Wana CHADEMA tuzungumzie mustakabali wa chama

Eng. Y. Bihagaze

JF-Expert Member
Sep 8, 2011
1,488
908
Chadema tuongeeni kidogo

Ndugu zangu wanaChadema tumepoteza kabisa welekeo!

Mtu mjinga, asiye na akili, akifeli kwenye jambo lake lolote atatafuta kisingizio. Na mara zote hurushia lawama kwa wengine. Chadema tumefeli! Kwenye uchaguzi huu 2020 tumefeli.

Kwamba tuliibiwa, kwamba tulikosa fedha, kwamba tulizidiwa na masababu yote hayo lakini output ni failure! Tusitafute mchawi nje, sisi wenyewe ndani. Lazima kujitafakari upya. Tatizo ni kiongozi mkuu wa chama.

Kuna damu changa yenye akili inayo chemka, wapewe usukani. Hii tabia ya kung’ang’ania madarakani hata kama boti limezama mwanaume bado uko tu na usukani ukidhani mashetani wataibuka kukuibua ni uzembe wa mawazo.

Mbowe kwenye chama hiki ni jabali, mpiganaji, sio milima miwili au mitatu amevuka na amevusha wengi. Heshima yake lazima ilindwe. Lakini ndio tutakuwa na akili zilezile za kudhani wewe ni bora zaidi na hakuna wa kuongoza chama zaidi yako.

Mimi nampa mbowe miezi mitatu hadi april 2021, atangaze kujiondoa CHADEMA apishe watu wengine na maono mengine na mwelekeo mpya. Hayo ya kusubiri eti mpaka 2024 mbali sana, utabadilishaje mwenyekiti wa chama wakati mna elekea kwenye uchaguzi?

Si ndio ujinga wenyewe huo wa kufelishana, tunajifelisha wenyewe kwa katiba, wenzetu mapema mwenyekiti wao wanamthibitisha mara baada ya uchaguzi ila Chadema tunangojea tume karibia.

Nikisema hivi utaona mjinga anapost we mataga! Hoja kama hizi kila anayetoa hoja makini mnamshambulia. Ni mtu mwenye uchungu na chama anapoona kuna kwa ujinga ulio wazi kabisa, asipopisha mtaniona natoka mzima mzima kumpigia kampeni Rais Magufuli katiba ibadilishwe aongezewe muda na hakuna atakayepinga CHADEMA kwa sababu kama mbowe tunasema ni bora kwenye chama aendelee sasa kwanini tusiseme Magufuli ni bora na aendelee! Miaka mingapi mbowe ni mwenyekiti wa CHADEMA?

Mtei alikuwa mwenyekiti kwa miaka sita(6) tu (1992-1998) Bob Makani akawa mwenyekiti tena miaka sita tu (1998-2004) kisha Mbowe akachukua kijiti hadi leo miaka sasa ngapi 22 tunakwenda yupo tu. Sasa kwanini Rais Magufuli asipewe mingine kumi? Kuna ubaya gani? Kama tabia ndio hii ya kuamini kwamba huyu ni bora kuliko wengine.

Mimi sidhani kama ishu ya Rais Magufuli kuongezewa muda CHADEMA tutaipinga, tutaanzia wapi kupinga! Wakati tuko kwenye boti hilo hilo!

Mjue tunahitaji chama makini, mbaya zaidi siku hizi tumekuwa Wizara ya Afya, yaani tunajichora kupita kawaida. Akili ya kiongozi mkuu wa chama ikishachoka hakuna ujenzi wa chama wala mbinu mpya, zile alizokuwa nazo zote zimegonga mwamba na kabakia kurukia maneno na matamshi ambayo baadae anachoreka!
 
Sikumaliza kusoma baada yakukutana na uharo wako. Chadema kama chama cha Siasa ina taratibu zake. Sasa wewe unawashwa nn?? Simlishinda uchaguzi?? Pambaneni kivyenu mjenge Nchi yenu ya Chato.
 
