Python Newbie
Member
- Jul 17, 2017
- 77
- 49
Za jioni wakuu,
Napenda kujifunza vitu vipya na kuanzia jumatatu ya wiki hii nimeanza kujifunza programming language ya python. IT sio fani yangu niliyosomea ila nataka nianze kutengeneza applications kama hobby na kujifunza kitu kipya.
Background ya IT : nilishawahi kujifunza HTML kama miaka 4 iliyopita kwa kutumia online tutorials nadhani nimeshasahu mengi.
Resources : Nimeamua kutumia Codecademy kama chanzo changu cha taarifa kwa sababu ni free na kozi zao ziko simple na well structured na kila hatua kuna mazoezi ya kufanya yanayosaidia kuelewa zaidi.
Nilipofikia: mpaka sasa nimemaliza asilimia 28 ya kozi nzima(nimetumia siku tatu - angalau saa moja kila siku) nimejifunza Syntax, Strings and Console, Conditionals and Control Flow sasa najiandaa kuanza Functions.
Malengo: Nategemea kumaliza kozi yangu ndani ya wiki mbili au tatu na kutengeneza application itakayosaidia kuorganize taarifa za wagonjwa wanapofika hospitali nia iwe kupunguza muda anaotumia mgonjwa hospitalini au application yoyote itakayofanana na hiyo.
Changamoto : Kutokana na niiyojifunza, nimetengeneza application inayoitwa JF Saccos ambayo mteja anaandika jina na umri. Nimeweka condition kuwa kwenye kuandika jina liandikwe bila kuweka namba yoyote na ikiwekwa namba basi apewe taarifa kuwa 'amekosea na aanze upya' jambo ambalo nimefanikiwa ila kwenye umri nimejaribu kuweka condition iwe zaidi ya miaka 18 na akikidhi vigezo akaribishwe na sentesi "Hongera ndugu %s, mwenye miaka %s,umefanikiwa kufungua akaunti" na akiwa chini ya miaka 18 apewe taarifa kuwa "Hairuhusiwi Wenye Umri Chini Ya Miaka 18". Ila tatizo hata nikiweka chini ya miaka 18 bado inakubali. Sijaelewa nini shida kwenye code. Walimu mnaweza kunisaidia. Mnaweza kuicheki hapa na nimeweka screenshot chini.
========
UPDATE 1
Nimesoma topic ya function ila bado kuna subtopic bado sijaimaliza...nilitaka nije na code inayojumuisha function ila nitasubiri nimalize kwanza function.
Nimefanya zoezi lingine kwa kuandika codes ya Project inayoitwa "JF Health Centre" inayomtaka user kuandika jina na umri na kumkaribisha kwenye huduma kwa kumtaja jina na umri na pia kumtaka kuchagua aina ya daktari aidha daktari bingwa au daktari wa kawaida(GP) na kumpatia gharama ya consultation kulingana na uchaguzi wa aina ya daktari.
View attachment 548112
Pia nimegundua kutokuwa na elimu ya loops inanifanya nisiweze kuiamuru code isimame pale user anapokosea aina ya entry. So nitasubiri nimalize loops nijue nitasolve vipi tatizo hilo though mdau @Arduino Sentinel alinidokezea.
Stefano Mtangoo
======
UPDATE 2
Habari za jioni wakuu ?
Leo nimekuja na nyongeza ya kile nilichojifunza na kukifanyia kazi. Kwa kifupi nimefanikiwa kusoma functions na nimejaribu kuiweka kwenye hii project yangu ya kujifunzia.
Program yangu kwa sasa inakubali majina mawili ya mgonjwa pamoja na umri,urefu na uzito na kisha inapiga hesabu ya BMI na kutoa taarifa kama mgonjwa ana uzito sawa au overweight.
Pia inampa uchaguzi wa aina ya daktari anayetaka kumuona('specialist' au 'gp') pamoja na aina ya check up anayotaka kufanyiwa('general' au 'full') na inapiga hesabu ya jumla ya gharama na kumtaarifu mgonjwa. Nimeweka gharama ya specialist ni elfu 30 na gp elfu 10 pia gharama ya general check up ni elfu 50 na full check up ni laki na nusu. So mwisho gharama ni kutokana na uchaguzi wa hivyo viwili.
