Wana CHADEMA tuzungumzie mustakabali wa chama

Wana CHADEMA tuzungumzie mustakabali wa chama

na Magufuli Kura za kubadili katiba aendelee kwa miaka kumi mingine atapigiwa na wengi ama wanajielewa au hawajielewi UTAJUA,..inshu si wengi..., UTAONA.. . TUONE..
Naona unaruka ruka tu, siku nyingine ukija huku ujipange vizuri, umehama kwa Mbowe ghafla umemrukia Magufuli, nikikubana na hapo unaweza kumrukia Mizengo Pinda.
 
ndio mtakeshaga na akili hizo hizo

Uko sahihi sana kwenye post yako namba moja, ni kweli kiongozi mzuri hawezi kukaa madarakani zaidi ya miaka 10, hivyo ni sahihi kabisa kwa Mbowe kuachia hicho cheo.

Sasa tuje kwenye uhalisia, vyama viko vingi, kwanini usipeleke huu ushauri wako kwenye vyama vingine ili vikue kupitia huu ushauri wako, au ww mwenyewe uanzishe chama chako tukione ukuaji wake, au ww ni motivational speaker? Magufuli hasubiri kisingizio cha Mbowe kuendelea kukaa madarakani, bali hayo ni matamanio yake muda wote. Huenda hujui tofauti ya nchi na chama, ndio maana unatumia kigezo cha uwenyekiti wa Mbowe kama kigezo cha Magufuli kukaa madarakani.

Kwa sasa hakuna chama chochote kinafanya siasa hapa nchini, hivyo sijui umetumia kigezo gani kujua uimara au kifo cha cdm. Sasa hivi tunashuhudia kiburi cha madaraka ya urais kupitia mwenyekiti wa ccm, na sio uimara wa siasa za ushindani. Kama ni uchaguzi ndio unataka kuutumia kama kigezo cha kuonyesha ccm ni imara na cdm imekufa, ni kuwa toka Magufuli ameingia madarakani hakujwahi kufanyika uchaguzi, bali kumekuwa na maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura. Kwa ujumla watu wamepuuza siasa za kishenzi zilizoletwa na huyu mlevi wa madaraka.
 
Sababu ya kuibiwa kura inasisitizwa ili agenda ya Uongozi na mabadiliko kuimarisha upya chama yasizungumzwe wakati hali ni mbaya.

Uchaguzi umepita kuibiwa tayari tumeibiwa jee tung'ang'anie kuibiwa kura kuwa ni agenda ya kila siku mpaka 2025?

Tutafute njia ya kuimarisha chama hali ni mbaya na viongozi katika kanda nyingi au hawatoi huduma ya kuendeleza Chama ama kuzembea na kisingizio ni hali ya kipesa hoi chamani.

Anzisha chama chako ili tuone ukuaji wake maana ww ni msomi. Au usomi wako unautumia kwenye vyama vya wanaume wengine?
 
Chadema😃😃😃😃😃

Hivi nikiwa ndio walipanga waweke rehani madini ili Mabeberu wawape pesa ya kuendesha nchi ambapo walitaka
Tundu awe rais
Salum makamu wa rais
Mbowe waziri mkuu
Lema waziri wa mambo ya ndani
........
.........

Nabaki kujichekea tuuu

Magufuli amesema aliamua kuachana na mradi wa gas maana gas yetu imeuzwa kwa wajanja, je cdm ndio waliiuza kwa hao wajanja? Hapa ndio utajua ww ni kiazi kwenye shamba la mihogo. Wenzio wanakuimbisha uzalendo uchwara huku akina JK waliouza hiyo gas wanajengewa mahekalu ya kumalizia uzee wao. Hii inaitwa utajua hujui.
 
na Magufuli Kura za kubadili katiba aendelee kwa miaka kumi mingine atapigiwa na wengi ama wanajielewa au hawajielewi UTAJUA,..inshu si wengi..., UTAONA.. . TUONE..

Huna unalojua zaidi ya kupiga siasa mfu hapa jukwaani. Shule zimeshafunguliwa, ila sijui ww mtoto unafanya nini humu jukwaani, au mzazi wako hajalipa ada?
 
Mustakabali wa chama hujadiliwa kwenye vikao vya chama, nyie minyau ya sisiyemu ndio mnakuja mitandaoni mkijidai ni CHADEMA

unamquote nyerere wakati uko chadema, unatakiwa umquote mbowe alivosema atakua wa mwisho kuhujumu chama
 
Magufuli amesema aliamua kuachana na mradi wa gas maana gas yetu imeuzwa kwa wajanja, je cdm ndio waliiuza kwa hao wajanja? Hapa ndio utajua ww ni kiazi kwenye shamba la mihogo. Wenzio wanakuimbisha uzalendo uchwara huku akina JK waliouza hiyo gas wanajengewa mahekalu ya kumalizia uzee wao. Hii inaitwa utajua hujui.
Chama imara na chama chenye uongozi bora ni kile kinachokubali makosa na kuwajibika kwa kubadilika
 
Chama imara na chama chenye uongozi bora ni kile kinachokubali makosa na kuwajibika kwa kubadilika

Unakubali makosa au unasema unakubali makosa, ama unadhani hatujui matumizi ya hiyo lugha ya ulaghai? Unasema unakubali makosa na kujisahihisha, lakini unazidi kukaa madarakani kwa njia ovu na matumizi mabaya ya madaraka! Uza ubongo huo maana unakaa nao kwa hasara.
 
Sababu ya kuibiwa kura inasisitizwa ili agenda ya Uongozi na mabadiliko kuimarisha upya chama yasizungumzwe wakati hali ni mbaya.

Uchaguzi umepita kuibiwa tayari tumeibiwa jee tung'ang'anie kuibiwa kura kuwa ni agenda ya kila siku mpaka 2025?

Tutafute njia ya kuimarisha chama hali ni mbaya na viongozi katika kanda nyingi au hawatoi huduma ya kuendeleza Chama ama kuzembea na kisingizio ni hali ya kipesa hoi chamani.
Kuna siku nilikuuliza maswali hukujibu hata moja, lakini bado unaendelea kupiga kelele kama msukule, labda unijibu hili leo, hiyo hali mbaya ya chama imesababishwa na Mbowe? mazingira ya kisiasa since 2015 hapa Tanzania unayafahamu? hebu tutajie chama cha upinzani kingine chenye hali nzuri ukiondoa ACT waliojiunga SUK.

Yaani unataka kusema Chadema kabla ya kampeni mwaka jana ilikuwa na hali mbaya kisiasa, halafu ghafla kwenye kampeni hali ikawa nzuri mpak wakafanya uharamia kwenye matokeo, then after kampeni hali ya Chadema imerudi ghafla kuwa mbaya tena kisiasa?!
 
na Magufuli Kura za kubadili katiba aendelee kwa miaka kumi mingine atapigiwa na wengi ama wanajielewa au hawajielewi UTAJUA,..inshu si wengi..., UTAONA.. . TUONE..
Vp umemuona leo kule Shinyanga?? Vp afya yake kwako unaona atatoboa 2025?? Siku zote ukishaona mtu anawasemehe aliowatuhumu basi ujue kuna jambo. Kaanza na wale Raia wa Ethiopia leo Wakurugenzi. Kesho keshokutwa??
Kwenye suala la corona umesikia tamko lake ni wazi kachoka. Hana uwezo tena wa kufikiri.
 
Back
Top Bottom