Naam,

  1. Chadema wamefeli
  2. Kura hazikuibiwa
  3. Mbowe ana muda mrefu sana aondoke iingie damu changa
  4. Tunahitaji Chama Makini
Haya Bwana Chadema,tumesikia!Mbowe mbandikeni kesi ya uhujumu akaozee jela akitoka damu changa inandesha Chama makini.Mbona rahisi tu!
 
kwa sasa ajenda ya kwenda nayo ni corona.
corona ni Ugonjwa wa msimu, december hadi April mafua yanakwisha, ni badiliko la majira ya aphelion na pelihelion yanayo badilika baada ya miaka 400, mwanzoni ilikuwa january to May sasa ni december to April, itasumbua miaka zaidi ya saba. HAKUNA CHANJO WALA KIDHIBITI HALI HII. NI MOVEMENT AMBAYO ITAISHA YENYEWE BAADA YA 7 YEARS. UKIPENDA KUAMINI AMINI USIPOTAKA KUAMINI ACHA. HUBADILISHI UKWELI.
 
corona ni Ugonjwa wa msimu, december hadi April mafua yanakwisha, ni badiliko la majira ya aphelion na pelihelion yanayo badilika baada ya miaka 400, mwanzoni ilikuwa january to May sasa ni december to April, itasumbua miaka zaidi ya saba. HAKUNA CHANJO WALA KIDHIBITI HALI HII. NI MOVEMENT AMBAYO ITAISHA YENYEWE BAADA YA 7 YEARS. UKIPENDA KUAMINI AMINI USIPOTAKA KUAMINI ACHA. HUBADILISHI UKWELI.
wenzako hawajui hilo,yaani ni kama kasuku kila wimbo wanafatisha.
 
Engineer Belhazier wape hongera CCM kwa ushindi wa kishindo pamoja na kuweza kkunda kama to za Bunge kupitia wale 19.
hii sio Chadema ya Kuendekeza, wacha lizame.. tujenge nchi.. chadema izame ife ipotee ikwishe.. watu gani hawasikii, hawaoni, hawatafakari, hawajiulizi..
 
Nimekusoma hata hueleweki, unasema Chadema waliibiwa kura 2020 halafu kwa akili zako mgando namna bora ya kupambana na hilo ni Mbowe aondoke! kwani akiondoka Mbowe akaja m/kiti mwingine CCM hawataiba?

Badala ulete solution ya kudumu itayomaliza tatizo la kuibiwa kura umekuja kupiga kelele tu kumhusu Mbowe, huyo Mbowe huo uenyekiti amepewa kwa kura za wengi wenye kujielewa, msigeuze uenyekiti wa Chadema uonekane kama usultani wa kurithishwa, hizi kelele zenu za kitoto about Mbowe mtawadanganya wasiojielewa tu.
 
Nimekusoma hata hueleweki, unasema Chadema waliibiwa kura 2020 halafu kwa akili zako mgando namna bora ya kupambana na hilo ni Mbowe aondoke! kwani akiondoka Mbowe akaja m/kiti mwingine CCM hawataiba?

Badala ulete solution ya kudumu itayomaliza tatizo la kuibiwa kura umekuja kupiga kelele tu kumhusu Mbowe, huyo Mbowe huo uenyekiti amepewa kwa kura za wengi wenye kujielewa, msigeuze uenyekiti wa Chadema uonekane kama usultani wa kurithishwa, hizi kelele zenu za kitoto about Mbowe mtawadanganya wasiojielewa tu.
na Magufuli Kura za kubadili katiba aendelee kwa miaka kumi mingine atapigiwa na wengi ama wanajielewa au hawajielewi UTAJUA,..inshu si wengi..., UTAONA.. . TUONE..
 
Chadema😃😃😃😃😃

Hivi nikiwa ndio walipanga waweke rehani madini ili Mabeberu wawape pesa ya kuendesha nchi ambapo walitaka
Tundu awe rais
Salum makamu wa rais
Mbowe waziri mkuu
Lema waziri wa mambo ya ndani
........
.........

Nabaki kujichekea tuuu
 
Chadema tuongeeni kidogo

Ndugu zangu wanaChadema tumepoteza kabisa welekeo!

Mtu mjinga, asiye na akili, akifeli kwenye jambo lake lolote atatafuta kisingizio. Na mara zote hurushia lawama kwa wengine. Chadema tumefeli! Kwenye uchaguzi huu 2020 tumefeli.

Kwamba tuliibiwa, kwamba tulikosa fedha, kwamba tulizidiwa na masababu yote hayo lakini output ni failure! Tusitafute mchawi nje, sisi wenyewe ndani. Lazima kujitafakari upya. Tatizo ni kiongozi mkuu wa chama.

Kuna damu changa yenye akili inayo chemka, wapewe usukani. Hii tabia ya kung’ang’ania madarakani hata kama boti limezama mwanaume bado uko tu na usukani ukidhani mashetani wataibuka kukuibua ni uzembe wa mawazo.

Mbowe kwenye chama hiki ni jabali, mpiganaji, sio milima miwili au mitatu amevuka na amevusha wengi. Heshima yake lazima ilindwe. Lakini ndio tutakuwa na akili zilezile za kudhani wewe ni bora zaidi na hakuna wa kuongoza chama zaidi yako.

