GE2025 Wanachama CCM Jimbo la Nachingwea Lindi, Wamerudisha Kadi za uanachama baada ya Mgombea ubunge waliyemtaka kuondolewa kwenye kinyang'anyiro

GE2025 Wanachama CCM Jimbo la Nachingwea Lindi, Wamerudisha Kadi za uanachama baada ya Mgombea ubunge waliyemtaka kuondolewa kwenye kinyang'anyiro

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,446
Reaction score
2,093
Wanachama wanaodaiwa kuwa wa Chama cha Mapinduzi (CCM) katika jimbo la Nachingwea mkoani Lindi, wameonekana wakirudisha vifaa mbalimbali na kadi za chama hicho, chanzo kikielezwa kuwa mgombea ubunge waliyemtaka ameondolewa kwenye kinyang'anyiro cha kuwania nafasi hiyo




Chanzo: Habari Digital
 
Kwani ni lazima agombee ccm tu? Ahamie ACT wazalendo wakampe kura huko kama wanamuhitaji
 
Rais wa Sasa kaharibu sana mfumo wa uchaguzi wa viongozi tunataka wananchi.Kinachofanyika Kwa Sasa ni yeye kupiga simu nataka nani awe mbunge Kwa njia yeyote
 
Waambie kura zao hatuzihitaji

Mbunge ameshachaguliwa Jana na Kamati Kuu, mgombea wa Jana wa Dodoma hata akipata kura 100 hizo hizo tutamtangaza ndiye Mbunge wao tu watake wasitake 🤗
Tena waache ujinga kabisa, kamati kuu imeshawapatia chaguo lao. Aliyeteuliwa na kamati kuu ndio chaguo lao.
 
Tena waache ujinga kabisa, kamati kuu imeshawapatia chaguo lao. Aliyeteuliwa na kamati kuu ndio chaguo lao.
Hakika Mkuu, wala hatutambui hizo kura zao za Wajumbe kama alishinda ama alishindwa

Muhimu sisi Kamati Kuu ndiyo tunaamua nani awe Mbunge wao 🤗
 
Hiki Chama sijui kama kinatumia akili kwa sasa, yaani watu wapoteze muda kuchagua, halafu nyie mnamjua mnayemtaka mmetulia tu. Si mngewaambia mapema basi huyo hatumtaki tunamtaka huyu
 
Waambie kura zao hatuzihitaji

Mbunge ameshachaguliwa Jana na Kamati Kuu, mgombea wa Jana wa Dodoma hata akipata kura 100 hizo hizo tutamtangaza ndiye Mbunge wao tu watake wasitake 🤗
Huu utqratibu aliuleta Marehemu, aliharibu sana nchi.
 
Kwani ni lazima agombee ccm tu? Ahamie ACT wazalendo wakampe kura huko kama wanamuhitaji
Je atakua kwenye mpango wa wabunge wakujazilishia bunge kuonyesha hata wapinzani wamo bungeni?
 
Simple tuu, jamaa ahame chama ila goli la mkono cjui kama litamuacha salama
 
Hakika Mkuu, wala hatutambui hizo kura zao za Wajumbe kama alishinda ama alishindwa

Muhimu sisi Kamati Kuu ndiyo tunaamua nani awe Mbunge wao 🤗
Sahihi kabisa mkuu, na kama wanahisi hizo kadi zao ndio zinatupa kura na kutuweka tulipo basi wasubiri Oktoba wajionee muujiza.
 
Back
Top Bottom