Boflo
JF-Expert Member
- Jan 20, 2010
- 4,384
- 4,409
Chuo kimoja kikuu kimefungwa nchini Nigeria baada ya ghasia kuzuka kuhusiana na tukio la kuuawa kwa wanafunzi wanne, waliodaiwa kuiba komputa na simu za mkononi.
Wanafunzi wanasema kuwa wanne hao waliuawa baada ya kudhaniwa kuwa wezi kutoka katika kijiji cha Aluu.
Chuo kikuu cha Port Harcourt (Uniport) kiliwaamuru wanafunzi kwenda nyumbani,baada ya maandamano yaliyokuwa yanafanyika kukumbwa na ghasia huku Nyumba na maduka zikichomwa.
Waandishi wa habari wanasema kuwa polisi wa kupambana na ghasia pamoja na wanajeshi, wameenda katika chuo hicho, ambacho maafisa wakuu wanasema kitasalia kufungwa hadi hali itakapotulia.
the evil killing of students in port-harcourt,nigeria - YouTube
Source BBC