Wanafunzi wa vyuo vikuu mkue jamani acheni utoto!!!

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,956
22,148
akuna serikali isiyo na matatizo na pengine kwa afrika mashariki tanzania inaongoza kila sekta
kwa upande wa elimu bomu kubwa limeangukiwa wizara hii pale walipopewa bomu lililoishinda wizara ya miundo mbinu na saasa limeamia elimu

Ok nije kwenye mada hapo juu..ndugu wapendwa ni kweli waweza kusema chuo kimevamiwa na watoto walio na umri mdogo sana ndio maana hata humu jf wanamizaha kupita uko nyuma

embu jiulize wanataka nauli ipunguzwe iwe 250

kule dom wanataka kila mwanafunzi awe na laptop

wapi utapata hili ndugu zanguni kuweni makini na migomo ya kijinga muulizen zito awape njia za migomo kudai haki zenu mpaka
 
kaka mie nakuunga mkono. mie siku ile nisikie eti wanafunzi wa UDOM wamegoma kisa laptop nilijiuliza sana na sikupata jibu aina ya wanavyuo tulio nao sasa ktk vyuo vyetu. Kitu kingine wamekuwa marimbukeni wa siasa na kuchotwa kiurahisi na wanasiasa bila kujijua kuwa wanatumika kama vile mtu anavyoitumia Jojo.Hali hii ya kutumiwa huwapelekea wao kujisahau malengo yao ya kuwepo chuoni na kusahau umuhimu wao na elimu yao ktk familia zao.
 
nakuunga mkono kaka, lakini cha kuzingatia hapa ni kwamba wanafunzi watendewew haki pale wanapostahili, mfano wanafunzi wa Udom college ya Informatics katika kipindi cha nyuma waliahidiwa kwamba lazima watapewa hicho walichokuwa wanakumbushia/wanadai, na aliyewaahidi ni kiongozi mkubwa sana serikalini. sasa kila mara awlikuwa wakikumbushia wanapigwa danadana. hakuna majibu ya moja kwa moja ya kuridhisha, na kwa kweli migomo mingi ya hapa Udom inasababishwa na baadhi ya watu wa Utawala. Baadhi yao wana majibu ya kejeli, jeuri, kebehi, hii ndo source ya migomo hapa chuoni. taarifa hazitoki katika muda muafaka, ktu ambacho kinaleta ukengeushi mkubwa sana hapa chuon. Wanafunzi wa Informatics kama wangepewa taarifa za mara kwa mara juu ya ahadi wallioahidiwa sidhani kama leo wangekuwa wapo hapo walipo leo. Cha msingi kila mtu awajibike vyema katika nafasi yake na wanafunzi sometimes wawe na subra na wawatumie zaid viongoz wao na hawa viongozi kwa kweli wajirekebishe katka suala ya uwajibikaji kwa sababu Serikal ya Wanafunzi imelala mno. Amkeni sasa kumekucha mtimize ahadi zenu....
 
pdiddy,mbona hueleweki na huna uhakika na usemacho ndio maana suala la UDOM unasema eti ulisikia!!!hakuna mwanachuo anayeingia barabarani bila sababu,UDOM waligomea special faculty requirements ambazo wanadhurumiwa/hawapewi kabisa na wakipewa hizo hela wananunua laptops ambazo kwa masomo yao lazima uwe nayo.Ila uongozi kama kujivua gamba wanasema eti waligomea laptops
 
usilaumu sana nahisi alioandika hii thread kasoma coarse ambazo special faculty req haina umuhimu so muambie afufuke sababu tayari ashakufa..
 
akuna serikali isiyo na matatizo na pengine kwa afrika mashariki tanzania inaongoza kila sekta
kwa upande wa elimu bomu kubwa limeangukiwa wizara hii pale walipopewa bomu lililoishinda wizara ya miundo mbinu na saasa limeamia elimu

Ok nije kwenye mada hapo juu..ndugu wapendwa ni kweli waweza kusema chuo kimevamiwa na watoto walio na umri mdogo sana ndio maana hata humu jf wanamizaha kupita uko nyuma

embu jiulize wanataka nauli ipunguzwe iwe 250

kule dom wanataka kila mwanafunzi awe na laptop

wapi utapata hili ndugu zanguni kuweni makini na migomo ya kijinga muulizen zito awape njia za migomo kudai haki zenu mpaka

Wewe mtoa mada kama umesoma ungwini bora ukae kimya......je, utasoma programming bila computer?? Kwa nchi kama India chuo kina dhamini wanafunzi mikopo ya laptops kupitia mabenki na wanafunzi wanalipa kidogo kidogo mpaka wana maliza masomo.