Code ni hizo hapo chini:
Unaweza kuijaribu hapa
Pia nimejifunza lists na library na ninaziandikia code ambapo kutakuwa na libray ya madaktari, vipimo, madawa nk
Karibuni kwa michango yenu
========
UPDATE 3
Za jioni wanajamii,
naomba msaada kwa yoyote atakayeweza kunisaidia...
Nimeandika calculator ya menu ya chakula pamoja na bei...yani inabpiga hesabu kutokana na vyakula unavyochagua then inakupa gharama ya jumla halafu kama gharama ni zaidi ya elfu 10 inamtaarifu mtoa huduma kuwa mteja apewe punguzo la bei ila kama ni chini ya 10 inamtaarifu kuwa mteja hatakiwi kupewa punguzo la bei.
Sasa shida ni hapo mwisho ambapo hata kama jumla ya gharama ni chini ya elfu 10 bado program inatoa taarifa kuwa mteja apewe punguzo la bei.
code ni hizo hapo naomba msaada
Stefano Mtangoo Arduino Sentinel Andy Kawa Graph
Napenda kujifunza vitu vipya na kuanzia jumatatu ya wiki hii nimeanza kujifunza programming language ya python. IT sio fani yangu niliyosomea ila nataka nianze kutengeneza applications kama hobby na kujifunza kitu kipya.
Background ya IT : nilishawahi kujifunza HTML kama miaka 4 iliyopita kwa kutumia online tutorials nadhani nimeshasahu mengi.
Resources : Nimeamua kutumia Codecademy kama chanzo changu cha taarifa kwa sababu ni free na kozi zao ziko simple na well structured na kila hatua kuna mazoezi ya kufanya yanayosaidia kuelewa zaidi.
Nilipofikia: mpaka sasa nimemaliza asilimia 28 ya kozi nzima(nimetumia siku tatu - angalau saa moja kila siku) nimejifunza Syntax, Strings and Console, Conditionals and Control Flow sasa najiandaa kuanza Functions.
Malengo: Nategemea kumaliza kozi yangu ndani ya wiki mbili au tatu na kutengeneza application itakayosaidia kuorganize taarifa za wagonjwa wanapofika hospitali nia iwe kupunguza muda anaotumia mgonjwa hospitalini au application yoyote itakayofanana na hiyo.
Changamoto : Kutokana na niiyojifunza, nimetengeneza application inayoitwa JF Saccos ambayo mteja anaandika jina na umri. Nimeweka condition kuwa kwenye kuandika jina liandikwe bila kuweka namba yoyote na ikiwekwa namba basi apewe taarifa kuwa 'amekosea na aanze upya' jambo ambalo nimefanikiwa ila kwenye umri nimejaribu kuweka condition iwe zaidi ya miaka 18 na akikidhi vigezo akaribishwe na sentesi "Hongera ndugu %s, mwenye miaka %s,umefanikiwa kufungua akaunti" na akiwa chini ya miaka 18 apewe taarifa kuwa "Hairuhusiwi Wenye Umri Chini Ya Miaka 18". Ila tatizo hata nikiweka chini ya miaka 18 bado inakubali. Sijaelewa nini shida kwenye code. Walimu mnaweza kunisaidia. Mnaweza kuicheki hapa na nimeweka screenshot chini.
========
UPDATE 1
Nimesoma topic ya function ila bado kuna subtopic bado sijaimaliza...nilitaka nije na code inayojumuisha function ila nitasubiri nimalize kwanza function.
Nimefanya zoezi lingine kwa kuandika codes ya Project inayoitwa "JF Health Centre" inayomtaka user kuandika jina na umri na kumkaribisha kwenye huduma kwa kumtaja jina na umri na pia kumtaka kuchagua aina ya daktari aidha daktari bingwa au daktari wa kawaida(GP) na kumpatia gharama ya consultation kulingana na uchaguzi wa aina ya daktari.
View attachment 548112
Pia nimegundua kutokuwa na elimu ya loops inanifanya nisiweze kuiamuru code isimame pale user anapokosea aina ya entry. So nitasubiri nimalize loops nijue nitasolve vipi tatizo hilo though mdau @Arduino Sentinel alinidokezea.
Stefano Mtangoo
======
UPDATE 2
Habari za jioni wakuu ?
