanya vibaya ili asiendelee na masomo.Pili wazazi waliojibana mpaka kupata mahitaji ya mtoto je watafidiwaje kwa sababu sio kosa lao wao walitii amri ya kupeleka watoto shule,
Mkuu, Mimi nimesoma haka kauzi kote. Ila hii hoja imenigusa sana. Mwanangu namjua uwezo wake. Lakini nikaambiwa lazima apelekwe sekondari (vipaji). Nimempeleka. Leo akirudishwa nani atarudisha kasenti kangu, manake nilitumia kama kilo saba hv ambayo sikuwahi kushika yangu nizaliwe.
 
Bora wenzetu wakenya mitihani yao primary inaheshimika sana bila slip result ya class eight, huwezi pokelewa shule yoyote ya secondary, public ama privet. Na la pili hakuna mambo ya usahili wa kuingia form one, maana yake nini basi? Ni kwamba mtihani wa taifa ni kipimo kinachoaminika kitaifa. Mtoto anapotafutiwa shule matokeo yake ya claas seven yawe kipimo, tunapoteza pesa nyingi kufanya usahili sehemu mbalimbali. Ni mtazamo wangu
 
Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) limesema kuwa wanafunzi ambao walichaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika shule za serikali nchini wanahitajika kufanya mtihani wa udahili tarehe 28 mwezi huu na wale watakaofaulu wataruhusiwa kujiunga na kidato hicho.
Taarifa hii ilitolewa kwa mara ya kwanza na Katibu Mkuu wa Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA), Dkt. Charles Msonde lakini kwa mujibu wa barua kutoka NECTA iliyosainiwa na Edgar Kasuga kwa niaba ya Katibu Mkuu kwenda kwa Makatibu Tawala wote wa Tanzania Bara siku ya Jumatatu, wale ambao hawatafaulu hawataruhusiwa kuendelea na masomo hayo ya sekondari.
NECTA inakusudia kutumia mtihani huo kuhakiki uwezo wa wanafunzi waliounesha katika kiwango chao cha ufaulu katika Mtihani wa Taifa wa Kumaliza Elimu ya Msingi uliofanyika mwaka jana. “Watakaofeli hawataruhusiwa kuendelea na masomo,” inasomeka sehemu ya barua hiyo. Makatibu Tawala wote, maafisa elimu na walimu wakuu wote wa shule za sekondari za serikali waliombwa kufikia leo wawe wamewasilisha orodha ya majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na shule zao ili maandalizi yafanyike.
Afisa mmoja wa NECTA amesema maandalizi kwa ajili ya mtihani huo yanaendelea na kwamba wanafunzi wajiandae. “Maandalizi yanaendelea vizuri na tutatoa taarifa kwa umma kuhusu mabadiliko yoyote yatakayojitokeza,” alisema.
Katika Mtihani wa Taifa wa Kumaliza Elimu ya Msingi uliofanyika mwaka jana, watoto 789,479 waliofanya mtihani huo ambapo wanafunzi 555,291 walifaulu. Idadi hii ya waliofaulu ni sawa na asilimia 70 ya wanafunzi wote waliofanya mtihani huo.
HT: THE CITIZEN
 
Hapa sipati mantiki yake, ni kama vile baraza haliwaamini waliosimamia mitihani ya drs la saba au wasahishaji. Mi nadhani, wangeongeza tu ufanisi ktk usimamizi wa mitihani.
 
Hili ndilo tatizo la mitihani ya kichagua!
Mwanafunzi anabahatisha kuchagua majibu sahihi anapata alama 243, anapangiwa Mzumbe, Kilakala, Ama Msalato!! Anapewa mtihani wa ndani anapata alama 43!
===
Naunga mkono hoja, ila lazima serikali iwafidie gharama zote na fidia juu wazazi na walezi walioangaika kupeleka wanafunzi kwenye shule hizo.
 
Hapa sipati mantiki yake, ni kama vile baraza haliwaamini waliosimamia mitihani ya drs la saba au wasahishaji. Mi nadhani, wangeongeza tu ufanisi ktk usimamizi wa mitihani.
Wewe una waamini mkuu?
 
Kama wabovu walifaulu vipi hiyo mitihani ya necta?
Kumbuka siku za karibuni Ndalichako alizuia Shule binafsi(private schools) kuwafanyisha mitihani ya mchujo wanafunzi wanaokwenda kusoma private schools, sasa hiki kinachotaka kufanywa na necta(serikali) kina tofauti gani na kile kilichokua kikifanywa na Shule binafsi?