Tatizo la wazee wa Tanzania wana endekeza siasa na wanafikiri hata nchi zingine zimeendelea kwa kupiga porojo. Lakini ukweli ni kwamba hilo halipo. Nawashauri viongozi wa Tanzania kwamba wasipo jali sayansi wenyewe wasifikiri kuna nchi kutoka ng'ambo itakuja kutufundishia vijana wetu bure mpaka waweze ku-design vifaa vya kisayansi.
 
<font size="3">Wewe mtoa mada kama umesoma ungwini bora ukae kimya......je, utasoma programming bila computer?? Kwa nchi kama India chuo kina dhamini wanafunzi mikopo ya laptops kupitia mabenki na wanafunzi wanalipa kidogo kidogo mpaka wana maliza masomo.</font><br />
<br />
<font size="3">Tatizo la wazee wa Tanzania wana endekeza siasa na wanafikiri hata nchi zingine zimeendelea kwa kupiga porojo. Lakini ukweli ni kwamba hilo halipo. Nawashauri viongozi wa Tanzania kwamba wasipo jali sayansi wenyewe wasifikiri kuna nchi kutoka ng'ambo itakuja kutufundishia vijana wetu bure mpaka waweze ku-design vifaa vya kisayansi.</font>
<br />
<br />
Huu ni utoto kwakweli. Hivi nani kakwambia laptop na faculty requirement? Laptop ni basic needs kwa kila mwanafunzi haijalishi anasoma nini. Unless muombe kuwekewa maabara maalum kwa ajili ya computer. Yaani utakuwa upuuzi wa hali ya juu kama chuo kitaanza kutoa laptop kwa wanafunzi wa Vyuo Vikuu. Ni mzigo usiobebeka. Nanyi wanafunzi hebu fungueni akilini zetu, jitahidi kufikiria zaidi ya utegemezi.
 
kuna sehemu wanafunzi wanakosea. lakini makosa makuu ni selikali na utawala kutofanya wajibu wao kwa wakati!
 
Hata sisi tulisoma vilevile na tukasoma hizo programming lakini hatukununua wala kumdai mtu laptop. Tuliendaga Kariakoo kule tukanunua PC used tukaipiga mtungo na TUKAFAULU VILEVILE..wanafunzi wa siku wana mizaha sana aisee..lol
 
Watu mnasahau haraka sana!

Wakati wa Kampeni Mzee wa Msoga kule Bagamoyo aliahidi laputop kwa kila mwalimu na wanafunzi

