Mkuu
Yericko Nyerere.
Umeweka sawasawa kisu kwenye mfupa! Nami naomba niwe kama muwindaji wa ndege! Nilenge shabaha kwanza ndio niachie manati bila kupiga kwenye kipago.
Naweke msingi wa nukta zangu kwa kusema yafuatayo.
1. CCM imeiacha misingi yake iliyo asisiwa nayo na kushika mkondo ambao haukuwa wa misingi mikuu, kwa kuicha misingi yake iliyo asisiwa nayo wananchi wengi wamekosa imani na matarajio ya ustawi endelevu kupitia ccm. (Misingi ya kujali utu, raslimali za nchi, udugu, amani na utulivu wa nchi, kupiga vita rushwa, nk havipo tena ndani ya ccm). CCM imeshindwa kutembea juu ya msingi yake na matokeo yake kwa kuogopa nguvu ya watu wenye fedha wamejikuta wanachagua wagombea ambao hawakidhi matarajio ya wananchi wala kufuata misingi iliyo asisiwa kwayo.
Mwl Nyerere alisha waonya mwaka 1995, kwa kuwaambia wachague mtu ambaye atakidhi matarajio ya watanzania maana watanzania wanahitaji mabadiliko. Alipaza sauti yake mzee watu pale Dodoma (R. I. P). "...Watanzania wasipo yaona, wasipo yapata mabadiliko ndani ya ccm watayatafuta nje ya ccm".
Yametimia! Watanzania hawana imani tena kuwa wanaweza kuyapata mabadiliko ndani ya ccm (kupitia wagimbea wa ccm), sasa hivi mabadiliko wanayatafuta nje ya ccm, nje ya ccm kupitia chama kikuu cha upinzani kinacho ilaza macho ccm. CHADEMA. Na ndio maana chama hiki leo kina watu wa familia ya Mwl Nyerere ambao nao kama watanzania wengine hawayaoti mabadiliko ndani ya ccm.
2. Watanzania wamechoshwa na uendashaji mbovu wa nchi yao ambao umegubikwa na rushwa kila mahali, rushwa imewaathiri watanzania kwa kuto kuzifaidi raslimali zao, madini yao yamebinafishwa kwa mikataba ya kilaghai, wanyama wao wanatoroshwa kwa rushwa na ghilba zisizo kuwa na haya, vyombo vya kusimamia haki na kulinda usalama wa watanzania haviaminiki tena! (Sio wananchi wa kawaida wala viongozi waandamizi wa serikali). Kila mahali ni rushwa, kwenye hili Mwl Nyerere aliwaambia wana ccm pale Dodoma "Chagueni mtu ambaye hata ukiulizwa swali, huyu atatusaidia kupiga vita rushwa?, jibu litoke ndani ya roho kwamba NDIO!" Wangapi wana ccm leo wanaweza kutoka mbele ya hadhara na kupiga kifua kwa kusema kiongozi/viongozi wetu wanapiga vita rushwa?! Hili limewachoshwa wananchi ndio maana wanaiona chadema kuwa ndio mkombozi wao na waliipa heshima kuanzia pale kwenye list of shame mwembe yanga.
3. Ccm kimeacha kuwa chama cha wakulima na wafanya kazi matokeo yake kimegeuka kuwa chama cha matajiri na mafisadi. Leo hii bila kuwa na mafurushi ya fedha ni vigumu kupenya kwenye chaguzi za ccm! Wenye chama ambao ndio wanawakilishwa na ile alama ya jembe na nyundo wanaona wameporwa chama chao! Kwa mantiki ya kawaida ukiporwa unacho miliki kama huwezi kukipigania kukirejesha unakuwa mpole na kutafuta kingine utakacho weza kuita cha kwako, hii ndio sababu ya wakulima na wafanyakazi wengi kuachana na ccm na kujiunga na chadema maana wamekuwa wanaambiwa wazi na peupe kuwa "ccm ina wenyewe". Wamewaacha wenyewe wenye ccm yao wamejiunga kwa chadema chama chao.
4. Ccm imekubuhi kwa kuwagawa watanzania kwa misingi ya dini na makabila, labda bila kujua athari zake, mara kadhaa ccm wamekuwa wakinadi kuwa vyama flani vya upinzani nivya dini fulani au mahali fulani. Walianza na NCCR, wakaja na CUF kuwa ni chama cha kidini na chama cha wapemba magaidi, leo wanasema chadema ni chama cha watu wa kaskazini wakristo. Watanzania wamegundua kuwa wao ni wamoja hawataki tena kugawanywa kwa udini na ukabila, wengi walio chukizwa na mambo hayo wameichukia na kuidharau ccm kwa propaganda zake chafu, wamekataa hila hizi, wameamua kujiunga na jeshi la ukombozi ili kurudisha heshima na utu wa mtanzania ulio jali haki na usawa. Matarajio yao yapo ndani ya chadema.
HITIMISHO.
Ccm imewaongoza watanzania kwa miaka 50 (nusu karne) kwa kuwa imeshidwa kutatua matatizo na changamoto ilizokumbana nazo na nyingine kwa kuzisababisha yenyewe, basi kinahitajika chama kingine chenye watu wenye upeo na fikra mpya zenye muono mwingine tofauti nawa ccm ili kuikwamua nchi yetu kutoka kwenye hili tope.
Mwanamahesabu mmoja wa bara la Ulaya aliwahikusema "... Problems cannot be solved by the same level of thinking which created them"
Muhimu ni ccm kutambua tu kuwa hawana hati miliki ya kuwaongoza watanzania kama wameichoka na hawaitaki iendelee kukaa madarakani.