Na vipi kuhusu wataofeli huo mtihani watapelekwa wapi sasa?
Hii serikali ya kutafuta kiki sana hii
Mkuu umeongea point yangu heshima kwako nakupa dah kibaya ni kwamba mtoto amekaa miezi yote ndo ameanza kusoma mambo mapya halafu umpe mtihani wa la saba
 
Wewe una waamini mkuu?
Siwaamini sana, ila njia bora nadhani ingekuwa kuiimarisha taasisi hisika si kuwafanyisha mtihani upya. Hata kwa muda waliokaa mtaaani laweza kuwa ni shida kwa wale waliokuwa zima moto.

Lakini vipi kwa wazazi na walezi waliokwisha fanya maandalizi yao? Kwani Mkuu, hakuna possibility la mtu kufaulu mtihani huu na akafeli ule?

Cha msingi hapa, kwakuwa wote ni watoto wa baba mmoja, nadhani suluhisho lilitakiwa ni kuimarisha taasisi husika tu. Watoto wapokee elimu bora, mitihani isimamiwe vyema, watakaofaulu wafaulu kweli.

Ila mi si muumini wa kipimo hiki cha mitihani ya kitaifa ya siku kadhaa kuwa ndicho kipimo cha mchujo kwa watahiniwa. Ubuniwe mfumo mpya, tumewaacha wengi bora kwa kigezo tu walifeli mitihani yao ya masaa kadhaa.
 
Kwa hiyo siku hizi ukifaulu paper hamna kuangusha shangwe,unakausha kwanza miezi kadhaa maana unaweza kuja kuumbuliwa na paper LA mchujo
 
Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) limesema kuwa
wanafunzi ambao walichaguliwa kujiunga na kidato
cha kwanza katika shule za serikali nchini wanahitajika
kufanya mtihani wa udahili tarehe 28 mwezi huu na
wale watakaofaulu wataruhusiwa kujiunga na kidato
hicho.
Taarifa hii ilitolewa kwa mara ya kwanza na Katibu
Mkuu wa Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA), Dkt.
Charles Msonde lakini kwa mujibu wa barua kutoka
NECTA iliyosainiwa na Edgar Kasuga kwa niaba ya
Katibu Mkuu kwenda kwa Makatibu Tawala wote wa
Tanzania Bara siku ya Jumatatu, wale ambao
hawatafaulu hawataruhusiwa kuendelea na masomo
hayo ya sekondari.
NECTA inakusudia kutumia mtihani huo kuhakiki
uwezo wa wanafunzi waliounesha katika kiwango chao
cha ufaulu katika Mtihani wa Taifa wa Kumaliza Elimu
ya Msingi uliofanyika mwaka jana. “Watakaofeli
hawataruhusiwa kuendelea na masomo,” inasomeka
sehemu ya barua hiyo. Makatibu Tawala wote, maafisa
elimu na walimu wakuu wote wa shule za sekondari za
serikali waliombwa kufikia leo wawe wamewasilisha
orodha ya majina ya wanafunzi waliochaguliwa
kujiunga na shule zao ili maandalizi yafanyike.
Afisa mmoja wa NECTA amesema maandalizi kwa ajili
ya mtihani huo yanaendelea na kwamba wanafunzi
wajiandae. “Maandalizi yanaendelea vizuri na tutatoa
taarifa kwa umma kuhusu mabadiliko yoyote
yatakayojitokeza,” alisema.
Katika Mtihani wa Taifa wa Kumaliza Elimu ya Msingi
uliofanyika mwaka jana, watoto 789,479 waliofanya
mtihani huo ambapo wanafunzi 555,291 walifaulu. Idadi
hii ya waliofaulu ni sawa na asilimia 70 ya wanafunzi
wote waliofanya mtihani huo.
Nina Imani Kama wako siriaz na paper itafanyika kwa Usimamizi makini ni wanafunzi laki moja tu watapata nafasi ya kuendelea wengine wote watafeli vibaya sanaaa
 
umuhimu wa kukarabati MTUMBWI, kuziba matobo ya kuokoa shehena ndio muhimu, sio kuupaka rangi ya kupendezesha macho
 
Hawa watu hawaeleweki as if wanafanya kazi bila kujiekewa.
Juzi tu wamesema elimu ya msingi itaishia kidato cha nne...sasa kwa nini leo mzuie watoto kupata elimu ya msingi
 
watarudishiwa pesa zao za michango na ada walizokwisha toa?au ni njia mbadala ya kuongeza pato la taifa!
 
Unachezea billion18 kila mwezi we we? na makusanyo ya kodi yameshukaaaaa?
Zalima zibuniwe mbinu mbadala.
 
Bora wafanye hvo juzi Form ID nmegundua wanafunzi wawili wa kike hawajui kusoma, na hii ni kawaida kila mwaka ..
 
Back
Top Bottom