JK aja na ndoto mpya


na Asha Bani


RAIS Jakaya Kikwete, amesema kuwa serikali imekwishakamilisha mpango wake unaoitwa 'Tanzania Beyond Tomorrow' ambao utahakikisha kuwa katika kipindi cha miaka mitano kila mwalimu atakuwa na &#8216;laptop' yake. Kikwete aliyasema hayo Ikulu juzi wakati alipokutana na baraza la watoto kutoka mikoa mbalimbali, ikiwa ni maadhimisho ya kilele cha mtoto wa Afrika ambapo watoto hao walipata nafasi ya kumuuliza rais maswali mbalimbali.
Kauli hiyo ya Rais Kikwete kwamba walimu watakuwa na laptop, ilitokana na swali aliloulizwa na mtoto Zurekha Kipupwe (14) kutoka Dar es Salaam, aliyehoji hatua ambazo serikali inazichukua kutokana na ukosefu wa walimu, nyumba, vitabu vya ziada na kiada, na maabara katika shule za kata.
Katika majibu yake, ndipo Rais Kikwete alipogusia kuhusu mpango huo Tanzania Beyond Tomorrow ambao alisema kuwa utahakikisha katika kipindi cha miaka mitano kila mwalimu anakuwa na laptop, yake na baada ya hapo kila mwanafunzi atakuwa na kompyuta yake.
Alisema, wao kama serikali watahakikisha mpango huo unafanikiwa na kwamba kwa kuanzia wataanza na mikoa sita kwa kuhakikisha kuwa walimu wote wa shule za msingi na sekondari wanakuwa na laptop na wanafunzi kompyuta.
Alisema tayari wamekwishafanya mazungumzo na wataalamu kutoka kwa wahisani kama vile Google na wengineo ili kuhakikisha mpango huo unafanikiwa.Alisema lengo la kufanya hivyo ni kuhakikisha kuwa walimu wanaacha kutumia chaki kama wenzetu Burundi ingawa sisi tumechelewa kuanza kutekeleza hilo. Awali akijibu swali na mtoto huyo, rais alikiri kuwa matarajio ya serikali ilikuwa ni kuhakikisha miaka mitano inatumika katika kujenga shule za kata lakini pia imeonekana wazazi walikuwa na shauku katika kujenga shule nyingi.
Pia alisema kuwa suala la upungufu wa walimu linashughulikiwa na kwamba serikali imeanzisha chuo cha Dodoma, Chang'ombe, Chuo Kikuu kishiriki cha Dar es Salaam, na chuo cha Mkwawa. "Hata hivyo kuhusiana na vitabu vya ziada na kiada serikali iko kwenye mkakati wa kuhakikisha kuwa kunapatikana vitabu kwa kuwa kwa sasa tunasubiri pesa tu kutoka kwa wahisani na kwa sasa tayari tumefikia katika hatua nzuri na wafadhili," alisema Rais Kikwete. Mbali na swali hilo, watoto hao walionekana kumuuliza rais maswali kadhaa mazito ikiwa ni pamoja na yale yanayohusiana na ufisadi.
Deogratius Michael (16), kutoka mkoa wa Mwanza alimuuliza Rais: "Kwa kuwa serikali imewashughulikia mafisadi kwa kuzikusanya fedha zilizochotwa na wengine kupelekwa mahakamani, je, kwa nini fedha hizo zisingepelekwa kwenye elimu?"

Akijibu hilo rais alikiri sekta ya elimu kuwa na matatizo mengi lakini akasisitiza kuwa kilimo ni muhimu katika kuhakikisha chakula cha kutosha kinaongezeka nchini. "Fedha hizo zilizokusanywa ni shilingi bilioni 40 na zimetumika katika kufungua dirisha la kilimo katika Benki ya TIB na fedha nyingine zimetumika katika kununulia pembejeo za kilimo ikiwa ni pamoja na mbolea na kutokana na hilo mavuno yameongezeka.
Maswali mengine aliyoulizwa ni pamoja na mpango wa serikali kuwarudisha mashuleni wanafunzi waliopata mimba na kisha kuendelea na masomo; rais alijibu kuwa suala hilo bado wanaendelea kufanya mazungumzo na wanaharakati. Wanaharakati wametofautiana: kuna kundi linadai warudishwe na sheria ipitishwe na wengine wanadai wasiruhusiwe. Akitolea majibu swali lingine aliloulizwa kwamba serikali inawasaidiaje wanafunzi walioshindwa kuendelea na masomo kwa kukosa ada Kikwete alisema kuwa serikali ina utaratibu wa wanafunzi wote waliokuwa na matatizo ya ada kujiandikisha halmashauri ambapo wanakuwa na mafungu yao kwa ajili ya kuwasomesha watoto.

Alieleza kuwa endapo halmashauri itazidiwa uwezo wa kuwasomesha watoto hao kama watakuwa wameomba wengi basi wanawasiliana na makao makuu na wanasaidiwa kwa hilo. Hata hivyo baada ya mahojiano hayo wanafunzi hao walimtaka Rais Jakaya Kikwete kuongeza muda wa miaka mitano na kupata ushindi wa kishindo tofauti na ule alioupata mwaka 2005..

Tanzania daima
 
Mimi kama mdau wa maendeleo, elimu na mlipa kodi siwezi ku-endorse mwanafunzi anayedai apewe laptop. This is outrageous. Ni kweli tunahitaji wasomi wengi zaidi kama taifa, lakini with this kind of wasomi NO PLEASE. Bora waendelee kufeli tu huko shule za kata. This kind of wasomi hawatalisaidia taifa bali ni mzigo wa kuni.
 
...kule dom wanataka kila mwanafunzi awe na laptop..

Hili linaweza kuonekana la kitoto lakini kwa karne ya leo ni la muhimu sana.