Mimi nampa mbowe miezi mitatu hadi april 2021, atangaze kujiondoa CHADEMA apishe watu wengine na maono mengine na mwelekeo mpya. Hayo ya kusubiri eti mpaka 2024 mbali sana, utabadilishaje mwenyekiti wa chama wakati mna elekea kwenye uchaguzi?

Si ndio ujinga wenyewe huo wa kufelishana, tunajifelisha wenyewe kwa katiba, wenzetu mapema mwenyekiti wao wanamthibitisha mara baada ya uchaguzi ila Chadema tunangojea tume karibia.

Nikisema hivi utaona mjinga anapost we mataga! Hoja kama hizi kila anayetoa hoja makini mnamshambulia. Ni mtu mwenye uchungu na chama anapoona kuna kwa ujinga ulio wazi kabisa, asipopisha mtaniona natoka mzima mzima kumpigia kampeni Rais Magufuli katiba ibadilishwe aongezewe muda na hakuna atakayepinga CHADEMA kwa sababu kama mbowe tunasema ni bora kwenye chama aendelee sasa kwanini tusiseme Magufuli ni bora na aendelee! Miaka mingapi mbowe ni mwenyekiti wa CHADEMA?

Mtei alikuwa mwenyekiti kwa miaka sita(6) tu (1992-1998) Bob Makani akawa mwenyekiti tena miaka sita tu (1998-2004) kisha Mbowe akachukua kijiti hadi leo miaka sasa ngapi 22 tunakwenda yupo tu. Sasa kwanini Rais Magufuli asipewe mingine kumi? Kuna ubaya gani? Kama tabia ndio hii ya kuamini kwamba huyu ni bora kuliko wengine.

Mimi sidhani kama ishu ya Rais Magufuli kuongezewa muda CHADEMA tutaipinga, tutaanzia wapi kupinga! Wakati tuko kwenye boti hilo hilo!

Mjue tunahitaji chama makini, mbaya zaidi siku hizi tumekuwa Wizara ya Afya, yaani tunajichora kupita kawaida. Akili ya kiongozi mkuu wa chama ikishachoka hakuna ujenzi wa chama wala mbinu mpya, zile alizokuwa nazo zote zimegonga mwamba na kabakia kurukia maneno na matamshi ambayo baadae anachoreka!
Mawazo uwa yanaheshimiwa ila yanapingwa vile vile.
- Nani aliengua wagombea wa vyama vya upinzania bila sababu za maana. (Serikali za mitaa na uchaguzi mkuu)​
- Nani aliohakikisha mawakala wa vyama pinzani hawapati nafasi ya kutimiza wajibu wao.​
- Nani alihakikisha form za matokeo katika vituo vya kupigia kura haziwafikii mawakala wa vyama vya upinzani ili wakose ushahidi wa kukata refaa.​
- Nani alikumbusha kuwa unalipwa vizuri, gari nzuri nyumba ya serikali alafu umtangaze mpinzani kushinda utakiona cha moto.​
- Nani alizuia critical international observers na asasi huru za kijamii.​
- Nani alihakikisha watu hawapashani habari kuhusu mwenendo mzima wa uchaguzi.​
- Nani alihakikisha vifurushi vya kura nje ya chumba cha kupigia kura vinakuwa sehemu ya hesabu.​
- Nani alihakikisha media zote za umma na binafsi hazitoi nafasi kwa vyam vya upinzani.​
- Nani anahakikisha sheria ya vyama vingi haitekelezwi kwa kupiga nmarufuku mikutano / maandamano ya vyama vya upinzani.​
- Nani anahakikisha kuwa watu watakao thubutu kuchagua wapinzani huduma ya umma wasipelekewe kabisa japo wanalipa kodi vile vile.​
Ni hayo tu kwa leo. karibu lunch mkuu.​
 
Sababu ya kuibiwa kura inasisitizwa ili agenda ya Uongozi na mabadiliko kuimarisha upya chama yasizungumzwe wakati hali ni mbaya.

Uchaguzi umepita kuibiwa tayari tumeibiwa jee tung'ang'anie kuibiwa kura kuwa ni agenda ya kila siku mpaka 2025?

Tutafute njia ya kuimarisha chama hali ni mbaya na viongozi katika kanda nyingi au hawatoi huduma ya kuendeleza Chama ama kuzembea na kisingizio ni hali ya kipesa hoi chamani.
 
Back
Top Bottom