Leo nimekuja na nyongeza ya kile nilichojifunza na kukifanyia kazi. Kwa kifupi nimefanikiwa kusoma functions na nimejaribu kuiweka kwenye hii project yangu ya kujifunzia.
Program yangu kwa sasa inakubali majina mawili ya mgonjwa pamoja na umri,urefu na uzito na kisha inapiga hesabu ya BMI na kutoa taarifa kama mgonjwa ana uzito sawa au overweight.
Pia inampa uchaguzi wa aina ya daktari anayetaka kumuona('specialist' au 'gp') pamoja na aina ya check up anayotaka kufanyiwa('general' au 'full') na inapiga hesabu ya jumla ya gharama na kumtaarifu mgonjwa. Nimeweka gharama ya specialist ni elfu 30 na gp elfu 10 pia gharama ya general check up ni elfu 50 na full check up ni laki na nusu. So mwisho gharama ni kutokana na uchaguzi wa hivyo viwili.
Code ni hizo hapo chini:
Code:
from datetime import datetime
date=datetime.now().strftime("%d-%m-%y %H:%M:%S")
print "KARIBU JF HEALTH CENTRE PATIENT'S DATABASE> Leo ni tarehe %s" %(date)
name=raw_input("Jina la kwanza la Mgonjwa:")
sir_name=raw_input("Jina la ukoo la Mgonjwa")
print "Umri:"
age=input()
age=float(age)
print "Uzito(kg):"
weight=input()
weight=float(weight)
print "Urefu(metre):"
height=input()
height=float(height)
bmi= weight/(height**2)
if bmi<30:
print "Ndugu %s %s, mwenye umri wa miaka %s,ana uzito sahihi kulingana na urefu" %(name,sir_name,age)
if bmi>30:
print "Ndugu %s %s, mwenye umri wa miaka %s,ana tatizo la ongezeko la uzito wa mwili(OVERWEIGHT)" %(name,sir_name,age)
def doctor(grade):
if grade=="specialist":
return 30000
if grade=="gp":
return 10000
def examination(exam):
if exam=="general":
return 50000
if exam=="full":
return 150000
def cost(grade,exam):
return doctor(grade)+ examination(exam)
grade=raw_input("Mgonjwa anataka kuonwa na 'specialist' au 'gp' ?")
exam=raw_input("Mgonjwa anataka kufanya 'general' au 'full' check up ?")
print "Jumla ya gharama ya matibabu ni shillingi za kitanzania %s" %cost(grade,exam)
Pia nimejifunza lists na library na ninaziandikia code ambapo kutakuwa na libray ya madaktari, vipimo, madawa nk
Karibuni kwa michango yenu
========
UPDATE 3
Za jioni wanajamii,
naomba msaada kwa yoyote atakayeweza kunisaidia...
Nimeandika calculator ya menu ya chakula pamoja na bei...yani inabpiga hesabu kutokana na vyakula unavyochagua then inakupa gharama ya jumla halafu kama gharama ni zaidi ya elfu 10 inamtaarifu mtoa huduma kuwa mteja apewe punguzo la bei ila kama ni chini ya 10 inamtaarifu kuwa mteja hatakiwi kupewa punguzo la bei.
Sasa shida ni hapo mwisho ambapo hata kama jumla ya gharama ni chini ya elfu 10 bado program inatoa taarifa kuwa mteja apewe punguzo la bei.
code ni hizo hapo naomba msaada
Code:
def breakfast(asubuhi):
if asubuhi=="chai":
return 1000
if asubuhi=="maziwa":
return 2000
def lunch(mchana):
if mchana=="wali":
return 2500
if mchana=="pilau":
return 3000
def dinner(usiku):
if usiku=="viazi":
return 4000
if usiku=="ndizi":
return 7000
def gharama(asubuhi,mchana,usiku):
return breakfast(asubuhi)+lunch(mchana)+dinner(usiku)
asubuhi=raw_input("Kifungua kinywa (chai au maziwa ?)")
mchana=raw_input("Chakula cha mchana(wali au pilau?)")
usiku=raw_input("Chakula cha usiku(viazi au ndizi)")
print "gharama ni tz sh. %s" %gharama(asubuhi,mchana,usiku)
if gharama<10000:
print "hakuna punguzo la bei"
if gharama>10000:
print "toa punguzo la bei"
Stefano Mtangoo Arduino Sentinel Andy Kawa Graph