Ni wajibu wa serikali kuchukua changamoto hii positively na kujaribu kuitafutia ufumbuzi. Kwa mfano, naamini kama serikali inaweza ikaingia mikataba hata na watengenezaji wa hizi laptops na zikawafikia wanafunzi hapa kwa bei nafuu kabisa! Hivi hata kwa bei za sasa za sokoni ya laptops za kawaida kabisa yale mabilioni wanayotaka kuwalipa dowans yangeweza kununua laptops ngapi? Tuliambiwa wanataka kulipa 94 billions ($ 65.8million), so kwa bei ya shillingi milioni 1.2 kwa laptop (mimi naamini kwa kuingia mkataba na manufacturer, unaweza kupata laptop nzuri tu kwa shilingi kati ya laki 6 mpaka 8!), unaweza kuwapa laptops wanafunzi zaidi ya elfu 78! Wanafunzi wa vyuo vikuu (undergraduate) wapo wangapi kwa sasa? Na kama haiwezi kuwapa bure (kama faculty requirement), si inaweza kuwakopesha tu kwa bei ya chini (subsidised)!

Wenzetu Rwanda wanazungumzia kuwa na laptop kwa kila mwanafunzi wa shule ya msingi, sisi hapa tunaona ni utoto kwa mwanafunzi wa chuo kikuu kudai laptop (shame on us!). Juzi niliona tangazo (nadhani ni la Haki Elimu) likimwonesha mwalimu anajaribu kufundisha wanafunzi wa shule ya msingi sehemu mbalimbali za komputa na jinsi ya kuwasha na kuzima bila kuwapo kwa komputa...yaani ni vichekesho tu...hata mwalimu mwenyewe anaonekana hiyo komputa anayojaribu kufundisha haijui sawasawa!


Rwanda: OLPC - 100,000 Computers to Be Imported This Year

Kigali — The government has plans to import up to 100,000 computers this year to boost the One Laptop Per Child (OLPC) programme that was launched by President Paul Kagame last September.

This was revealed yesterday by Richard Niyonkuru, the coordinator of the OLPC programme, during a meeting that brought together different stake-holders in Kigali City to devise ways of extending the project to private schools in the City.

"The ministry had planned to import only 10 000 laptops but the President, through the ministry for ICT, told us to order for 100 000," said Niyonkuru at the meeting that took place at Nyarugenge District headquarters.
According to Niyonkuru, the first consignment which is expected between April and May will be of 40 000 laptops while others which will come in two consignments of 30 000 will come in the subsequent months.

 
Abdulhalim naona umeanza kuongea kwa hisia...nimependa ulivyo jitambulisha kuwa wewe ni mdau wa maendeleo. Lakini usije kusahau kuwa hayo maendeleo hayafikiwi bila kuwa na elimu bora...unajua kwa haraka haraka mtu akisia kuwa eti wanadai laptop wale wasio jua vizur umuhimu wa kompyuta huona kuwa ni anasa. Lakini napenda nikuhakikishie kuwa kwa ulimwengu wa sasa kompyuta ni kifaa muhmu sana cha kazi....nashangaa kuona unatereza na kutaka kutoka nje ya hicho ulichodai kuwa wewe ni mdau wa maendeleo kwa kuta
 
Wazee wao wananyanyasika vijijini waowanadai laptop!!Ndizo zinazofundisha?
 
unajua nimesoma ulichoandika ni mawazo na mtazamo wako siwezi kukupinga lakini kumbuka kunanchi kama rwanda wanakauli mbiu ya one student one laptop na imewezekana,pili swala la mgomo la wanafunzi wa informatics nimelifuatialia kwa karibu sana mbali na laptop kama uongozi wa chuo unavyodai pia hapo informatics hawana walimu wa kufundisha bahazi ya kozi inapelekea kozi ya semista nzima kufundishwa wiki moja,naomba TCU ifuatatilie kwa kwa karibu iwezekani kila mwaka wanafunzi wasio pungua 70 wanafeli na kuacha masomo je tujiulize mbona vyuo,vingine akuna kitu kama hicho
 
kaka mie nakuunga mkono. mie siku ile nisikie eti wanafunzi wa UDOM wamegoma kisa laptop nilijiuliza sana na sikupata jibu aina ya wanavyuo tulio nao sasa ktk vyuo vyetu. Kitu kingine wamekuwa marimbukeni wa siasa na kuchotwa kiurahisi na wanasiasa bila kujijua kuwa wanatumika kama vile mtu anavyoitumia Jojo.Hali hii ya kutumiwa huwapelekea wao kujisahau malengo yao ya kuwepo chuoni na kusahau umuhimu wao na elimu yao ktk familia zao.

unaweza kutusaidia malengo ya kuwepo vyuoni?
 
