Pretty R.
JF-Expert Member
- Apr 14, 2012
- 200
- 31
Jamani wanafamilia wa JF mimi mwenzenu nimehitimu chuo mwaka jana mwezi wa 6. Nimezunguka na bahasha mpaka hivi leo sijabahatika kupata kazi wala kibarua. Nimetembea mpaka viatu vimeisha soli. Humu JF najua kuna watu wenye positions zao na pia wenye ofisi zao au miradi inayohitaji wafanyakazi na naamini kabisa watalisoma tangazo langu. Naomba kama kuna atakayeweza kunisaidia anisaidie jamani nimeshakata tamaa ya maisha. Nimesoma utawala na jamii. Mungu awabariki sana ndugu zangu.