Hili linaweza kuonekana la kitoto lakini kwa karne ya leo ni la muhimu sana.

Ni wajibu wa serikali kuchukua changamoto hii positively na kujaribu kuitafutia ufumbuzi. Kwa mfano, naamini kama serikali inaweza ikaingia mikataba hata na watengenezaji wa hizi laptops na zikawafikia wanafunzi hapa kwa bei nafuu kabisa! Hivi hata kwa bei za sasa za sokoni ya laptops za kawaida kabisa yale mabilioni wanayotaka kuwalipa dowans yangeweza kununua laptops ngapi? Tuliambiwa wanataka kulipa 94 billions ($ 65.8million), so kwa bei ya shillingi milioni 1.2 kwa laptop (mimi naamini kwa kuingia mkataba na manufacturer, unaweza kupata laptop nzuri tu kwa shilingi kati ya laki 6 mpaka 8!), unaweza kuwapa laptops wanafunzi zaidi ya elfu 78! Wanafunzi wa vyuo vikuu (undergraduate) wapo wangapi kwa sasa? Na kama haiwezi kuwapa bure (kama faculty requirement), si inaweza kuwakopesha tu kwa bei ya chini (subsidised)!

Wenzetu Rwanda wanazungumzia kuwa na laptop kwa kila mwanafunzi wa shule ya msingi, sisi hapa tunaona ni utoto kwa mwanafunzi wa chuo kikuu kudai laptop (shame on us!). Juzi niliona tangazo (nadhani ni la Haki Elimu) likimwonesha mwalimu anajaribu kufundisha wanafunzi wa shule ya msingi sehemu mbalimbali za komputa na jinsi ya kuwasha na kuzima bila kuwapo kwa komputa...yaani ni vichekesho tu...hata mwalimu mwenyewe anaonekana hiyo komputa anayojaribu kufundisha haijui sawasawa!


SMU idea yako ni nzuri lakini si endelevu. Hawa wanafunzi wanaingia chuo kila mwaka. Kwahiyo serikali kila mwaka iwe inanunua laptops? Mie nadhani wao kama hawana vitu vya kufundishiwa kama Maabara ingekuwa rahisi kuelewa tatizo ni nini. Hivi kweli katika elimu yetu priority inaweza kuwa laptop kwa wanafunzi wa Informatics? Umuhimu wa ICT unafahamika tena kwa kila mtu, kununua computer ni moja ila cha msingi professional yoyote inahitaji jitihada binafsi kujiendeleza. Vinginevyo, wanaosoma kilimo watadai matrekta muda si mrefu na wale wa mifigo sijui watadai nini au wanapewa nini. Tujifunze kujitafutia uwezo na si kuwa tegemezi.
 
Abdulhalim naona umeanza kuongea kwa hisia...nimependa ulivyo jitambulisha kuwa wewe ni mdau wa maendeleo. Lakini usije kusahau kuwa hayo maendeleo hayafikiwi bila kuwa na elimu bora...unajua kwa haraka haraka mtu akisia kuwa eti wanadai laptop wale wasio jua vizur umuhimu wa kompyuta huona kuwa ni anasa. Lakini napenda nikuhakikishie kuwa kwa ulimwengu wa sasa kompyuta ni kifaa muhmu sana cha kazi....nashangaa kuona unatereza na kutaka kutoka nje ya hicho ulichodai kuwa wewe ni mdau wa maendeleo kwa kuta
Why laptops? Kwanini msidai maabara ya computer au library yenye computer za kueleweka na za kutosha? Computer si anasa ni basics na kila mwanafunzi anastahili computer lakini hoja ya serikali igawe computer kwa kila mwanafunzi haina mashiko. Hata huo mpango wa serikali naamini utakuwa endelevu kama tu shule zitapewa maabara za computer na si kugawa computer.
 
Back
Top Bottom